Wazazi Wanapozeeka

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,446
Reaction score
829,814
Waache wazeeke kwa upendo uleule waliokulea nao.

Waruhusu waongee na wasimulie hadithi tena na tena kwa subira na shauku ile ile waliyokusikiliza ukiwa mtoto. Waache wawe washindi, kwani mara nyingi walikuacha ushinde hata kama hukustahili ushindi
.

Waache wafurahie marafiki zao, wazungumze na wajukuu zao... Waache wafurahie kuishi kati ya vitu ambavyo vimeambatana nao kwa muda mrefu, kwa sababu wanateseka wakati wanaona kuwa vipande vya maisha yao vimeng'olewa.

Waache wafanye makosa, kama ulivyofanya mara nyingi... Waache waishi na kujaribu kuwafurahia kwenye sehemu ya mwisho ya safari yao, kama vile walivyokushika mkono ulipoanza yako.

Wape support wafikie mwisho mwema! Watakuwa walinzi wako kiroho kwenye ulimwengu usioonekana watakapokuwa ni roho mautini nje ya mwili uharibikao..



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Brother mbona una nondo mno? Why?
 
Hapo ndipo malipo na pa kupokea baraka tele Asante kwa neno la busara.
 
Wazazi wanapo zeeka. Kuna mengi ya kujifunza toka kwao.
Kuna vitu walivyo viona, kwako huto viona na vikitokea tena!Uliza wazazi walivikabili vipi?
Enyi watoto wa Elifuumbili, kaeni kwa wema na wazazi wenu..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…