Ngambo Ngali
JF-Expert Member
- Apr 17, 2009
- 3,517
- 1,359
CHADEMA wameteua, Dakta slaa ulingoni,
CCM kuwatungua, kuwatoa mjengoni,
Uteuzi ulotulia, kama maji mtungini
Watani wamepagawa, sasa wanatapatapa
Slaa chaguo poa, tutakavyo kutimia,
Hakuna wa kutania, wala pua kuitia,
Kazi kwetu kuamua, Oktoba yakaribia,
Kura zote kwa SLAA, ili tupate raha.
Kura zote kwa Slaa, ili tupate raha,
Nchi kaipigania, bila kuwa na staha,
Na mengi katuambia, hakujali majeraha
SLAA chaguo la leo, kwa faida ya milele.
Kumbukeni wajameni, ni yeye alisimama,
Macho yenu fungueni, mwembe yanga kalalama
Yanachotwa mabenkini, mambo huko si salama,
Bila yeye kukemea, mapesa karibu kwisha
Akaenda migodini, akazipiga kelele
Tuachieni madini, msiyapigie misele
Mgawo uwe makini , hatutapiga kelele
Serikali ikabaini,asemacho ni bayana.
Kama tukipiga kura , SLAA kumkubali,
Tutapata barabara, shule na maji kweli
Yeye atatupa kula, kusaza ugali na wali,
Tumchague Slaa, kama twahitaji raha.
CCM kuwatungua, kuwatoa mjengoni,
Uteuzi ulotulia, kama maji mtungini
Watani wamepagawa, sasa wanatapatapa
Slaa chaguo poa, tutakavyo kutimia,
Hakuna wa kutania, wala pua kuitia,
Kazi kwetu kuamua, Oktoba yakaribia,
Kura zote kwa SLAA, ili tupate raha.
Kura zote kwa Slaa, ili tupate raha,
Nchi kaipigania, bila kuwa na staha,
Na mengi katuambia, hakujali majeraha
SLAA chaguo la leo, kwa faida ya milele.
Kumbukeni wajameni, ni yeye alisimama,
Macho yenu fungueni, mwembe yanga kalalama
Yanachotwa mabenkini, mambo huko si salama,
Bila yeye kukemea, mapesa karibu kwisha
Akaenda migodini, akazipiga kelele
Tuachieni madini, msiyapigie misele
Mgawo uwe makini , hatutapiga kelele
Serikali ikabaini,asemacho ni bayana.
Kama tukipiga kura , SLAA kumkubali,
Tutapata barabara, shule na maji kweli
Yeye atatupa kula, kusaza ugali na wali,
Tumchague Slaa, kama twahitaji raha.