Julius Kaisari
JF-Expert Member
- Oct 12, 2010
- 1,176
- 675
Amakweli, imefikia hatua watz tunatia imani..Ndiyo,tunatia huruma. Tunahitaji neema ya kina Rostam,Mkono,Lowasa kutuhurumia.. Yaani kwa ufupi ni kama yatima fulani.. Yule wakili mwizi, wakiri wa mafisadi, mtengeneza madili, tajiri mwenza wa tapeli RA,EL, yule mshirika wa kukwiba mafweza BoT,leo anatuonea imani watz,? Yaani kuiba waibe wao,kutapeli watapeli wao, mali na Fedha,na rasilimali za watz, Leo baada ya kubwabwaja kwingi kwa kina kubenea,tanzania daima,JF,mashirika ya kijamii yenye nia njeama,CDM, wote wenye uchungu na umasikiniwa nchi yetu yenye utajiri tele, leo anaibuka shujaa wa kututtetea? Ama kweli vya MLEVI HULIWA NA MGEMA!