KakaKiiza
JF-Expert Member
- Feb 16, 2010
- 11,457
- 8,295
Mimi ninawaasa hasa Watumishi waserikali wote waliopo madarakani kuachana na kujihusisha na ushabiki wa siasa!!hasa waliokwenye vyombo vyenye maamzi yasiyokuwa rasimi na yaliyokuwa rasimi!!Siasa ni kamali!!na nina washauri msione wapinzani kama wahaini ni wapinzani kwakuwa Tanzania imechagua mfumo wa vyama vingi!!Leo hii nipo mimi mwanachama wa chama Tawala lakini kesho yupo mwanachama wa chama cha Upinzani madarakani!!Nasema hivyo kwa sababu hizi wale wote waliokuwa wakimbeza Maalim Seif sharrif!Leo hii ni makamo wa wakwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar!!je wewe mtumishi wa serikali uliyekuwa ukimwona kama mhaini na ukawa unambeza je leo ukipangwa kufanya kazi kwenye ofisi yake utafanyeje au utaacha kazi??Hivyo jifunzeni kutokana na historia!Leo hi makamanda wa polisi unguja na Pemba wanamuogopa kwa yale waliyomfanyia mwaka mwaka huo kule zanzibar wanakosa raha wanajiuliza leo wakipangiwa kufanya kazi naye watapishana vipi naye watampigia vipi saluti??wakati walisha hapa kwamba hawawezikumpigia salute raia??Leo naona niishie hapo watumishi watakuwa wamenielewa nini ninamaanisha!!Asanteni!!