ACT Wazalendo
JF-Expert Member
- May 5, 2014
- 629
- 1,561
Watanzania Tushikamane Wakati Huu wa Majonzi ya Kupoteza Askari Wetu
Chama cha ACT Wazalendo kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kushambuliwa na kuuawa kwa askari 8 wa jeshi la Polisi jana jioni katika eneo la Jaribu Mpakani, wilayani Kibiti, mkoa wa Pwani.
Chama cha ACT Wazalendo kinatoa pole kwa familia za mashujaa wetu hawa 8 waliouawa wakati wakilinda usalama wetu wananchi, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu pamoja na Jeshi zima la Polisi.
ACT Wazalendo tunaungana na wito wa kuwataka Watanzania kushikamana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kipindi hiki cha majonzi kwa Taifa pamoja na kutoa ushirikiano kwao kuhakikisha matendo ya namna hii yanakomeshwa.
Tunachukulia kitendo hiki Kama kitendo cha shambulio dhidi ya Jamhuri yetu na hatua kali na madhubuti zinapaswa kuchukuliwa.
Mlolongo wa matukio ya namna hii unaonyesha kuwa nchi yetu inapambana na kundi lisilo la kawaida na hivyo weledi wa hali ya juu unatakiwa katika kukabiliana na tishio hili dhidi ya Jamhuri yetu. Jeshi la polisi linatakiwa kufanya kazi zake Kwa uangalifu mkubwa na kuepuka kabisa na kuwaingiza raia wasio na hatia kwenye mateso yeyote kwani adui asipopatikana madhara yake ni makubwa zaidi. Matukio ya aina hii katika miezi ya hivi karibuni yawe funzo katika kukabiliana na uhalifu Kama huu. Tunatahadharisha kutotumia mwanya huu kuingiza wasiohusika kwani kufanya hivyo ni kuwapa ushindi wahalifu.
ACT Wazalendo tunaamini Jeshi letu la Polisi litahakikisha linawasaka, kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wote waliohusika na mauaji haya ya askari wetu.
Mohammed Said Babu
Katibu, Kamati ya Amani na Usalama - ACT Wazalendo
Aprili 14, 2017
Dar es salaam
Chama cha ACT Wazalendo kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kushambuliwa na kuuawa kwa askari 8 wa jeshi la Polisi jana jioni katika eneo la Jaribu Mpakani, wilayani Kibiti, mkoa wa Pwani.
Chama cha ACT Wazalendo kinatoa pole kwa familia za mashujaa wetu hawa 8 waliouawa wakati wakilinda usalama wetu wananchi, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu pamoja na Jeshi zima la Polisi.
ACT Wazalendo tunaungana na wito wa kuwataka Watanzania kushikamana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kipindi hiki cha majonzi kwa Taifa pamoja na kutoa ushirikiano kwao kuhakikisha matendo ya namna hii yanakomeshwa.
Tunachukulia kitendo hiki Kama kitendo cha shambulio dhidi ya Jamhuri yetu na hatua kali na madhubuti zinapaswa kuchukuliwa.
Mlolongo wa matukio ya namna hii unaonyesha kuwa nchi yetu inapambana na kundi lisilo la kawaida na hivyo weledi wa hali ya juu unatakiwa katika kukabiliana na tishio hili dhidi ya Jamhuri yetu. Jeshi la polisi linatakiwa kufanya kazi zake Kwa uangalifu mkubwa na kuepuka kabisa na kuwaingiza raia wasio na hatia kwenye mateso yeyote kwani adui asipopatikana madhara yake ni makubwa zaidi. Matukio ya aina hii katika miezi ya hivi karibuni yawe funzo katika kukabiliana na uhalifu Kama huu. Tunatahadharisha kutotumia mwanya huu kuingiza wasiohusika kwani kufanya hivyo ni kuwapa ushindi wahalifu.
ACT Wazalendo tunaamini Jeshi letu la Polisi litahakikisha linawasaka, kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wote waliohusika na mauaji haya ya askari wetu.
Mohammed Said Babu
Katibu, Kamati ya Amani na Usalama - ACT Wazalendo
Aprili 14, 2017
Dar es salaam