pharaoh_2
Senior Member
- Jun 25, 2015
- 143
- 123
Nimeikuta mahali:-
WARAKA WA VIJANA OP.KIKWETE KWA VIONGOZI NA WAKUU WA SERIKALI.
Ndg. Sisi ni vijana wa op.kikwete kama tulivyo tanabaisha hapo juu!! Tumefanya kazi ya jkt na kulitumikia jeshi la kujenga Taifa takribani miaka 3. Tumeshiriki katika operation mbali mbali ndani ya nchi yetu kama ifuatavyo: operation shamba- hii ilikuwa ni program ya kuzalisha chakula ndani ya jeshi la kujenga Taifa , operation Mifungo - hii ilikuwa ni kuhakikisha mifugo yetu ya jeshi la kujenga Taifa inashiba na kwenye op hii kulikuwa na changamito zake mara kadhaa tumekoswa koswa na tembo,simba nk, tumeshiriki operation Bangi - hii ilikuwa ni kupambana na walima bangi ndani ya nchi yetu wanaoharibu vijana na nguvu kazi ya Taifa kwa ujumla, tumeshiriki operation kibiti!! Hii kila kiongozi tunadhani anaelewa vyema, tumeshiki operation madawati na ujenzi wa nyumba za walimu pamoja na mashule pia tumekuwa tukishiki ulinzi wa nchi yetu kupitia vikosini na sehemu mbali mbali pale ilipobidi, lakini mbali na kushiriki operation zote hizo na kulitumia Taifa ili kwa moyo mmoja tumeambulia kurudishwa nyumbani na nafasi zetu kuchukuliwa na vijana ambao hata mwaka walikuwa hawana ndani ya jeshi la kujenga taifa yani (JKT). Hata usaili wa jwtz walikuwa hawajafanya kwaiyo hatujui walichukuliwa kwa vigezo vipi na sisi tuliachwa kwa vigezo vipi!!! Ni masikikitiko makubwa sana wale wanao ongea kwenye vyombo vya habari na kuhubili uzalendo ndo wanakuwa mstali wa mbele kuwavunja moyo na uzalendo vijana wa Kitanzania. Uzalendo utatoka wapi kwa namna hii?? Kama wananchi wanaamini ndani ya jeshi ndo kunatendeka haki lakini sasa inakuwa kinyume chake !! Taifa ili tunalipeleka wapi?? Tunafahamu Jkt hawaajiri pia tunatambua na kuheshimu sana Mkataba tulioingia na Jkt lakini ajira zilizotolewa ndani ya Jwtz kupitia Mh. Rais akiwa Arusha hazikufuata utaratibu yani seniority!! Waliopata nafasi hizo ni watoto wa wakubwa jeshini wala si watoto wa maskini kama serikali yetu tukufu inavyo taka!!! Tunachelea kusema hata jina la jeshi basi libadilishwe yani liwe "jeshi la Wanajeshi" badala ya "Jeshi la wanachi". Maana wanufaika wakubwa wa ajira hizo ni familia za kijeshi!! Rai yetu!! Kwa viongozi na serikali Nchi hii ni yetu wote! Hakuna sababu ya sisi kutengwa. Hata jeshi la polisi wametoa nafasi lakini sisi tumeendelea kutengwa!!! Dhambi yetu ni nini hasa? Je hatuna vigezo? Au sisi ni kina nani ndani ya Taifa ili mpaka tutengwe hivi? Chonde chonde tunaomba ajira na sisi ndani ya vyombo vya ulinzi na usalama vya Taifa letu ili Pendwa Tanzania. Sisi si wanaharakati na hatufikirii kuwa wana harakati Bali ni vijana wazalendo kabisa wenye vilio na manunguniko ndani ya nafsi zetu na tunaomba kilio hichi kisikike kwa viongozi wetu hasa wazalendo na waangalie namna njema ya kutusaidia. Aksanteni.
WARAKA WA VIJANA OP.KIKWETE KWA VIONGOZI NA WAKUU WA SERIKALI.
Ndg. Sisi ni vijana wa op.kikwete kama tulivyo tanabaisha hapo juu!! Tumefanya kazi ya jkt na kulitumikia jeshi la kujenga Taifa takribani miaka 3. Tumeshiriki katika operation mbali mbali ndani ya nchi yetu kama ifuatavyo: operation shamba- hii ilikuwa ni program ya kuzalisha chakula ndani ya jeshi la kujenga Taifa , operation Mifungo - hii ilikuwa ni kuhakikisha mifugo yetu ya jeshi la kujenga Taifa inashiba na kwenye op hii kulikuwa na changamito zake mara kadhaa tumekoswa koswa na tembo,simba nk, tumeshiriki operation Bangi - hii ilikuwa ni kupambana na walima bangi ndani ya nchi yetu wanaoharibu vijana na nguvu kazi ya Taifa kwa ujumla, tumeshiriki operation kibiti!! Hii kila kiongozi tunadhani anaelewa vyema, tumeshiki operation madawati na ujenzi wa nyumba za walimu pamoja na mashule pia tumekuwa tukishiki ulinzi wa nchi yetu kupitia vikosini na sehemu mbali mbali pale ilipobidi, lakini mbali na kushiriki operation zote hizo na kulitumia Taifa ili kwa moyo mmoja tumeambulia kurudishwa nyumbani na nafasi zetu kuchukuliwa na vijana ambao hata mwaka walikuwa hawana ndani ya jeshi la kujenga taifa yani (JKT). Hata usaili wa jwtz walikuwa hawajafanya kwaiyo hatujui walichukuliwa kwa vigezo vipi na sisi tuliachwa kwa vigezo vipi!!! Ni masikikitiko makubwa sana wale wanao ongea kwenye vyombo vya habari na kuhubili uzalendo ndo wanakuwa mstali wa mbele kuwavunja moyo na uzalendo vijana wa Kitanzania. Uzalendo utatoka wapi kwa namna hii?? Kama wananchi wanaamini ndani ya jeshi ndo kunatendeka haki lakini sasa inakuwa kinyume chake !! Taifa ili tunalipeleka wapi?? Tunafahamu Jkt hawaajiri pia tunatambua na kuheshimu sana Mkataba tulioingia na Jkt lakini ajira zilizotolewa ndani ya Jwtz kupitia Mh. Rais akiwa Arusha hazikufuata utaratibu yani seniority!! Waliopata nafasi hizo ni watoto wa wakubwa jeshini wala si watoto wa maskini kama serikali yetu tukufu inavyo taka!!! Tunachelea kusema hata jina la jeshi basi libadilishwe yani liwe "jeshi la Wanajeshi" badala ya "Jeshi la wanachi". Maana wanufaika wakubwa wa ajira hizo ni familia za kijeshi!! Rai yetu!! Kwa viongozi na serikali Nchi hii ni yetu wote! Hakuna sababu ya sisi kutengwa. Hata jeshi la polisi wametoa nafasi lakini sisi tumeendelea kutengwa!!! Dhambi yetu ni nini hasa? Je hatuna vigezo? Au sisi ni kina nani ndani ya Taifa ili mpaka tutengwe hivi? Chonde chonde tunaomba ajira na sisi ndani ya vyombo vya ulinzi na usalama vya Taifa letu ili Pendwa Tanzania. Sisi si wanaharakati na hatufikirii kuwa wana harakati Bali ni vijana wazalendo kabisa wenye vilio na manunguniko ndani ya nafsi zetu na tunaomba kilio hichi kisikike kwa viongozi wetu hasa wazalendo na waangalie namna njema ya kutusaidia. Aksanteni.