Watanzania Tushikamane Wakati Huu wa Majonzi ya Kupoteza Askari Wetu

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
May 5, 2014
629
1,561
Watanzania Tushikamane Wakati Huu wa Majonzi ya Kupoteza Askari Wetu
Chama cha ACT Wazalendo kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kushambuliwa na kuuawa kwa askari 8 wa jeshi la Polisi jana jioni katika eneo la Jaribu Mpakani, wilayani Kibiti, mkoa wa Pwani.

Chama cha ACT Wazalendo kinatoa pole kwa familia za mashujaa wetu hawa 8 waliouawa wakati wakilinda usalama wetu wananchi, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu pamoja na Jeshi zima la Polisi.

ACT Wazalendo tunaungana na wito wa kuwataka Watanzania kushikamana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kipindi hiki cha majonzi kwa Taifa pamoja na kutoa ushirikiano kwao kuhakikisha matendo ya namna hii yanakomeshwa.

Tunachukulia kitendo hiki Kama kitendo cha shambulio dhidi ya Jamhuri yetu na hatua kali na madhubuti zinapaswa kuchukuliwa.

Mlolongo wa matukio ya namna hii unaonyesha kuwa nchi yetu inapambana na kundi lisilo la kawaida na hivyo weledi wa hali ya juu unatakiwa katika kukabiliana na tishio hili dhidi ya Jamhuri yetu. Jeshi la polisi linatakiwa kufanya kazi zake Kwa uangalifu mkubwa na kuepuka kabisa na kuwaingiza raia wasio na hatia kwenye mateso yeyote kwani adui asipopatikana madhara yake ni makubwa zaidi. Matukio ya aina hii katika miezi ya hivi karibuni yawe funzo katika kukabiliana na uhalifu Kama huu. Tunatahadharisha kutotumia mwanya huu kuingiza wasiohusika kwani kufanya hivyo ni kuwapa ushindi wahalifu.

ACT Wazalendo tunaamini Jeshi letu la Polisi litahakikisha linawasaka, kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wote waliohusika na mauaji haya ya askari wetu.

Mohammed Said Babu
Katibu, Kamati ya Amani na Usalama - ACT Wazalendo
Aprili 14, 2017
Dar es salaam
 
Watanzania Tushikamane Wakati Huu wa Majonzi ya Kupoteza Askari Wetu
Chama cha ACT Wazalendo kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kushambuliwa na kuuawa kwa askari 8 wa jeshi la Polisi jana jioni katika eneo la Jaribu Mpakani, wilayani Kibiti, mkoa wa Pwani.

Chama cha ACT Wazalendo kinatoa pole kwa familia za mashujaa wetu hawa 8 waliouawa wakati wakilinda usalama wetu wananchi, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu pamoja na Jeshi zima la Polisi.

ACT Wazalendo tunaungana na wito wa kuwataka Watanzania kushikamana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kipindi hiki cha majonzi kwa Taifa pamoja na kutoa ushirikiano kwao kuhakikisha matendo ya namna hii yanakomeshwa.

Tunachukulia kitendo hiki Kama kitendo cha shambulio dhidi ya Jamhuri yetu na hatua kali na madhubuti zinapaswa kuchukuliwa.

Mlolongo wa matukio ya namna hii unaonyesha kuwa nchi yetu inapambana na kundi lisilo la kawaida na hivyo weledi wa hali ya juu unatakiwa katika kukabiliana na tishio hili dhidi ya Jamhuri yetu. Jeshi la polisi linatakiwa kufanya kazi zake Kwa uangalifu mkubwa na kuepuka kabisa na kuwaingiza raia wasio na hatia kwenye mateso yeyote kwani adui asipopatikana madhara yake ni makubwa zaidi. Matukio ya aina hii katika miezi ya hivi karibuni yawe funzo katika kukabiliana na uhalifu Kama huu. Tunatahadharisha kutotumia mwanya huu kuingiza wasiohusika kwani kufanya hivyo ni kuwapa ushindi wahalifu.

ACT Wazalendo tunaamini Jeshi letu la Polisi litahakikisha linawasaka, kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wote waliohusika na mauaji haya ya askari wetu.

