Waume na wake za watu,hawajijui?

Waume na wake za watu,hawajijui?

Eiyer

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2011
Posts
28,259
Reaction score
20,914
Kilichonifanya nijiulize maswali ni mambo na ukatili unaotaka kumtokea kijana huyu.
'
Huyu kijana ni mwanafunzi wa SAUTI,anaishi nyumbani kwao,yaani kwa baba yake na mama yake.
'
Jirani na anapoishi kuna mama ambae anamtaka huyu kijana kimapenzi,lakini kijana amekua akikataa.
'
Tatizo linakuja baada ya mume wa mama yule kuambiwa kuwa kijana yule "anatembea" na mkewe.
'
Mume badala ya kuhoji na kujua nini ni nini,amemfuata kijana yule na kumwambia atamfanya kitu ambacho hatasahau kwa "kutembea" na mkewe.
'
Kijana amechanganyikiwa.
'
Ninachotaka kuwauliza hawa wake za watu na waume ya watu ni kuwa hawajijui?
'
Kuna vijana wa kike na kiume wamejikuta wakiingizwa kwenye matatizo na hawa wake na waume za watu.
'
Unapomshawishi kijana wa kik au wa kiume na kumuingiza kwenye mahusiano haramu,unajua unachokifanya?
'
Kuna vijana wengi wamejikuta wamehama miji kwa sababu hii.Na hawa wenza nao wanaposikia mume au mke anangonoka na kijana au binti fulani huenda kuwaadhibu hawa vijana bila kujiuliza kama binti au kijana huyo ana uwezo wa kumtongoza mume au mke wako.
'
Hawa vijana wamekua wahanga wa hawa wake na waume za watu wasiokua na staha.
'
Adhabu kama vipigo,kuswekwa rumande,kumwagiwa maji ya moto n.k zimekua zikiwapata sana wakati wao ndo unakuta walilazimishwa kuingia kwenye uhusiano huo.
'
Hebu wahurumieni!
 
Hao vijana nao hawajitambui, hapa naona wote ni uozo tuu, ikiwa mke anatoka nje ya ndoa anaepaswa kulaumiwa ni mume na wala si yule anaetembea na mkeo coz inaashiria hujtimizi majukumu yako katika ndoa na vivyo hivyo kwa mume anaetoka nje ya ndoa , cha msingi wanandoa waheshimu ndoa zao na vijana nao watafute wapenzi wa marika na sifa kama zao ukiona mke au mume wa mtu anakuzingua mwambie mkewe au mumewe umalize mchezo ila kama unamega mke au mume wa mtu kipigo ni halali yako coz wewe si mwizi bana, au mnataka tuhalalishe wizi kwa kisa tu anaeiba ni kijana...............
 
Huwa hawatafuti chanzo ila wanakimbilia kwenye tukio na always ni yule kijana aliyesemekana ametembea na mke wake
Huwa hawahangaiki na wake zao au kutaka kujua ilianzaje mpaka yakatokea hayo ya mke wake kutembea na kijana wa watu ila wanawakimbilia wale vijana kuwaambia kuwa wao ndio wametembea na wake zao
tatizo ni kubwa kuna sehem ambazo kwa kweli vijana kwa kupenda maisha mepesi wameingia kwenye mtego wa kuwatamani wake za watu na kutembea nao na pengine ni hayo ya wamama kuwataka vijana wadogo bila kujali kuwa wameolewa na wana waume zao
 
Hakuna kijana anayelazimishwa kutembea na mke wa mtu. Ukiona mpaka unahisiwa ujue na wewe umekaribisha mazoea ya kijinga mpaka mnafikia kufikiriwa vibaya. Mwanamke siku zote ana akili za mashaka linapokuja suala la dhambi
 
Hao vijana nao hawajitambui, hapa naona wote ni uozo tuu, ikiwa mke anatoka nje ya ndoa anaepaswa kulaumiwa ni mume na wala si yule anaetembea na mkeo coz inaashiria hujtimizi majukumu yako katika ndoa na vivyo hivyo kwa mume anaetoka nje ya ndoa , cha msingi wanandoa waheshimu ndoa zao na vijana nao watafute wapenzi wa marika na sifa kama zao ukiona mke au mume wa mtu anakuzingua mwambie mkewe au mumewe umalize mchezo ila kama unamega mke au mume wa mtu kipigo ni halali yako coz wewe si mwizi bana, au mnataka tuhalalishe wizi kwa kisa tu anaeiba ni kijana...............

Hapa vijana lawama zinawaepuka kwa kuwa hawa wake na waume za watu hutumia ubabe,fedha na uzoefu wa kimaisha kuwarubuni hawa vijana.Hivyo wanajikuta wanafanya bila ridhaa yao!
 
