Richard
Platinum Member
- Oct 23, 2006
- 16,630
- 25,586
Ajali za kila mara zimekuwa ndiyo habari kubwa nchini kwa sasa.
Kule eneo la Mparanga wilayani Mkuranga, kulitokea ajali kubwa na watu 24 wakafariki na wengine 10 kujeruhiwa vibaya.
Juzi kule Mbalizi mkoani Mbeya ajali ingine ikatokea na watu 20 wamefariki na wengine 45 kujeruhiwa vibaya.
Pamoja na kwamba vyanzo vya ajali zote hizi mbili ni mwendo wa kasi na uendeshaji magari usofuata sheria za barabarani, bado uchunguzi unatakiwa ufanyike ili kubaini vyanzo vingine zaidi ambavyo vinasababisha kutokea kwa ajali kama hizi.
Leo hii waziri wa mambo ya ndani mheshimiwa Lugola amevunja mabaraza ya usalama barabarani nchini kote, sidhani kama mheshimiwa waziri ameshauriwa vyema juu ya hili.
Kinachotakiwa kufanyika ni kuangalia muundo wa mabaraza haya kama kunahitajika marekebisho, utendaji wake, bajeti yake ni kiasi gani, ufanisi wa kampeni zake na ni watu wa aina gani wanaunda mabaraza haya.
Akifanya hivyo atabaini kwamba pengine anayahitaji sana mabaraza haya kuliko kuyavunja na kubakia na idara za usalama barabarani ambazo nazo hazijafikia kiwango cha kimataifa.
Ni vizuri mheshimiwa waziri Lugola akafikira tena juu ya hatua yake hii alochukua ambayo hata kama ni kusoma kwa ndani ya masaa 48 yalopita basi atakuwa alikuwa tayari ametoa maamuzi kabla ya kuapishwa.
Kuna haja ya waziri Lugola akaangalia suala la madereva wa magari makubwa na mabasi madogo na kuangalia namna ya kuwasaidia hawa madereva ambao hizo kazi za udereva ndizo ajira zao na wana familia zinazowategemea.
Kama si hivyo, basi madereva hawa huwa wanaacha magari hayo yaendeshwe na wahuni ambayo wakiishakolea bangi vichwani huamua kuendesha watakavyo.
Madereva kutoiva kisawasawa kwa kufahamu sheria za usalama barabarani.
Madereva wanapaswa kufanyiwa mitihani na kupimwa uwezo wao wa kuendesha magari makubwa na mabasi madogo.
Mitihani hii yaani "driver's competency test" inaangalia uwezo wa dereva kukumbuka sheria za usalama barabani na uzingatiaji wa sheria hizo.
Wanapofaulu mitihani hii basi wanapatiwa cheti maalum cha DCT na kinadumu kwa miaka mitano tu na kila baada ya miaka mitano wanafanya mtihani mwingine.
Pia madereva wapimwe hali zao kiafya pamoja na macho baada ya miaka mitatu ili kubaini hali yoyote ya utata kiafya na kama macho yao yana nguvu kuona umbali fulani.
Chuo cha usafirishaji kichunguzwe namna kinavyotoa vyeti vya udereva.
Kwa kuwa chuo hiki ndicho chuo kinachotambulika rasmi na serikali basi kinapaswa kufanyiwa uhakiki wa wasimamizi wake wa mitihani kama kuna dalili za rushwa kutolewa kwa watahiniwa.
Hii itaondoa mashaka makubwa juu ya taasisi hiyo na hata kule VETA na vyuo vingine vya udereva ambavyo pengine havijakidhi hadhi ya kufundisha udereva.
Iundwe taasisi ya udhibiti wa madereva na magari yote.
Ni vizuri serikali ikaunda taasisi maalum mfano wa NIDA ambayo itakusanya taarifa zote za madereva na magari yote.
Kazi ya taasisi hii itakuwa rahisi mno kwa kuwa tayari taarifa nyingi za madereva zitakuwa zipo NIDA kwa wale watanzania lakini madereva wageni watakuwa na kanzi-data yao.
Magari yanapofanyiwa ukaguzi basi taarifa zote badala ya kuwekwa kwenye makaratasi, zoezi zima la ukaguzi linafanywa kupitia mtandaoni na taarifa zinaingizwa moja kwa moja kwenye mfumo wa computer.
Hii itasaidia kubaini magari na madereva wazembe au waso madereva pale wanapopita katika vituo vya ukaguzi.
Dereva anapofika kwenye kituo anaingiza kadi ya DCT na anaingizwa kwenye mfumo ambao itamuangalia atakapokuwa akisafiri na gari hadi anapofika mwisho wa safari.
Hivyo basi pamoja na gari kuwa na kifaa cha kudhibiti mwendo (sifahamu vimeishia wapi) bado anakuwa anafahamu kwamba anaangaliwa namna anavyoendesha gari.
Hali hii itaenda sambamba na udhibiti wa magari kuona ubora wa injini, ubora wa matairi na kama yanafaa kuendelea kutumika baada ya muda fulani.
