T14 Armata
JF-Expert Member
- Mar 7, 2017
- 13,798
- 46,706
Mwisho anapeleka aibu nyumbaniMwisho atataka kupata hata mtoto ,mwisho kabisa atataka awe na pumzi tu ,,
Kiongozi kuna jumuiya tumeanzishaNinakesha nikiomba my daughter a master mpaka PhD.
Wazazi tunatofautiana sana.
Umemaliza kila kitu. Hata mimi nina ushuhuda wa mabinti wengi wanaoishi kimaskini kwa kuharakia ndoa.Mabinti wote niliograduate nao chuo na kuolewa haraka wanaishi maisha duni. Cha ajabu wote walikuwa watumishi na watu wa imani, kasoro gumegume mmoja aliolewa na mzungu kibabu ana miaka kama 65 wako Marekani kwa sasa.
Hao walioolewa hawajapata kazi hadi sasa, na maisha sio mazuri kivile ukizingatia elimu yao hawajaitumia ama kuajiriwa ama kujiajiri. Kuna ambao nina ushahidi wanajutia na mwingine nimemchangia gharama za hospitali.
Mtu kamaliza chuo hajaenda intervie yoyote, hajaajiriwa au kujiajiri. Huyo mbio kafunga ndoa. Hapo ana honeymoon, akitoka analea mume, akitoka anapewa mimba, analea mimba, anajifungua, analea kichanga. Baada ya hapo tiyari hatakiwi kukaa mbali na mtoto, hawezi tena kuwa free kwenda interview siku ya interview mtoto anaamka anaharisha.
Unakuta hamna hamna miaka miwili imekatika wapo tu hamna hatua wamefanya. Familia changa inakula hela balaa, gharama za maisha zimepanda. Mke elimu anayo ila kazi hana.
Nashauri binti ukimaliza chuo focus kwanza kuwa na chochote cha kuingiza kitu. Ajiriwa kwanza, hivi nani atakuajiri private sector ukiwa na mtoto wa miezi 6 kila siku una dharura? Alafu entry level opportunities zina mizunguko mingi huiwezi ukiwa na ndoa changa na watoto wadogo.
Kazi za serikali chache. Unless uhakikishe unayeolewa naye anaweza cover kila kitu, mna nyumba na bima na cashflow ya kueleweka.
Halafu anakuja kuwa mama ntilie.Ninakesha nikiomba my daughter a master mpaka PhD.
Wazazi tunatofautiana sana.
Destine ya mtoto wa kike awe na kazi au hana kazi ni kupata mme! Stability ya binti ni mme! Utake/usitake hata kama wewe baba uko vizuri lakini ukiona binti yako yupo yupo tu ni shida! Tatizo ni kupata mme sahihi vinginevyo akiangukia kwa wavuta bangi ni shida zaidi!Habari!
Nilipomaliza chuo nilipatwa na mkasa. Ile nimemaliza tu mitihani nikamtaarifu mama, tukaongea tu vizuri kwa muda mfupi chumbani kwake, sasa wakati natoka nje akaniuliza swali 'kwahiyo ushapata mtu wa kukuoa?' moyo ulishtuka halafu chap nikaendelea na safari hapo nikajifanya sijamsikia.
Ikawa wimbo anaoupenda 'ushapata wa kukuoa? Nikawa namwambia sipo tayari kwa sasa nikimjibu hivyo anaanza kutoa risala 'unajua inabidi uolewe mimi najisikia vibaya kukuona tu hapa nyumbani'
Siku moja nikamwambia mimi sijapata hata wa kunioa, akasema 'uzuri wote huo hakuna aliyesema anataka kukuoa' ilibidi tu nicheke mimi nilikua nishasoma akili yake kwamba uoga wa maisha unamsumbua
Ishapita miaka 3 tokea kisa hiki kitokea, juzi nikasema acha niwaulize wenzangu kama wanakutana na maswahibu kama yangu sababu huu wimbo mama angu bado anauimba
Rafiki yangu FLORA
Yeye aliniambia alivyomaliza Mitihani alichelewa kurudi nyumbani kwa miezi kadhaa, sasa kuna siku akaumwa akalazwa mama yake alivyoenda hospital akamkuta Flora yupo na boyfriend wake ila huyo bf akawapisha waongee
Mama ake akamuuliza 'huyo kijana ni nani' Flora akamjibu ni rafiki yake.
