Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
WARATIBU wa uchaguzi , wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo wamekutana jijini Arusha kwa siku tatu kwa ajili ya mafunzo ikiwa ni maandalizi ya kuwawezesha kutekeleza ipasavyo kazi na jukumu lililo mbele yao.
Akifungua mafunzo hayo leo Mjumbe wa Tume huru ya Taifa ya uchaguzi ,Dkt.Zakia Abubakar amesema kuwa ,wameteuliwa kwa mujibu wa Sheria na tangu tarehe ya uteuzi wao wana wajibu wa kikatiba na kisheria kusimamia na kuratibu uendeshaji wa uchaguzi wa Rais ,wabunge ,madiwani kwa Tanzania bara kwa niaba ya Tume katika maeneo yao ya uteuzi.
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Amesema kuwa, dhamana waliyopewa ya kusimamia na kuratibu uendeshaji wa uchaguzi ni nyeti na muhimu kwa mustakabali wa Taifa letu hivyo wanategemewa kwa kuzitambua utendaji wao.
Aidha amewataka kuwajibika ipasavyo katika kipindi chose cha utumishi wao wa Tume hadi hapo watakapokamilisha jukumu hilo la uchaguzi mkuu.
Akifungua mafunzo hayo leo Mjumbe wa Tume huru ya Taifa ya uchaguzi ,Dkt.Zakia Abubakar amesema kuwa ,wameteuliwa kwa mujibu wa Sheria na tangu tarehe ya uteuzi wao wana wajibu wa kikatiba na kisheria kusimamia na kuratibu uendeshaji wa uchaguzi wa Rais ,wabunge ,madiwani kwa Tanzania bara kwa niaba ya Tume katika maeneo yao ya uteuzi.
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Amesema kuwa, dhamana waliyopewa ya kusimamia na kuratibu uendeshaji wa uchaguzi ni nyeti na muhimu kwa mustakabali wa Taifa letu hivyo wanategemewa kwa kuzitambua utendaji wao.
Aidha amewataka kuwajibika ipasavyo katika kipindi chose cha utumishi wao wa Tume hadi hapo watakapokamilisha jukumu hilo la uchaguzi mkuu.