keynessian
JF-Expert Member
- Feb 28, 2014
- 591
- 422
Habari za wasaa huu mchumi mwenzangu Lipumba,
Tunaheshimu uamuzi wako wa kujiuzulu uliouchukua hivi karibuni, ni simanzi kubwa kwa wanaharakati wa mabadiliko nchini.
Kitendo hichi mpaka sasa kimezua maswali maswali mengi kuliko majibu,kimefanya juhudi zako zote za kupigania mabadiliko kuwa sawa sawa na hamna kitu, lakini pia umejivunjia heshima yako kubwa ulijiwekea kwa muda mrefu wananchi walitarajia mtu mwenye busara kama wewe ambayo umejitokeza mara nyingi kuwania nafasi ya urais kwamba utakuwa ni mtu mwenye busara na hekima kubwa mwenye uwezo wa kufanya maamuzi kwa kutambua athari ya maamuzi yako kwa sasa na baadaye.
Ni aibu sana kwa mwanazuoni mkubwa kama wewe kutoa excuse kwa kusema dhamira yangu inanisuta. Vipi kama ungekuwa kiongozi mkuu wa nchi ni maamuzi mangapi ya hovyo ungeyefanya na kusema dhamira yako imekusuta?
Hii wanazuoni wanaiita intellectual negligence, umeeonesha udhaifu mkubwa sana kwenye maamuzi,umedhalilisha taaluma na ninasema bila kumungunya hauna sifa ya kuwa kiongozi.
Aidha nipende kutoa shukrani kwa dhati kwa watanzania waliokukataa kwenye sanduku la kura miaka yote uliyogombea, lakini lingine ambalo ni likubwa nawashukuru sana viongozi wa CUF wakiongozwa na Maalim Seif pamoja na wanachama wote wa CUF kwa kukupuuza wewe pamoja na kitendo chako cha kujiuzulu.
Ushauri wangu kwako: Kuendelea kujitokeza kwenye vyombo vya habari na kuponda UKAWA ni kuendelea kujivunjia kale kaheshima kadogo kalichobakia,ingekuwa busara zaidi kama ungekaa pembeni na kuwa mtazamaji.
Ni hayo tu.
Keynessian!
Tunaheshimu uamuzi wako wa kujiuzulu uliouchukua hivi karibuni, ni simanzi kubwa kwa wanaharakati wa mabadiliko nchini.
Kitendo hichi mpaka sasa kimezua maswali maswali mengi kuliko majibu,kimefanya juhudi zako zote za kupigania mabadiliko kuwa sawa sawa na hamna kitu, lakini pia umejivunjia heshima yako kubwa ulijiwekea kwa muda mrefu wananchi walitarajia mtu mwenye busara kama wewe ambayo umejitokeza mara nyingi kuwania nafasi ya urais kwamba utakuwa ni mtu mwenye busara na hekima kubwa mwenye uwezo wa kufanya maamuzi kwa kutambua athari ya maamuzi yako kwa sasa na baadaye.
Ni aibu sana kwa mwanazuoni mkubwa kama wewe kutoa excuse kwa kusema dhamira yangu inanisuta. Vipi kama ungekuwa kiongozi mkuu wa nchi ni maamuzi mangapi ya hovyo ungeyefanya na kusema dhamira yako imekusuta?
Hii wanazuoni wanaiita intellectual negligence, umeeonesha udhaifu mkubwa sana kwenye maamuzi,umedhalilisha taaluma na ninasema bila kumungunya hauna sifa ya kuwa kiongozi.
Aidha nipende kutoa shukrani kwa dhati kwa watanzania waliokukataa kwenye sanduku la kura miaka yote uliyogombea, lakini lingine ambalo ni likubwa nawashukuru sana viongozi wa CUF wakiongozwa na Maalim Seif pamoja na wanachama wote wa CUF kwa kukupuuza wewe pamoja na kitendo chako cha kujiuzulu.
Ushauri wangu kwako: Kuendelea kujitokeza kwenye vyombo vya habari na kuponda UKAWA ni kuendelea kujivunjia kale kaheshima kadogo kalichobakia,ingekuwa busara zaidi kama ungekaa pembeni na kuwa mtazamaji.
Ni hayo tu.
Keynessian!