Mfikirishi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 7,495
- 8,539
Huu mtindo wa wateule kuja hadharani na kujisifia kwa teuzi wanazopata unazidi kushika kasi.
Wao wanajisifia kulamba teuzi huku sisi wakiendelea kutuhimiza kujiajiri!
Wengine hadi (rejea Naibu Waziri wa Afya Mollel, Nape et al.) wanakosa amani kabisa na kupata viriba tumbo kwa kufuatilia mikeka ya teuzi! Wengine wanatwambia hali si ngumu tutafute pesa!
Wanakula hadi wanavimbiwa! Na kwa sasa ni kama hakuna kitu wanaweza kufanya zaidi ya kuubiria teuzi!
Kifupi wanatuona kama manyani sisi tunaopambana kwa jasho, machozi na damu!