Watanzania wengi hawajui kuandika

Watanzania wengi hawajui kuandika

Tatizo sio wa Tanzania pekee bali ni mfumo wetu wa elimu upo upo tu juzi nasikia kuna vitabu feki vya kufundishia ni ajabu na aibu
 
Sio kwamba hawajui,bali wanachukulia poa tu.
Pia language budget ndo maana mtu anaandika vyovyote akijua wazi wataelewa hata akiandika herufi tofauti.
Ni kweli watu wamerelax, kuandka humu siyo mtihani, and its not official report... Kwahiyo kikubwa ujumbe kusudiwa ufike.. So far unafka kwa % kubwa sana....
 
Kwa muda mrefu nimekuwa nikifuatilia mijadala mbalimbali kwenye mitandao na maeneo mengi na nimegundua watanzania wengi hawana mbinu za uandishi eidha kwa makusudi au kwakutokujua mfano:

Fedha=feza
Thamani=Samani
Mpira=Mpila
Teremka=Telemka
Basi=Bax

Pia wengi wamekuwa wakiandika jumbe ambazo mwishowe hazileti maana au mantiki na hivyo kumfanya msomaji kupuuzia ujumbe husika. Kunatakiwa jitihada kubwa sana kuwasaidia vijana kuweza kuandika kwa ufasaha.

Asanteni tujirekebishe
Tuliofundishwa na walimu wa UPE hatuna matatizo haya. Haya makapi ya shule za kata ndio yanafundisha uandishi huo.
 
Tuliofundishwa na walimu wa UPE hatuna matatizo haya. Haya makapi ya shule za kata ndio yanafundisha uandishi huo.
Hapana. Siku zote lugha ya kitaaluma huwa haibadiliki. Wazungu pamoja na kuwa na maneno km gonna, wanna n.k lkn hawayatumii hata ss pia. Ni maneno ya mtaani yanayotumiwa hasa na vijana ktk mawasiliano yao. Wenyewe wanayaita swaga. Thatha joho tunaendaga wapi vile kula bata? Kama hivyo.
 
ni tatizo kubwa tz, hasa vijana mbwembwe nyingi kwenye uandishi mfano bx,thawa nk, mwisho wa siku inajenga mazingira mabovu na kushindwa kufikisha ujumbe ulio sahihi na wakueleweka.
 
Tofautisha kushindwa kujaza taarifa na kutojua kuandika.
Kwahiyo mtu kukuomba umsaidie kujaza taarifa haimanishi hajui kusoma na kuandika. Ni lugha tu hasa hiii ya kigeni inaleta mkanganyiko.
kushindwa kujaza taarifa nako semea mimi ni kule kunakotokana na kutojua kusoma na kuandika
 
Watanzania wengi ni kweli hawajui kuandika na kusoma, thats true.
Ilikuwa ni aibu sana kwenye kuandikisha vitambulisho vya uraia maeneo ya vijijini.
Hapa wilayani kwangu (mkoa wa Iringa) ambapo makao makuu ya wilaya yapo kilometa 4 nilishangaa mpaka nkaishiwa mshangao kuona mamia ya watu hawajui kuandika.
Kumbe inaonekana watu walishindwa kujiandikisha kwa ajili ya kupiga kura kwa sababu hiyo.
Sasa kwenye uraia hawakuwa na vitambulisho hivyo, wakalazimika kuandika barua ambayo inasainiwa na mwenyekiti wa kijiji. Mwanzoni mwenyekiti akawa anawaandikia ila wakawa wengi sana hivyo mwenyekiti alichoka, akaandika barua moja akaibandika ili kila mtu akopi, cha ajabu watu walishindwa kukopi, wakabaki wanasubiri msaada wa kuandikiwa.
Wote kuanzia bodaboda mpaka wazee.
.
Hii hadithi yako inachekesha kidogo lakini zaidi inasikitisha sana. Nyerere aliwahi kusema, "literacy Tanzania, ilifika wakati tulikuwa zaidi ya 90%, lakini itafika wakati watu hawajui kusoma wala kuandika lakini watu hawatajali kabisa". Naona ndipo tunakoelekea sasa.
 
Kuna watu mpaka majina ya asili ya kidini wameshindwa kuyatamka na kuwaita majina yaliyochakachuliwa mfano

1. ORALIA wao wanaamini kuwa ni OLALIA
 
Back
Top Bottom