WAPO Radio watuhumiwa "kununuliwa"

WAPO Radio watuhumiwa "kununuliwa"

Status
Not open for further replies.

1954tanu

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2013
Posts
1,038
Reaction score
487
Tangu mchakato wa uteuzi wa wagombea ndani ya vyama ufanyike WAPO Radio ilionekana kuweka urari sawa wa taarifa zake kuhusiana na hali na mambo ya kisiasa ndani na nje ya vyama. Hata hivyo, tangu mikutano ya kampeni ifikie nusu ya muda wake wamiliki wa redio hiyo wameanza kushutumiwa kwamba wanaonekana kumwuunga mkono mgombea wa urais kupitia CCM.

Hivi karibuni, takribani wiki mbili, askofu Rwezaula na askofu Gamanywa (wote ni wa BSIC) wametawala vipindi vyote vya Meza ya Busara wakifafanua suala la amani. Mfano,askofu Rwezaula amezungumzia sana suala la amani akionesha kwamba eti amani huanza ndipo haki huja. Msimamo huo umeonekana kutokubalika na wasikilizaji waliowengi.

Kwa upande mwingine, inaonekana kama askofu Rwezaula amesahau au amejisahaulisha historia ya ukombozi wa mataifa ya Afrika. Historia inaonesha kwamba kukosekana kwa haki ndiko kuliko ibua Vita vya Majimaji. Afrika kusini chini ya ANC na PAC waliingia vitani dhidi ya weupe wachache kwa kuwa walinyimwa haki zao.

Askofu Rwezaula amesahau haraka mno kwamba redio yao ilikuwa ikiripoti taarifa za migomo ya madaktari, walimu, wafanyakazi mbali mbali, wanavyuo na migogoro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji; makundi hayo yote kwa ujumla wake kila moja linadai kunyimwa au kupokwa haki zake. Aidha, migogoro hiyo imeishia kwa uvunjifu wa inayoitwa amani.

Aidha,Mungu ameonesha kwamba anakerwa na watawala wasiotenda haki. Na haki ilipokosekana kwa waebrania ( wayahudi) huko Misri walipomlilia Mungu wao; akasikia kilio chao. Akamtumia Musa kuwakomboa waebrania toka kwa wamisri waliowanyima haki waebrania.
Jambo la msingi hapa ni kwa redio WAPO kutoa elimu ya uchaguzi p wa amani pasipokuegemea upande wowote.

Pamoja na hayo, askofu Gamanywa siku ya juzi alijitahidi kubainisha falsafa ya redio yake (WAPO Radio) kwamba haina mafungamano na makundi au vyama vya kisiasa ingawa bado baadhi ya wasikilizaji waliopiga simu studio walionesha mashaka kwa ufafanuzi wake.
Ni suala la kufahamu kuwa wasikilizaji wanapoanza kuwa na mashaka na kutokubaliana kwa udhahiri na chombo cha habari ni dalili mbaya.

Kwa ufupi tu, uongozi wa WAPO redio unafahamu fika kwamba vipindi vyao vya Meza ya Busara, Linalo Nishangaza, Upanga wa Roho ni miongoni mwa vipindi vyenye wasilikilizaji wengi; ni vipindi ambavyo vimekuwa ni majukwaa ya mijadala huru na wazi tofauti kabisa na mijadala mingi ya mitandaoni.. Hebu waweke kando ushabiki na upenzi wao kwa chama fulani.

Mithali 24: 24-25

===================================

Update: 13 Oct 2015

Habari hii imekanushwa kwenye hii thread=>Wapo Redio, wakanusha habari zinazodai Wamenunuliwa Kisiasa
 
Yaani ktk radio iliyonisikitisha ni hii, wapo ili kuwa na kipindi chake cha MEZA YA BUSARA, kilikuwa ni chimbuko la mijadala ya nguvu miaka yote, na wachangiaji makini sana, hata yule mtangazaji wake MBOGO, yupo makini ila kipindi hiki cha miezi hii wamiriki ndio wamekiharibu kabisa!! na hata hoja wanazozungumzia wakiulizwa maswali kuzitetea wanashindwa kabisa, ila nawashukuru wachangiaji wengi hawakubaliani kabisa na hao viongozi na iko wazi kabisa kuwa wanatumika. SASA HATUSIKILIZI LA SHEHE WALA ASKOFU, NI LOWASA TU.
 
Nilikuwa mpenzi sana wa Radio hii na Saa kumi na moja nilikuwa namsikiliza Gamanywa sasa hivi nimeacha kabisa!.Gamanywa achana na siasa za maji taka usituaminishe kuwa upinzani utaleta vurugu
 
Sisi wengine hata hatuijui. Nadhani inasikika kaeneo flani tu hukohuko Dsm.

Mabadiliko hayazuiliki na wakijaribu tu kuyazuia, yatawasomba mazima!!

