Wassira uko wapi ututabirie tena?

Wassira uko wapi ututabirie tena?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Komredi Stephen Wasira nakutafuta. Hata Lumumba sikuoni siku hizi. Nakutafuta nikuombe utoe utabiri mwingine. Ule naona umekwenda kinyume. Umewaimarisha badala ya kuwasambaratisha. Najua nawe una karama za kiutabiri. Komredi Wasira, fanya mambo. Redio zitatangaza na magazeti kuandika kwa wingi. Safari hii utabiri wako utatimia. Please, show yourself for CCM!

Komredi Wasira, ni wewe uliyetabiri kuwa CHADEMA itasambaratika na kufa miaka ya nyuma. Makada walipa-ada tukakushangilia kwa kutusaidia. Kwa kuwaombea mabaya (kiutabiri) wapinzani wetu. Tukakuona kama mkombozi wa chama na hata kupewa airtime ya kutosha kwenye Mchakato wa Katiba mpya na hata kwenye kuandaa Ilani ya CCM ya mwaka huu kama Mwenyekiti wa Ilani. Tukakuona kuwa wewe ni kiboko ya wapinzani hasa CHADEMA.

Uko wapi Komredi? Nakutafuta kweli kweli. Najua umeshashinda kumkwamisha Bulaya asigombee Jimbo nawe kule Bunda. Bulaya angepitishwa kugombea, pasingetosha. Lakini,weledi wako kisiasa umemkwamisha Bulaya kisasa bila anasa wala mikasa. Ikaonekana amekataliwa na wanaCHADEMA wenyewe. Hiyo imekaa safi. Bulaya kwisha kazi yake. Labda abaki kama Mbunge wa Vitu...hapana ni viti maalum. U wapi Komredi?

CHADEMA wamemea na kuenea. Wameungana na wenzao na kuunda UKAWA na sasa wana power. Tafadhali jitokeze Komredi utabiri tena kuhusu CHADEMA na hata UKAWA. Harakisha kwakuwa sasa hali inatisha na inatuambia pisha. Uko wapi Komredi Wasira utabiri tena?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Mzee wangu Tupatupa,zamani tulikuwa tunasema ...'ADUI yako mwombee Njaa"...nadhani ili adhoofu afutikiea mbali...

Lakini sisi wa leo tunasema hivi..."Adui yako Muombee maisha marefu" ili aone utakavyobarikiwa................

CDM tunawaombea CCM maisha marufu ili muone Mungu atakavyotubariki.................😛ray2:
 
Mzee Tutapatupa nakushukuru kwa updates zako. Lakini Jitokeze na kwenye Mtandao wa majirani zetu wa MF. Ebu twambie malengo ya vikao vya wazito wa chama chetu kokote wanakokutana wanalenga nini? Sasa itakuwaje kama kibao kikibadilika? Wambie vijana kwa wazee msimamo wa chama chetu. Kwa nini waliochukua fomu za Uraisi sasa tunasikia wamerudi tena majimboni wakati walisha tuaga? Wengine tuliwaaga hata wafanyakazi kwenye wizara zetu lakini potelea mbali ngoja wachukue fomu za Ubunge tu.
 
Mzee Tutapatupa nakushukuru kwa updates zako. Lakini Jitokeze na kwenye Mtandao wa majirani zetu wa MF. Ebu twambie malengo ya vikao vya wazito wa chama chetu kokote wanakokutana wanalenga nini? Sasa itakuwaje kama kibao kikibadilika? Wambie vijana kwa wazee msimamo wa chama chetu. Kwa nini waliochukua fomu za Uraisi sasa tunasikia wamerudi tena majimboni wakati walisha tuaga? Wengine tuliwaaga hata wafanyakazi kwenye wizara zetu lakini potelea mbali ngoja wachukue fomu za Ubunge tu.

Nitafanya hivyo

Mzee Tupatupa
 
Asante sana mzee Tupa tupa....unajua hata wenzio lumumba huwa hawakuelewi. Wanakaaaga kimyaaa sababu ya kuwa mkweli. Heshima yako sana kiongozi. Mweeeeeee
 
Komredi Stephen Wasira nakutafuta. Hata Lumumba sikuoni siku hizi. Nakutafuta nikuombe utoe utabiri mwingine. Ule naona umekwenda kinyume. Umewaimarisha badala ya kuwasambaratisha. Najua nawe una karama za kiutabiri. Komredi Wasira, fanya mambo. Redio zitatangaza na magazeti kuandika kwa wingi. Safari hii utabiri wako utatimia. Please, show yourself for CCM!

Komredi Wasira, ni wewe uliyetabiri kuwa CHADEMA itasambaratika na kufa miaka ya nyuma. Makada walipa-ada tukakushangilia kwa kutusaidia. Kwa kuwaombea mabaya (kiutabiri) wapinzani wetu. Tukakuona kama mkombozi wa chama na hata kupewa airtime ya kutosha kwenye Mchakato wa Katiba mpya na hata kwenye kuandaa Ilani ya CCM ya mwaka huu kama Mwenyekiti wa Ilani. Tukakuona kuwa wewe ni kiboko ya wapinzani hasa CHADEMA.

Uko wapi Komredi? Nakutafuta kweli kweli. Najua umeshashinda kumkwamisha Bulaya asigombee Jimbo nawe kule Bunda. Bulaya angepitishwa kugombea, pasingetosha. Lakini,weledi wako kisiasa umemkwamisha Bulaya kisasa bila anasa wala mikasa. Ikaonekana amekataliwa na wanaCHADEMA wenyewe. Hiyo imekaa safi. Bulaya kwisha kazi yake. Labda abaki kama Mbunge wa Vitu...hapana ni viti maalum. U wapi Komredi?

CHADEMA wamemea na kuenea. Wameungana na wenzao na kuunda UKAWA na sasa wana power. Tafadhali jitokeze Komredi utabiri tena kuhusu CHADEMA na hata UKAWA. Harakisha kwakuwa sasa hali inatisha na inatuambia pisha. Uko wapi Komredi Wasira utabiri tena?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Nikwambie kitu ccm sasa ndo inaimalika na cdm ndo kwisha habari yake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom