jaxonwaziri
JF-Expert Member
- Feb 17, 2010
- 375
- 195
Hivi majuzi tu huyu bwana alisema yaliyopo hapa chini, wengi sana tukaumizwa kwa ulevi huu na jeuri. Tukajiuliza anatoa wapi jeuri ya kejeli hii?
View attachment 12285
Je, watanzania, tutakumbuka ufinyu wa fikra zake na kuamua kumfunza adabu yeye, na wenzake wote wanaopewa dhamana na wananchi na baadaye wanaanza kuwadharau wananchi hao hao waliompa dhamana husika?
Tusifanye makosa, hatuhitaji viongozi wa namna hii, kwanza naombeni msamaha kwenu ninyi watu mlio makini humu jamvini kwa kumuita jamaa huyu "kiongozi". Neno kiongozi lina maana ya pekee na inayostahili kuheshimiwa. Ila huyu, ni picha tu, yupo pale kucheka cheka tu!
Kura zote kwa Dr Wilbroad Slaa pamoja na wabunge wa upinzani, chagua CCM pale tu, mbunge wa CCM ni mtu makini na ameonyesha utendaji uliotukuka katika historia ya uongozi wake!
Tumeona madudu wanayoyafanya katika chaguzi. Wanatabia ya zengwe na wizi uliokithiri. Pia rushwa na kila aina ya uozo! Tumeshuhudia kwa wazi kabisa utumikaji wa mbinu chafu ili kupata nafasi za uongozi, tujiulize tukiendelea kukabidhi taifa kwa watu kama hawa, tutekuwa tunaipeleka wapi Tanzania? Jibu ni rahisi, HATUWATAKI na katika karatasi za kura mwaka huu tutawaeleza wazi kuwa "WAMEOZA" na "TUMEWACHOKA"
View attachment 12285
Je, watanzania, tutakumbuka ufinyu wa fikra zake na kuamua kumfunza adabu yeye, na wenzake wote wanaopewa dhamana na wananchi na baadaye wanaanza kuwadharau wananchi hao hao waliompa dhamana husika?
Tusifanye makosa, hatuhitaji viongozi wa namna hii, kwanza naombeni msamaha kwenu ninyi watu mlio makini humu jamvini kwa kumuita jamaa huyu "kiongozi". Neno kiongozi lina maana ya pekee na inayostahili kuheshimiwa. Ila huyu, ni picha tu, yupo pale kucheka cheka tu!
Kura zote kwa Dr Wilbroad Slaa pamoja na wabunge wa upinzani, chagua CCM pale tu, mbunge wa CCM ni mtu makini na ameonyesha utendaji uliotukuka katika historia ya uongozi wake!
Tumeona madudu wanayoyafanya katika chaguzi. Wanatabia ya zengwe na wizi uliokithiri. Pia rushwa na kila aina ya uozo! Tumeshuhudia kwa wazi kabisa utumikaji wa mbinu chafu ili kupata nafasi za uongozi, tujiulize tukiendelea kukabidhi taifa kwa watu kama hawa, tutekuwa tunaipeleka wapi Tanzania? Jibu ni rahisi, HATUWATAKI na katika karatasi za kura mwaka huu tutawaeleza wazi kuwa "WAMEOZA" na "TUMEWACHOKA"