ng'adi lawi
JF-Expert Member
- Sep 27, 2014
- 2,956
- 1,115
Matokeo ya uchaguzi wa rais wa Zanzibar hayajatangazwa lakini watu wote wauminifu wanakiri kuwa mgombea wa CUF alishinda. Hivi kuna hofu gani kwa Rais Shein kuwa makamu wa kwanza wa Rais katika serikali ya umoja wa kitaifa? Maalim Seif aliahidi kwenye kampeni kuwa akishinda ataifanya Zanzibar kuwa Singapore au Dubai ya East Africa. Kwa nini msimjaribu? Sote tunajua kuwa Singapore na Dubai ni miji maarufu kwa biashara na bandari zenye eneo la kuweka na kuuza bidhaa za nchi zote duniani(Free Port). Mpeni Maalim Seif hiyo miaka mitano alete wawekezaji ili tusiende tena Dubai kwa shopping. Au hamtaki kuwa matajiri?