Waziri Kigwangalla angalia Jinsi ya kufufua Utalii wa ndani katika Mbuga ya Sanane Island. Tunapoteza mapato.

Zero Hours

JF-Expert Member
Apr 1, 2011
12,944
18,653
Weekend iliyopita niliamua kufanya Utalii wa ndani katika Kisiwa cha Sanane kilichopo Mkoani Mwanza. Niliamua kupeleka Familia yangu ambao kwao ingekuwa ni mara ya kwanza kufika mbuga ya Sanane.

Binafsi nilitembelea hiki kisiwa mara ya mwisho ilikuwa mwaka 2013.
FB_IMG_1592156178607.jpg
FB_IMG_1592156200049.jpg


Hata ivyo sikufurahia sana kulinganisha miaka kama 20 iliyopita.

Nakumbuka hiki kisiwa kilikuwa na vivutio na burudani nyingi sana tofauti na wanyama wachache waliopo hivi sasa kama swala, Mamba, Punda na ngedere .

Nakumbuka sana apo zamani kulikuwa na SOKWE aliyekuwa kivutio kikubwa sana kipindi icho bila Kusahau Simba, mbwa mwitu, Tembo, Tausi na wanyama wengine wengi. Nilikuwa mdogo sana nikiwa na umri wa miaka kati ya 7 hadi 12.

Nakumbuka miaka iyo siku za weekend, mamia ya watu ( asilimia kubwa wakiwa Watanzania) walikuwa wakijazani katika kisiwa hiki wakiburudika na vivutio vingi vya kitalii vilivyokuwa vimesheheni katika mbuga ya saanane.
93473294_526975041528337_6685288447603305122_n.jpg
90427309_900963887005598_5287040032137840018_n.jpg


Sina uhakika kama leo hii hivi vivutio vilirudishwa tena tokea mara ya mwisho kutembelea mbuga hii maana hata wekend iliyopita sikufanikiwa kufika katika mbuga hii. Changamoto kubwa ilikuwa ni Usafiri wa majini kufika katika mbuga hii.


Nilifika ofisini na kuuliza utaratibu ukoje na wakanifahamisha utaratibu mpya uliopo sasa. Na huu utaratibu mpya ndyo ulionifanya nishindwe kufika uko.

Utaratibu hivi sasa ni; unatakiwa kukodi boti private kwa cost ya 59,000 pamoja na 5,900 kama kingilio cha kila kichwa. Huu utaratibu sio kama ule wa zamani ambao kulikuwa na masaa maalumu ambayo boti ilikuwa inaondoka endapo kuna watu au watalii wanaotaka kwenda katika hii mbuga.

Binafsi hii cost ilinikatisha tamaa kabisa. Nikawaambia wanafamilia yanguu hii ni karibia 70,000 si bora tukanunue mbuzi mzima tukamchome tule tufrahie tu maana hata uko tunakoenda kuona sana sana tungeona swala na mamba tu.

Ukilinganisha na cost za zamani hii ni pesa ndefu sana na inadiscourage utalii wa ndani. Mwananchi wa kawaida kama mimi hatuwezi kabisa hizi gharama. Nakumbuka mara ya mwisho 2013 nilienda sanane kwa gharama ya elf 4000 tu.

Kwa hali niliyoona leo katika zile office za mbuga ya Sanane ni kuwa tunapoteza mapato mengi sana amabayo tungepata kutokana na utalii wa ndani katika hiki kisiwa. Yani hakuna watalii na pamedolola tu. Ni kama wale wahudumu wa maliasili ( TANAPA) wanakula tu mshahara wa bure

Kwa muda niliokuwepo pale zaidi ya saa zima, sikuona mtu wala mtalii hata mmoja anayekuja kuuliza kwenda kule. Nilishangaa sana wakati miaka ya zamani, siku za weekend watu waalikuwa wakijazana kuelekea Mbugani. Boti 2 zilikuwa zinapishana yani zinaenda na kurudi zikipeleka na kurudisha watu ( watalii). Serikali ilikuwa ikukusanya pesa nyingi sana wakati ule.

Waziri wa Maliasili na Utalii Dr. Kingwangalla Pamoja na Serikali ya Awamu Ya 5 tunawaomba muangalie jinsi ya kufufua utalii katika kisiwa hiki. Hatuwezi kutangaza utalii wakati sisi wananchi wenyewe tunashindwa kutembelea mbuga zetu za Wanyama.

Hatuhitaji kusubiri Wazungu ndyo waje kutalii mbuga zetu. Hata sisi tunaweza ingiza pato la taifa kupitia utalii wa ndani na kutangaza vivutio vyetu vya utalii.

Ushauri wangu ni, vile vivutio vilivyokuwepo zamani pamoja na huduma na burudani zirudishwe bila kusahau kupunguza gharama ili kuvutia wananchi kutembelea Mbuga ya sanane ili kutangaza kimataifa vivutio vyetu vya utalii.

Ikishindikana apewe mwekezaji binafsi afufue hii mbuga ya Wanyama. Hata mimi mnaweza nibinafsishia hii mbuga muone maajabu.
 
huyo kigwangala unayemtaja saivi roho juu anawaza uchaguzi, je atarudi au laah! kashaanza kuhonga phoenix huko
 
Mkuu hawa TANAPA kwenye kutoa usafiri wa maji kwenye vivutio vyao wameshindwa kabisa. Wakati hilo jambo lipo ndani ya uwezo wao.

Wanaweza wakanunua boti ndogo nyingi kwenye kisiwa cha saa 8 zikawa zinabeba watalii wa ndani kwa bei ndogo kwa trip.Hizo bei wawafanyie wageni wanaoenda kutalii.

Kama wanaweza kununua Land Cruiser Hard Top Series 79 mpya basi hata boti wangenunua 2 kwenye hiyo pesa.
 
Mkuu hawa TANAPA kwenye kutoa usafiri wa maji kwenye vivutio vyao wameshindwa kabisa. Wakati hilo jambo lipo ndani ya uwezo wao.

Wanaweza wakanunua boti ndogo nyingi kwenye kisiwa cha saa 8 zikawa zinabeba watalii wa ndani kwa bei ndogo kwa trip.Hizo bei wawafanyie wageni wanaoenda kutalii.

Kama wanaweza kununua Land Cruiser Hard Top Series 79 mpya basi hata boti wangenunua 2 kwenye hiyo pesa.
I think Tatizo kubwa sio usafiri kwao. Ukienda pale utakuta boat kama tatu hivi za kisasa. Wanadai kwa trip ni watu 15. Zipo tu idle.

Labda hapo nyuma walijikuta wanapata hasara baada ya hizi boat kuondoka kwa ratiba maalum bila kuwa na watu wa kutosha.

Ni kuwa hii mbuga imekosa kivutio cha kushawishi watu kwenda kutalii. Wanachotakiwa ni kurudisha vivutio vilivyokuwepo na kuboresha zaidi na watu watamiminika sana kuliko kusubiri watalii wa kizungu.

Nauhakika bei ikiwa chini ya 4000 kwa kila kichwa, watu watamiminika hata izo boti 3 zitazidiwa kabisa.
 
huyo kigwangala unayemtaja saivi roho juu anawaza uchaguzi, je atarudi au laah! kashaanza kuhonga phoenix huko
Sasa si ndye mhusika hivi sasa hadi octoba mpaka baraza la mawaziri livunjwe.
 
Kisiwa cha saanane hakilipi sisi tunataka sehemu ambayo dollars zinaingia as serengeti NP, Arusha NP, Kilimanjaro NP 😎!

Ndiyo maana wakubwa wote wa TANAPA n.k ni Arusha usikii sijui burigi chato au sahare national park huko hakuna hela ndugu na bahati mbaya now dollars zote zinaenda mfuko mkuu a.k.a hazina kuu 😷!
 
Kigwangalaa hana habari yupo zake jimboni anagawa rushwa illi apitishwe kugombea ubunge
 
Kisiwa cha saanane hakilipi sisi tunataka sehemu ambayo dollars zinaingia as serengeti NP, Arusha NP, Kilimanjaro NP !

Ndiyo maana wakubwa wote wa TANAPA n.k ni Arusha usikii sijui burigi chato au sahare national park huko hakuna hela ndugu na bahati mbaya now dollars zote zinaenda mfuko mkuu a.k.a hazina kuu !



Wabinafsishe sasa waone. Yani kule mtu akijenga zoo, fishing site, beach, swiming pool hotel, camping site, lodge. Ukumbi wa kufanyia sherehe kama harusi, etc...yani wangosha badala ya kujazana kule rock city mal au samaki samaki, watafulika sanane na pesa itaingia mpaka serikali itaona wivu.
 
I think Tatizo kubwa sio usafiri kwao. Ukienda pale utakuta boat kama tatu hivi za kisasa. Wanadai kwa trip ni watu 15. Zipo tu idle.

Labda hapo nyuma walijikuta wanapata hasara baada ya hizi boat kuondoka kwa ratiba maalum bila kuwa na watu wa kutosha.

Ni kuwa hii mbuga imekosa kivutio cha kushawishi watu kwenda kutalii. Wanachotakiwa ni kurudisha vivutio vilivyokuwepo na kuboresha zaidi na watu watamiminika sana kuliko kusubiri watalii wa kizungu.

Nauhakika bei ikiwa chini ya 4000 kwa kila kichwa, watu watamiminika hata izo boti 3 zitazidiwa kabisa.
Hata wakiweka hiyo bei ya 4000 watashawishi sana watu wengi waende.
Boti hizo hazina utumiaji mkubwa wa mafuta. Wao itakuwa wamelenga kupata pesa ndefu zaidi ila sio kufanya watu wengi waende.
 
Back
Top Bottom