Kwa mfano taasisi hii itaangalia aina ya matairi yote yanayoingizwa nchini na kwa kuwa bado kiwanda chetu cha general Tyre bado hakijaanza kazi rasmi ya uzalishaji matairi, basi matairi yote kutoka nje yanapaswa kuangaliwa ubira wake na kuthibitka kuwa ni bora kabla ya kutumika kwenye barabara zetu.
Uboreshaji barabara alama za barabani na ufungaji kamera maalum
Hali ya barabara zetu bado si ya kuridhisha na ukiangalia barabara ya Mbalizi ambayo ina mteremko inahitaji kingo maalum, alama za kutosha kuonya madereva kuhusu mteremko huo na kamera maalum kuchukua picha za magari yanayozidisha mwendo.
Alama za barabani bado ni muhimu sana kwa nchi kama ya kwetu na wala alama hizi hazigharimu fedha nyingi kuzitengeneza.
Serikali kupitia kila mkoa ingepanga bajeti maalum kwa kila idara ya usalama barabani kuhakikisha kila mkoa una alama za kutosha za barabani na kamera maalum "speed camera".
Kamera hizi maalum zitaondoa mianya ya rushwa kwa askari wa usalama barabarani ambao huruhusu magari yaendelee na safari ilhali yana matairi mabovu au ubovu mwingine.
Pia kanera hizi zitakuwa zimeunganishwa na mtandao maalum wa internet na picha maalum zikipigwa na gari kuzidisha mwendo, basi taarifa zinakwenda moja kwa moja kituo cha usalama barabani cha mkoa ambao watamshugulikia huyo dereva mkosefu.
Madereva ambao wanapatikana na makossa ya kuzidisha mwendo hupewa faini maalum ambayo watatakiwa kuifuata kwenye kituo cha idara ya usalama barabani na kisha kuipeleka TRA ambako watalipa faini hiyo na kuongeza trilioni zetu za kila mwezi kama mapato ya taifa.
Ifanyike kampeni ya AJALI SASA BASI nchi nzima.
Kwa kuwa wananchi ndiyo waathirika wakuu wa ajali hizi ambazo zinasababisha umauti na watu kupoteza ndugu zao na pia kusababisha ulemavu wa kudumu na matatizo mengine, basi serikali iwashirikishe wananchi kwenye kampeni ya nchi nzima.
Kufanyike kampeni na wananchi wapewe namba maalum ya kuripoti gari yoyote ile inayozidisha mwendo katika barabara yoyote ile na dereva ashitakiwe kwa uzembe au kusababisha ajali.
Narudia kutoa ushauri, Mheshimiwa waziri afikirie tena uamuzi wake wa kuvunja mabaraza ya usalama barabarani.
Kule eneo la Mparanga wilayani Mkuranga, kulitokea ajali kubwa na watu 24 wakafariki na wengine 10 kujeruhiwa vibaya.
Juzi kule Mbalizi mkoani Mbeya ajali ingine ikatokea na watu 20 wamefariki na wengine 45 kujeruhiwa vibaya.
Pamoja na kwamba vyanzo vya ajali zote hizi mbili ni mwendo wa kasi na uendeshaji magari usofuata sheria za barabarani, bado uchunguzi unatakiwa ufanyike ili kubaini vyanzo vingine zaidi ambavyo vinasababisha kutokea kwa ajali kama hizi.
Leo hii waziri wa mambo ya ndani mheshimiwa Lugola amevunja mabaraza ya usalama barabarani nchini kote, sidhani kama mheshimiwa waziri ameshauriwa vyema juu ya hili.
Kinachotakiwa kufanyika ni kuangalia muundo wa mabaraza haya kama kunahitajika marekebisho, utendaji wake, bajeti yake ni kiasi gani, ufanisi wa kampeni zake na ni watu wa aina gani wanaunda mabaraza haya.
Akifanya hivyo atabaini kwamba pengine anayahitaji sana mabaraza haya kuliko kuyavunja na kubakia na idara za usalama barabarani ambazo nazo hazijafikia kiwango cha kimataifa.
Ni vizuri mheshimiwa waziri Lugola akafikira tena juu ya hatua yake hii alochukua ambayo hata kama ni kusoma kwa ndani ya masaa 48 yalopita basi atakuwa alikuwa tayari ametoa maamuzi kabla ya kuapishwa.
Kuna haja ya waziri Lugola akaangalia suala la madereva wa magari makubwa na mabasi madogo na kuangalia namna ya kuwasaidia hawa madereva ambao hizo kazi za udereva ndizo ajira zao na wana familia zinazowategemea.
Kama si hivyo, basi madereva hawa huwa wanaacha magari hayo yaendeshwe na wahuni ambayo wakiishakolea bangi vichwani huamua kuendesha watakavyo.
Madereva kutoiva kisawasawa kwa kufahamu sheria za usalama barabarani.
Madereva wanapaswa kufanyiwa mitihani na kupimwa uwezo wao wa kuendesha magari makubwa na mabasi madogo.
Mitihani hii yaani "driver's competency test" inaangalia uwezo wa dereva kukumbuka sheria za usalama barabani na uzingatiaji wa sheria hizo.
