Wasio na bajeti wanahitaji mabadiliko?

Wasio na bajeti wanahitaji mabadiliko?

John Masonga

Member
Joined
Oct 6, 2015
Posts
14
Reaction score
1
Mimi nataka kuhusu hii sera ya mabadiliko ya serikali, je hawa ndugu zangu ambao matumizi yao hayana control yani hawana kupangilia bajeti kwenye matumizi yao je na hao pia wanahitai mabadiliko? hivi unakuta mtu ana laki moja mchana halafu hadi saa tatu usiku hana hela anaamka asubuhi hela ya chai hana kwa matumizi mabaya kama hayo je kuna sababu ya mtu huyo kudai mabadiliko wakati yeye mfujaji wa hela ovyo? tujadili wadau
 
Ukiwauloza ni nini wamebadilisha makwao na wanakotoka utashangaa majibu yao ..wanajua kudai kwa nguvu zote lakini hata wao kwao kudeliver ni msamiati wa kikorea
 
Tatizo wamekariri, kwao wao maana ya mabadiliko ni kuitoa CCM madarakani. Siyo kosa lao ila ndivyo walivyokaririshwa na wagombea wa vyama vyao.

Ushauri wangu tu ni kwamba waanze kujifunza nini maana ya mabadiliko ya kweli, kisha wajifunze ni kiongozi gani anaweza kuleta mabadiliko ya kweli. kisha wazisome tena ilani za wagombea wote na wawasikilize wagombea wanapohutubia bila ushabiki wowote na wafanye maamuzi kwa kuingalia Tanzania ya miaka 10 ijayo...

Kama utafanya hivo utagundua wazi kuwa Rais anayetufaa kututoa hapa tulipo na kutupeleka mbele ni John Pombe Magufuli... Mimi, wewe na yule tumpe kura zetu
 
Back
Top Bottom