Hivi ni kweli kwamba watu waliosoma maths kwa angalau ngazi ya kidato cha 5 na 6 wana uwezo mkubwa wa kufikiri na kuchanganua mambo ukilinganisha na wale waliosoma masomo ya Art kama Kiswahili!?
Ni kweli, mbali na kuchanganua mambo hata unapoongea nao na kuwauliza maswali huwa wanatoa majibu kwa haraka sana bila kujali jibu ni sahihi au sio sahihi.
Mkuu kwa taarifa yako somo la Economics limejaa hesabu za nguvu,kama hesabu haipandi kichwani mwako huwezi kufaulu somo/shahada ya ECONOMICS. Hesabu ndio kila kitu Duniani.
Ndilo tatizo lao kubwa, na wengi wao waliopewa Uongozi ndio wametuharibia Taifa letu kimadili,akili zao masaa yote zinafikiria ma deal tu na matanuzi!!
Tushukuru Mungu kwa kumuwezesha mwanasayansi mwenzetu kuongoza Taifa letu - nina imani ataleta mabadiriko makubwa sana yenye Tija.
Hivi ni kweli kwamba watu waliosoma maths kwa angalau ngazi ya kidato cha 5 na 6 wana uwezo mkubwa wa kufikiri na kuchanganua mambo ukilinganisha na wale waliosoma masomo ya Art kama Kiswahili!?