Wassira: Nisingekuwa 'msafi' UKAWA wangenimaliza

Wassira: Nisingekuwa 'msafi' UKAWA wangenimaliza

Kagose

Member
Joined
Jan 26, 2014
Posts
32
Reaction score
4
Katika mahojiano na Gazeti la Dira ya Mtanzania,Mbunge wa Bunda na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na uratibu) Stephen Masatu Wasira amesema kuwa ccm inao viongozi wasafi na yenyewe ni safi ndio maana imelilea Taifa katika misingi ya upendano,mshikamano,amani,utulivu na kwamba ccm inazidi kuboresha huduma na ustawi wa watu katika Taifa hili.

Wasira anasema yeye mwenyewe anajiamini kwa dhati kuwa ni msafi na mwadilifu mbele ya Taifa lake na chama chake."Kama kuna mtu anauona uchafu wangu awaeleze watanzania;asiogope wala asijifiche kusemea pembeni"

Katika mahojiano hayo,Wasira anakiri kuwa kama asingekuwa msafi Ukawa wangemmaliza maana wanamuona kuwa ni mtu anayewakera sana.Wasira anasema hao watu(Ukawa) wamejitahidi sana kumchunguza na dosari zake ili wammalize na kumnyamazisha kabisa,lakini wameshindwa kuzipata maana hazipo.

Hivi wana jf, ni kweli kuwa kiumbe huyu ni msafi kiasi hicho?
 
laiti kama MWL NYERERE angekuwepo huyu wasira asingerudi ccm , hana usafi wowote ! Aling'olewa kwenye ubunge wa bunda mahakamani kwa sababu ya RUSHWA , hajawahi kusafishwa .
 
Katika mahojiano na Gazeti la Dira ya Mtanzania,Mbunge wa Bunda na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na uratibu) Stephen Masatu Wasira amesema kuwa ccm inao viongozi wasafi na yenyewe ni safi ndio maana imelilea Taifa katika misingi ya upendano,mshikamano,amani,utulivu na kwamba ccm inazidi kuboresha huduma na ustawi wa watu katika Taifa hili.

Wasira anasema yeye mwenyewe anajiamini kwa dhati kuwa ni msafi na mwadilifu mbele ya Taifa lake na chama chake."Kama kuna mtu anauona uchafu wangu awaeleze watanzania;asiogope wala asijifiche kusemea pembeni"

Katika mahojiano hayo,Wasira anakiri kuwa kama asingekuwa msafi Ukawa wangemmaliza maana wanamuona kuwa ni mtu anayewakera sana.Wasira anasema hao watu(Ukawa) wamejitahidi sana kumchunguza na dosari zake ili wammalize na kumnyamazisha kabisa,lakini wameshindwa kuzipata maana hazipo.

Hivi wana jf, ni kweli kuwa kiumbe huyu ni msafi kiasi hicho?

Kha! Wammalize kivipi wakati maneno yake (Kauli zake) ni msaada mkubwa kwa ukawa katika mapambano dhidi ya CCM!!!!
 
UKAWA hawajui ku~capitalise kwenye vitu kama hivi,wakati wale 201 wanaalikwa usiku kwa mawaziri ili wawapoze,ukawa wangejenga hoja na kutoa mfano kwamba mmoja wa mawaziri wa jk alipatikana na hatia ya rushwa na hivyo si ajabu anaendeleza mchezo wake hapa bungeni kwa kuwarubuni 201 ,dovutwa,cheyo,mrema,arfi na wengine.Hii ikirudiwa miezi miwili mfululizo wasira hakuna mahali atapewa jukwaa
 
Huyu si alishawahi kuenguliwa ubunge kwa tuhuma za rushwa.Wanasiasa bwana wakipata sehemu ya kula wanasahau dhambi zao zote za nyuma.

Tanzania inaweza kuwa nchi ya kwanza kuruhusu watu waliothibitishwa kuwa wala rushwa kukaa kama mawaziri wa utawala bora,wizara ambayo inarayibu mambo ya TAKUKURU na iko ofisi ya rais,rais hakutakiwa kukaa nae karibu
 
Usafi gani unao ? uchafu mtupu wadhani hatujui ulivyoibia wakulima na viwanda vya pamba kule bunda vile vya villian.Sura na akili kama nyani.
 
Kha! Wammalize kivipi wakati maneno yake (Kauli zake) ni msaada mkubwa kwa ukawa katika mapambano dhidi ya CCM!!!!

Ni kweli nawakumbusha kidogo alipo sema chadema haitamaliza mwaka lazima ife yaani ile kauli ilichukuliwa kwa uzito unaostahili ndio ulikuwa mwanzo wa wasaliti wote kujulikana zzk na timu yake wale ma mm 1-3 na vibaraka wengine kama akina kansa mbaruku na mipango mingi mingine ya kutungua chopa kesi za ugidi na mambo mengi yanayofanana na hayo ki ukweli chadema ni mpango wa mungu mara nyingi wale wote wanaopingana na mpango wa mungu huwa mwisho wao ni mbaya
 
Nimeshapanda naye ndege mara 2 hivi,Dubai anafuata nn?kama sio biashara alizopata mtaji kifisadi.
 
Ukigeugeu ni dhambi kubwa! Mara upinzani Mara Chama twawala,njaa mbaya sana!! Eti Wasira nae Msafi! Majanga matupu wakuu! Msalani upoo.
 
Back
Top Bottom