Mama ake akamwambia bills ni kiasi gani ili alipie! Flora akamwambia 'rafiki yangu ameshalipia' mama yake akaguna
Sasa Flora alivyorudi kwao, mama yake akaanza kuimba nyimbo kila mara 'Yule rafiki yako yuko wapi akuoe kuliko kushinda ndani kila siku' Flora akaishia tu kucheka.
Rafiki yangu REBECCA
Yeye alikua anabanwa sana, ni wale watoto geti kali. Alivyomaliza chuo kuna siku akamuomba mama yake ruhusa ya kwenda kumsalimia rafiki yake.
Mama yake hakumuuliza maswali mengi kama alivyokua anafanya hapo awali.
Jioni mapema Rebecca aliporudi mama yake akamwambia 'Mbona umerudi mapema' akamjibu nilienda kumuona tu mara moja
Mama yake akamwambia 'Ebu tembeatembea wachumba wakuone sio kujifungia tu ndani'
Ila ameniambia huo wimbo mama yake aliuacha baada ya yeye kupata kazi.
Rafiki yangu ASHA
Huyu ndiye amenichekesha sana, anasema tulivyomaliza chuo baba yake akawa anamwambia 'fanya uolewe sitaki kukuona nyumbani kwangu'
Kuna siku akaenda kazini kwa baba yake akamkuta yupo na wanaume wengine akawasalimia.
Kijana mmoja akamwambia mzee wake kwamba akujua kama ana binti mkubwa vile! Mzee wake akajibu 'Huyu ni binti yangu kamaliza chuo mwaka huu na bado hajaolewa' wote wakaishia kucheka.
Haikupita miezi mingi baba yake akamletea mchumba, ubani ukachomwa sasa hivi yupo kwenye ndoa.
Nilichokiona wazazi wengi ambao hawajajipata kazi wanayotupa watoto wa kike ni kuolewa tena kama mtoto hajapata kazi ya kufanya.
Ila ukiwa na kazi nzuri unapata pesa, hii risala ya kuolewa hawatoi hata ukifikisha miaka 40.
Sasa sijui wa kulaumiwa ni CCM, wazazi wetu au sisi watoto.
SikweliIla ukiwa na kazi nzuri unapata pesa, hii risala ya kuolewa hawatoi hata ukifikisha miaka 40.
mjini shule, usitamani vyote vimelipiwa,Nikiomba nije kwenu unarukaruka kama pop corn kumbe bi mkubwa ashanichungulia kwenye darubini anaona kabisa chalii yule pale ndio mkwe.
Hahahahaha, boda boda wanajipigia tu usikuteMwisho anapeleka aibu nyumbani
Una miaka mingapi ?Binafsi sijawahi kuulizwa hili swali na mtu yoyote yule wa familia yangu.
Braza unazingua kishenz...Yani ni Hahahahah😂😂Hahahahaha hongera zake, na alivyo mzuri sasa yule binti
Bado kwani una miaka mingapi ?Sina mpango wa kuolewa, sifikirii hata kwa sasa
Yaani kuhusu ndoa mimi bado sana..!
Hata mtoto wa kiume yuko vizuri kuoa alafu anazingua ni shida! Kijana akiwa na uwezo alafu hana mke kama baba ni shida! Popote uendako! Stability ya kijana/binti ni kuwa na mwenza! Ebu fikiria kijana/binti ana kipato cha kutosha na hana mwenza uwe na uhakika anaishi maisha ya ushetani kusagana, mashangazi/michepuko! Kama wewe mzazi uwezi kulichukulia kwa uzito umeishafail ukiletewa wajukuu wasioeleweka usipige kelele! At least try to do something!Ukiona mzazi analazimisha mambo hamtakii mema mwanae hii si sawa jamani 😂😁 hata Mimi mwaka juzi nililazimishwa kuletewa mke now nimemuacha Kila mtu Aishi maisha yake kulazimishana sio vizuri kuoa anu kuolewa ni jambo ambalo Lina hitaji mda sana Cc ephen_