Niko Shinyanga
 
Nawapongeza sana wachangiaji wa hii radio ktk kipindi cha meza ua busara. Mbogo ni mtu mzuri sana na anaendesha vizuri kipindi. Ila hawa maaskofu siwaelewi kabisa Rwezaura na Gamanywa. Wachangiaji Salvatore, Baba Ngoyai, Mzee hamis, Tilalila na wengine wengi hongereni sana kwa michango mizuri.
 
Ukawa kila mtu mbaya kanunuliwa.mshanusa kushindwa
 
Kama ndo wameshaanza hayo ki ukwel sitaisikiliza tena. Katika station niliyokuwa naipenda kuisikiliza ni wapo kwani ni wawazi. Sa kama na shekeli imeshaingia na kwao bye bye!
 
Kama ndo wameshaanza hayo ki ukwel sitaisikiliza tena. Katika station niliyokuwa naipenda kuisikiliza ni wapo kwani ni wawazi. Sa kama na shekeli imeshaingia na kwao bye bye!

Tatizo ushahidi hauna kwani Mbogo kaondolewa na vipindi vyake?
 
Nilikuwa mpenzi sana wa Radio hii na Saa kumi na moja nilikuwa namsikiliza Gamanywa sasa hivi nimeacha kabisa!.Gamanywa achana na siasa za maji taka usituaminishe kuwa upinzani utaleta vurugu

Ha ha ha ha mwaka huu ni shida lakini tarehe 25 sio mbali baada ya hapo itakua kusahau yaliyopita na kusonga mbele!
 
WAPO Radio Yatuhumiwa Kununuliwa!
Tangu mchakato wa uteuzi wa wagombea ndani ya vyama ufanyike WAPO Radio ilionekana kuweka urari sawa wa taarifa zake kuhusiana na hali na mambo ya kisiasa ndani na nje ya vyama. Hata hivyo, tangu mikutano ya kampeni ifikie nusu ya muda wake wamiliki wa redio hiyo wameanza kushutumiwa kwamba wanaonekana kumwuunga mkono mgombea wa urais kupitia CCM.

Hivi karibuni, takribani wiki mbili, askofu Rwezaula na askofu Gamanywa (wote ni wa BSIC) wametawala vipindi vyote vya Meza ya Busara wakifafanua suala la amani. Mfano,askofu Rwezaula amezungumzia sana suala la amani akionesha kwamba eti amani huanza ndipo haki huja. Msimamo huo umeonekana kutokubalika na wasikilizaji waliowengi.

Kwa upande mwingine, inaonekana kama askofu Rwezaula amesahau au amejisahaulisha historia ya ukombozi wa mataifa ya Afrika. Historia inaonesha kwamba kukosekana kwa haki ndiko kuliko ibua Vita vya Majimaji. Afrika kusini chini ya ANC na PAC waliingia vitani dhidi ya weupe wachache kwa kuwa walinyimwa haki zao.

Askofu Rwezaula amesahau haraka mno kwamba redio yao ilikuwa ikiripoti taarifa za migomo ya madaktari, walimu, wafanyakazi mbali mbali, wanavyuo na migogoro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji; makundi hayo yote kwa ujumla wake kila moja linadai kunyimwa au kupokwa haki zake. Aidha, migogoro hiyo imeishia kwa uvunjifu wa inayoitwa amani.

Aidha,Mungu ameonesha kwamba anakerwa na watawala wasiotenda haki. Na haki ilipokosekana kwa waebrania ( wayahudi) huko Misri walipomlilia Mungu wao; akasikia kilio chao. Akamtumia Musa kuwakomboa waebrania toka kwa wamisri waliowanyima haki waebrania.
Jambo la msingi hapa ni kwa redio WAPO kutoa elimu ya uchaguzi p wa amani pasipokuegemea upande wowote.

Pamoja na hayo, askofu Gamanywa siku ya juzi alijitahidi kubainisha falsafa ya redio yake (WAPO Radio) kwamba haina mafungamano na makundi au vyama vya kisiasa ingawa bado baadhi ya wasikilizaji waliopiga simu studio walionesha mashaka kwa ufafanuzi wake.
Ni suala la kufahamu kuwa wasikilizaji wanapoanza kuwa na mashaka na kutokubaliana kwa udhahiri na chombo cha habari ni dalili mbaya.

Kwa ufupi tu, uongozi wa WAPO redio unafahamu fika kwamba vipindi vyao vya Meza ya Busara, Linalo Nishangaza, Upanga wa Roho ni miongoni mwa vipindi vyenye wasilikilizaji wengi; ni vipindi ambavyo vimekuwa ni majukwaa ya mijadala huru na wazi tofauti kabisa na mijadala mingi ya mitandaoni.. Hebu waweke kando ushabiki na upenzi wao kwa chama fulani.

Mithali 24: 24-25

Hata hueleweli! unawayawaya tu kumtetea fisadi Lowasa.
 
Mtanzania wa jana sio wa leo,pindi unapofanya kinyume watu wanakuelewa ndani ya dk moja HATUPASWI KUSHINDANA NA MAJIRA BALI ITATULAZIMU KUYAFUATA MAJIRA HATA KAMA HATUTAKI.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom