WAZIRI LUKUVI NJOO USOME HAPA

boyskillz

Senior Member
Apr 29, 2013
109
104
Kuna watu wamenihoji mtazamo Wangu kuhusu ile bomoa bomoa inayoendelea maeneo mbali mbali hapa jijini Dar es Salaam.

Ndugu zangu si jambo zuri au la kawaida kuona nyumba yako au yenu ikiangushwa chini na wakati huo hauna sehemu ya kujishikiza kwa hiyo itakulazimu ulale nje.

Sipingi wala sizuii serikali kufanya ilichokusudia lakini NAPINGA kwa namna moja au nyingine njia wanazo tumia katika kuziondosha nyumba hizo na wakazi hao.

My take
Kama serikali inaamua kuwaamisha wananchi eneo fulani basi sio kuwalipa pesa na viwanja Bali ni serikali yenyewe iingie jukumu la kwenda kuwajengeja wananchi nyumba kwanza eneo wanaloona linastahili iwakabidhi kisha ndo ikabomoe maeneo yasiyotakiwa kuwapo makazi.

Kwasababu serikali si wanaamini kwamba fidia ile wanayolipwa wakazi inatosha basi serikali yenyewe ikajenge kwanza nyumba hizo kwa hio fidia wanayoiamini ni stahiki kisha wakawagawie wananchi nyumba na sio kiwanja ama pesa kwa sababu nyumba haikamiliki siku moja ukahamia

Ingekuwa ni vyema hatua hizo pia zingechukuliwa hapa Dar kwanza ndo wazibomoe nyumba hizo wanazosema zipo kwenye vyanzo vya maji.

Wanatuambia maeneo hayo hayafai kuwapo na mkazi yoyote! Naomba tujiulize kama wanafahamu hayafai mbona katika kampeni walienda huko huko pasipofaa kubembeleza wakazi wa maeneo hayo ambao Leo wameonekana wadhambi katika macho ya mkuu wa mkoa na waziri wake.

Kwanini serikali ilipeleka umeme maeneo hayo yasiyofaa? kwanini walipeleka huduma zingine za kijamii na wanajua hayafai? Kwanini waliweka hata ofisi za Mtendaji? Kwanini walitoa vibali wananchi wajenge hko? Na mbona ule mradi wao wa mabasi yaendayo kasi bado umepita huko? Kwanini walienda kufanya kampeni maeneo yasiyofaa? Mkuu wa mkoa atujibu maswali haya machache tu.

Kinacholiliwa sasa hivi na wananchi hawa sio nyumba hizo Bali ni mstakabali wa maisha yao, kuna watoto wadogo kabisa hata wengine hawajaanza kutambaa,kuna vikongwe wasiojiweza, kuna wanafunzi hko kuna watu wengine wamepoteza vyeti vyao vya elimu kwa sababu bomoa bomoa ilipokumba maeneo hayo wao walikua makazini.

Naamini serikali ni sikivu iliangalie upya swala hili wajenge kwanza nyumba maeneo yanayostahili wawape wananchi.

Mwisho, Nampongeza Mh. Mbunge aliyeenda kutetea wananchi wake mahakamani na akatuonesha kwa kuna UTAWALA wa sheria nchini kwetu tuachane na Mambo ya KUKURUPUKA.
Namuombea ashinde kesi hio japo ime base maeneo machache.

Eng Enock Ally
 
Kuna watu wamenihoji mtazamo Wangu kuhusu ile bomoa bomoa inayoendelea maeneo mbali mbali hapa jijini Dar es Salaam.

Ndugu zangu si jambo zuri au la kawaida kuona nyumba yako au yenu ikiangushwa chini na wakati huo hauna sehemu ya kujishikiza kwa hiyo itakulazimu ulale nje.

Sipingi wala sizuii serikali kufanya ilichokusudia lakini NAPINGA kwa namna moja au nyingine njia wanazo tumia katika kuziondosha nyumba hizo na wakazi hao.

My take
Kama serikali inaamua kuwaamisha wananchi eneo fulani basi sio kuwalipa pesa na viwanja Bali ni serikali yenyewe iingie jukumu la kwenda kuwajengeja wananchi nyumba kwanza eneo wanaloona linastahili iwakabidhi kisha ndo ikabomoe maeneo yasiyotakiwa kuwapo makazi.

Kwasababu serikali si wanaamini kwamba fidia ile wanayolipwa wakazi inatosha basi serikali yenyewe ikajenge kwanza nyumba hizo kwa hio fidia wanayoiamini ni stahiki kisha wakawagawie wananchi nyumba na sio kiwanja ama pesa kwa sababu nyumba haikamiliki siku moja ukahamia

Ingekuwa ni vyema hatua hizo pia zingechukuliwa hapa Dar kwanza ndo wazibomoe nyumba hizo wanazosema zipo kwenye vyanzo vya maji.

Wanatuambia maeneo hayo hayafai kuwapo na mkazi yoyote! Naomba tujiulize kama wanafahamu hayafai mbona katika kampeni walienda huko huko pasipofaa kubembeleza wakazi wa maeneo hayo ambao Leo wameonekana wadhambi katika macho ya mkuu wa mkoa na waziri wake.

Kwanini serikali ilipeleka umeme maeneo hayo yasiyofaa? kwanini walipeleka huduma zingine za kijamii na wanajua hayafai? Kwanini waliweka hata ofisi za Mtendaji? Kwanini walitoa vibali wananchi wajenge hko? Na mbona ule mradi wao wa mabasi yaendayo kasi bado umepita huko? Kwanini walienda kufanya kampeni maeneo yasiyofaa? Mkuu wa mkoa atujibu maswali haya machache tu.

Kinacholiliwa sasa hivi na wananchi hawa sio nyumba hizo Bali ni mstakabali wa maisha yao, kuna watoto wadogo kabisa hata wengine hawajaanza kutambaa,kuna vikongwe wasiojiweza, kuna wanafunzi hko kuna watu wengine wamepoteza vyeti vyao vya elimu kwa sababu bomoa bomoa ilipokumba maeneo hayo wao walikua makazini.

Naamini serikali ni sikivu iliangalie upya swala hili wajenge kwanza nyumba maeneo yanayostahili wawape wananchi.

Mwisho, Nampongeza Mh. Mbunge aliyeenda kutetea wananchi wake mahakamani na akatuonesha kwa kuna UTAWALA wa sheria nchini kwetu tuachane na Mambo ya KUKURUPUKA.
Namuombea ashinde kesi hio japo ime base maeneo machache.

Eng Enock Ally


Hili Hapa Chini ni TAMKO la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam!

Mkuu wa Mkoa Wa Dar Atoa Tamko

Wakati mahakama kuu ikisimamisha zoezi la bomoa bomoa, Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Said Meck Sadick amejitetea na kukanusha taarifa za upotoshaji ambazo zimekuwa zikitolewa na viongozi wa kisiasa hususani wenyekiti wa mitaa na baadhi ya wakazi wanaoishi maeneo hatarishi ya mabondeni juu ya serikali kuvunja nyumba, ikizingatia kutotoa maeneo mbadala ya kujenga makazi mapya ya kudumu.
Meck sadick amesema mwaka 2011 yalipotokea mafuriko serikali iliwapatia viwanja wakazi waliokuwa na nyumba katika maeneo hatarishi ya mabondeni kwa Wilaya zote tatu za Mkoa Dar es Salaam katika eneo la Mabwepande wilaya Kinondoni.


Kwa mujibu mkuu wa mkoa jumla ya viwanja 1007 viligawiwa kwa wakazi hao wa mabondeni na viwanja vitatu havikugawiwa kwa sababu viliangukia maeneo yasiyofaa kwa makazi.

Aidha sambamba na kupatiwa viwanja wakazi hao walipatiwa misaada ya kibinadamu pamoja na vifaa vya kiujenzi ikiwemo mifuko ya saruji 100 mabati na mbao kila kaya na kuwawekea huduma muhimu za kijamii.

Amesema wakazi hao wamediriki kuuza viwanja vyao kwa bei ya chini na kurudi maeneo waliyokuwa wakiishi awali na wengine kuuza na kupangisha nyumba zao walizojenga mabondeni licha ya Serikali kuwataka waondoke katika maeneo hayo hatarishi.


Vile vile amesema Serikali kwa kushirikiana na halmashauri zote nchini imeanza na inaendelea na zoezi la bomoa bomoa kwa ajili ya kuwaondoa wakazi wote wanaoishi maeneo hatarishi na wale waliovamia maeneo yasiyostahili kujengwa.
Pia amesema zoezi hili la bomoa bomoa litafanyika nchi nzima ambapo kwa sasa limeanzia Mkoa Dar es Salaam na wakazi waliojenga katika maeneo hatarishi wabomoe wenyewe na kuondosha baadhi ya vifaa vya ujenzi ambavyo vitawasaidia kwenda kuendeleza makazi mapya katika viwanja walivyopewa na serikali.
Amewataka wananchi kuacha kuendelea kulalamika wakati wanafahamu kuwa wamevunja sheria licha ya serikali kuwataka kuondoka kabla hawajapata madhara ikiwemo kuvunjiwa nyumba zao.



Sasa ulitata Serikali ifanye nini tena zaidi ya Hapo?
 
Na mshauri mbunge wa kinondoni zitakapopiga mvua za maana ao watu wake wakaathirika basi asisite kwenda mahakamani kuzuia mvua hivo zisiathiri watu wake
 
Barbarossa
Sadiki anasema nyumba zillzofidiwa Ni takribani elfu moja,zinazo bomolewa zaidi ya elfu kumi
that's the crux of it
 
Back
Top Bottom