Hakuna kijana anayelazimishwa kutembea na mke wa mtu. Ukiona mpaka unahisiwa ujue na wewe umekaribisha mazoea ya kijinga mpaka mnafikia kufikiriwa vibaya. Mwanamke siku zote ana akili za mashaka linapokuja suala la dhambi

Una uhakika kuwa mwanamke ana akili za mashaka?Pia sijaelewa una maana gani unaposema hakuna kijana anaelazimishwa kufanya ngono na mke wa mtu,hebu fafanua hapo!
 
hata wewe hauna uhakika lkn kinacho takiwa hapo kwa huyo mwanaume anatakiwa ku2mia hekma na busara
 
Hapa vijana lawama zinawaepuka kwa kuwa hawa wake na waume za watu hutumia ubabe,fedha na uzoefu wa kimaisha kuwarubuni hawa vijana.Hivyo wanajikuta wanafanya bila ridhaa yao!

Kabla sijakupa muongoza wa mada yako, nikujibu hii hoja kuwa hakuna mtu mzima anayejikuta amefanya umalaya bila ridhaa yake. Ni ukosefu wa uwepo wa Mungu katika maisha yetu ndio unatufanya tushawishike kufanya dhambi.
Fuatilia hekima hii


Mwanagu, shika maagizo ya baba yako,
wala usiache sheria ya mama yako.

Yafunge hayo katika moyo wako daima,
jivike hayo shingoni mwako.

Uendapo yatakuongoza, ulalapo yatakulinda,
na uamkapo yatazungumza nawe.

Maana maagizo hayo ni taa, na sheria hiyo ni nuru,
na maonyo ya kumwadilisha mtu na njia ya uzima.

Yakulinde na mwanamke mwovu, asikupate,
na kukuponya na ubembelezi wa mgeni.

Usiutamani uzuri wake moyoni mwako,
wala usikubali akunase kwa kope za macho yake.


Maana kwa malaya, mtu hutiwa katika hali ya kuhitaji kipande cha mkate,
na kahaba humuwinda mtu anase nafsi yake iliyo ya thamani.

Je mtu aweza kutia moto kifuani pake,
na nguo zake zisiteketee?

Je mtu anaweza kukanyaga makaa ya moto,
na nyayo zake zisiungue?

Ndivyo alivyo aingiaye kwa mke wa jirani yake,
kila mtu amgusaye huyo atakuwa na hatia.

Watu hawamdharau mwivi,
akiiba na kusihbisha, iwapo aona njaa

lakini akipatikana atalipa mara saba,
atatoa mali yote ya nyumba yake.

Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa,
afanya jambp litakalomwangamiza nafsi yake.


Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima,
wala fedheha yake haitafutika;

maana wivu ni ghadhabu ya mtu,
wala hatahurumia siku ya kujilipiza kisasi;

hatakubali ukombozi uwao wote,
wala hatakuwa radhi, ujapomlipa vitu vingi.


Mithali 6:20-35


Mkuu, huwezi kukwepa lawama kwa kuwa ulisikiliza maneno ya Mwanamke. Wewe mwanaume uliumbwa, ukapewa ufahamu zaidi ya mwanamke, sasa iweje leo usilaumiwe kwa kuwa eti ulishawishiwa na mwanamke?!

Hapo kwenye Mithali 6:29, unaambiwa kila amgusaye mwanamke malaya (anayemsaliti mume wake), naye ana hatia. Kukosa kwako uadilifu, si kosa la mtu mwingine ndio maana Hekima anatuambia ''shika maagizo ya baba yako, wala usiache sheria ya mama yako''.

Eva alipompotosha Adama akavunja agano na Mungu, Mungu hakumuadhibu Eva peke yake, aliwaadhibu wote. Adam alijitetea kuwa mwanamke uliyenipa ndiye aliyenipotosha, lkn je, maagizo ya Mungu na maneno ya Eva yepi yalipaswa kufuatwa? Kwa hiyo utaona kuwa hakuna excuse kwa dhambi utakayofanya na kusingizia ulishwawishiwa.

Jihadhari na mienendo ya mwanamke, kwani ukamilifu wake u mashakani tangu kuumbwa kwake.

Mwanzo wa dhambi ulitoka katika mwanamke,
na kwa sababu yake sisi sote tunakufa.

Yoshua bin Sira 25:24
 
Hao vijana nao hawajitambui, hapa naona wote ni uozo tuu, ikiwa mke anatoka nje ya ndoa anaepaswa kulaumiwa ni mume na wala si yule anaetembea na mkeo coz inaashiria hujtimizi majukumu yako katika ndoa na vivyo hivyo kwa mume anaetoka nje ya ndoa , cha msingi wanandoa waheshimu ndoa zao na vijana nao watafute wapenzi wa marika na sifa kama zao ukiona mke au mume wa mtu anakuzingua mwambie mkewe au mumewe umalize mchezo ila kama unamega mke au mume wa mtu kipigo ni halali yako coz wewe si mwizi bana, au mnataka tuhalalishe wizi kwa kisa tu anaeiba ni kijana...............

Mbona unaji-contradict aisee?? Kipigo cha ninii sasa? Si asepe tu?
 
Back
Top Bottom