Nipo hapa Airport Dar es salaam, barabarani nimeona mamia ya magari ya abiria na binafsi, aisee wamesimama tu muda mrefu wamesubilishwa kwaajiri ya misafara ya viongozi wakuu wa nchi.
Takribani takika 45 mbele ndio naona kuna ndege zinatua hapa....Inawezekana kabla hata kiongozi hajaanza safari huko atokako, huku barabarani raia huwa wanapigwa stop ya maana.
Sasa bado watanzania wapo kwenye foreni wanasubili mkuu apumzike kidogo uwanjani hapo, Kisha asalimiane na watu, alafu ndio taratiibu aanze safari kwenda town, na Kisha huku nyuma fungulia wuu wuu ifanyike.. Kuna thamani ya muda kweli?