Watanzania tusichague marobot

Watanzania tusichague marobot

muembeni

Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
31
Reaction score
5
Inasikitisha sana kuona kuwa rasimu ya katiba iliyokuwa ikiungwa mkono na zaidi ya asilimia 60 ya watanzania iliyeyuka hivi hivi kupitia kwa wale tunaowaita wawakilishi wa wananchi tuliowachagua wenyewe (wengi wao).

Hao wawakilishi wetu walikuwa mwanzoni ni watetezi wa katiba ya walio wengi lakini mara walipofika ulingoni na kutiwa ufunguo wa kichama walitusahau wananchi tuliowaajiri na kuamua kutumikia matakwa ya chama chao hivyo ndugu zangu watanzania tusiisahau dharau hii waliyotufanyia na hakuna sehemu nyengine ya kuwaadhibu waajiriwa wetu hawa ila katika masanduku ya kura.

Hivyo wale wote waliotugeuka Dodoma na kuifisha katiba ya watanzania tysiwachague huenda ikawa ni funzo kwa wengine ya kuwa Nchi kwanza na chama baadae.
 
watanzania tukiichagua tena ccm tusahau habari ya katiba mpya. ni samia suluhu hasani mgombea mwenza wa maghufuli aliyekuwa makamu mwenyekiti wa bunge la katiba lililochakachua maoni ya wananchi pale dodoma....watanzaniabtusikubali kamwe...
 
Back
Top Bottom