Wanapofaulu mitihani hii basi wanapatiwa cheti maalum cha DCT na kinadumu kwa miaka mitano tu na kila baada ya miaka mitano wanafanya mtihani mwingine.
Pia madereva wapimwe hali zao kiafya pamoja na macho baada ya miaka mitatu ili kubaini hali yoyote ya utata kiafya na kama macho yao yana nguvu kuona umbali fulani.
Chuo cha usafirishaji kichunguzwe namna kinavyotoa vyeti vya udereva.
Kwa kuwa chuo hiki ndicho chuo kinachotambulika rasmi na serikali basi kinapaswa kufanyiwa uhakiki wa wasimamizi wake wa mitihani kama kuna dalili za rushwa kutolewa kwa watahiniwa.
Hii itaondoa mashaka makubwa juu ya taasisi hiyo na hata kule VETA na vyuo vingine vya udereva ambavyo pengine havijakidhi hadhi ya kufundisha udereva.
Iundwe taasisi ya udhibiti wa madereva na magari yote.
Ni vizuri serikali ikaunda taasisi maalum mfano wa NIDA ambayo itakusanya taarifa zote za madereva na magari yote.
Kazi ya taasisi hii itakuwa rahisi mno kwa kuwa tayari taarifa nyingi za madereva zitakuwa zipo NIDA kwa wale watanzania lakini madereva wageni watakuwa na kanzi-data yao.
Magari yanapofanyiwa ukaguzi basi taarifa zote badala ya kuwekwa kwenye makaratasi, zoezi zima la ukaguzi linafanywa kupitia mtandaoni na taarifa zinaingizwa moja kwa moja kwenye mfumo wa computer.
Hii itasaidia kubaini magari na madereva wazembe au waso madereva pale wanapopita katika vituo vya ukaguzi.
Dereva anapofika kwenye kituo anaingiza kadi ya DCT na anaingizwa kwenye mfumo ambao itamuangalia atakapokuwa akisafiri na gari hadi anapofika mwisho wa safari.
Hivyo basi pamoja na gari kuwa na kifaa cha kudhibiti mwendo (sifahamu vimeishia wapi) bado anakuwa anafahamu kwamba anaangaliwa namna anavyoendesha gari.
Hali hii itaenda sambamba na udhibiti wa magari kuona ubora wa injini, ubora wa matairi na kama yanafaa kuendelea kutumika baada ya muda fulani.
Kwa mfano taasisi hii itaangalia aina ya matairi yote yanayoingizwa nchini na kwa kuwa bado kiwanda chetu cha general Tyre bado hakijaanza kazi rasmi ya uzalishaji matairi, basi matairi yote kutoka nje yanapaswa kuangaliwa ubira wake na kuthibitka kuwa ni bora kabla ya kutumika kwenye barabara zetu.
Uboreshaji barabara alama za barabani na ufungaji kamera maalum
Hali ya barabara zetu bado si ya kuridhisha na ukiangalia barabara ya Mbalizi ambayo ina mteremko inahitaji kingo maalum, alama za kutosha kuonya madereva kuhusu mteremko huo na kamera maalum kuchukua picha za magari yanayozidisha mwendo.
Alama za barabani bado ni muhimu sana kwa nchi kama ya kwetu na wala alama hizi hazigharimu fedha nyingi kuzitengeneza.
Serikali kupitia kila mkoa ingepanga bajeti maalum kwa kila idara ya usalama barabani kuhakikisha kila mkoa una alama za kutosha za barabani na kamera maalum "speed camera".
Kamera hizi maalum zitaondoa mianya ya rushwa kwa askari wa usalama barabarani ambao huruhusu magari yaendelee na safari ilhali yana matairi mabovu au ubovu mwingine.
Pia kanera hizi zitakuwa zimeunganishwa na mtandao maalum wa internet na picha maalum zikipigwa na gari kuzidisha mwendo, basi taarifa zinakwenda moja kwa moja kituo cha usalama barabani cha mkoa ambao watamshugulikia huyo dereva mkosefu.
Madereva ambao wanapatikana na makossa ya kuzidisha mwendo hupewa faini maalum ambayo watatakiwa kuifuata kwenye kituo cha idara ya usalama barabani na kisha kuipeleka TRA ambako watalipa faini hiyo na kuongeza trilioni zetu za kila mwezi kama mapato ya taifa.
Ifanyike kampeni ya AJALI SASA BASI nchi nzima.
Kwa kuwa wananchi ndiyo waathirika wakuu wa ajali hizi ambazo zinasababisha umauti na watu kupoteza ndugu zao na pia kusababisha ulemavu wa kudumu na matatizo mengine, basi serikali iwashirikishe wananchi kwenye kampeni ya nchi nzima.
Kufanyike kampeni na wananchi wapewe namba maalum ya kuripoti gari yoyote ile inayozidisha mwendo katika barabara yoyote ile na dereva ashitakiwe kwa uzembe au kusababisha ajali.
Narudia kutoa ushauri, Mheshimiwa waziri afikirie tena uamuzi wake wa kuvunja mabaraza ya usalama barabarani.