Mohammed Said Babu
Katibu, Kamati ya Amani na Usalama - ACT Wazalendo
Aprili 14, 2017
Dar es salaam
Mohammed Said Babu, kuna tofauti gani kati ya Saanane na hawa askari? Mbona hukutoa wito kama huu kwa janga lililompata Ben? ACT Wazalendo, wazalendo hawawi discriminatory! Wote tunalia kwa hili lililotokea, lakini nyinyi kama taasisi, sauti ya wanyonge hampashwi kuonyesha ubaguzi wa hivi!
 
Kinachonishangaza ni hii hali ya Bata kaharisha lakini kuku kanya. Watu saba wameuawa hakuna kusema lolote askari kuuawa kila MTU mdomo juu. Subiri Mungu atahukumu sio kwa nafasi mlionao bali kwa maneno na matendo yenu. Time will tell. Mjue walikufa kama kuku ni ndugu za watu nao wana uchungu. Saanane ana ndugu nao wana machungu.
 
Shikamaneni wenyewe, mimi sishikamani nao mpaka siku wakiamua kuacha kua tawi la sisiem na kuanza kufanya kazi kiueledi.
 
Nyambafuuu......shikamana na ccm na policcm wenzako tuache sisi .......
Rais katangaza vita ya raia na vyombo vya dola
 
IMG_0378.JPG
Wewe ISIS siyo wewe kweli uliyehusika? Maana nasikia ni magaidi ndo yametekeleza hicho!
Mimi ni Goddess ISIS, google OSIRI, ISIS NA HORUS, usikurupuke na assuming! Duh!
 
Watanzania Tushikamane Wakati Huu wa Majonzi ya Kupoteza Askari Wetu
Chama cha ACT Wazalendo kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kushambuliwa na kuuawa kwa askari 8 wa jeshi la Polisi jana jioni katika eneo la Jaribu Mpakani, wilayani Kibiti, mkoa wa Pwani.

Chama cha ACT Wazalendo kinatoa pole kwa familia za mashujaa wetu hawa 8 waliouawa wakati wakilinda usalama wetu wananchi, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu pamoja na Jeshi zima la Polisi.

ACT Wazalendo tunaungana na wito wa kuwataka Watanzania kushikamana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kipindi hiki cha majonzi kwa Taifa pamoja na kutoa ushirikiano kwao kuhakikisha matendo ya namna hii yanakomeshwa.

Tunachukulia kitendo hiki Kama kitendo cha shambulio dhidi ya Jamhuri yetu na hatua kali na madhubuti zinapaswa kuchukuliwa.

Mlolongo wa matukio ya namna hii unaonyesha kuwa nchi yetu inapambana na kundi lisilo la kawaida na hivyo weledi wa hali ya juu unatakiwa katika kukabiliana na tishio hili dhidi ya Jamhuri yetu. Jeshi la polisi linatakiwa kufanya kazi zake Kwa uangalifu mkubwa na kuepuka kabisa na kuwaingiza raia wasio na hatia kwenye mateso yeyote kwani adui asipopatikana madhara yake ni makubwa zaidi. Matukio ya aina hii katika miezi ya hivi karibuni yawe funzo katika kukabiliana na uhalifu Kama huu. Tunatahadharisha kutotumia mwanya huu kuingiza wasiohusika kwani kufanya hivyo ni kuwapa ushindi wahalifu.

ACT Wazalendo tunaamini Jeshi letu la Polisi litahakikisha linawasaka, kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wote waliohusika na mauaji haya ya askari wetu.

Mohammed Said Babu
Katibu, Kamati ya Amani na Usalama - ACT Wazalendo
Aprili 14, 2017
Dar es salaam
Kama x mass watu husherekea kwa kuwapongeza watoto walazaliwa cku hiyo kwanini tusitumie nafasi hii kuwakumbuka pia wanaokufa kipindi hichi kama mashujaa walokufa na Kristo?
 
Mbona hatukusikia kauli ya watawala alipopotea BEN SAANANE.Mungu anawajibu kwamba binadamu wote ni sawa
 
Back
Top Bottom