Wapiga debe wametushinda akili?

Wapiga debe wametushinda akili?

Mkyamise

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2014
Posts
526
Reaction score
677
Ni wazi kwamba serikali inajitahidi kujenga miundombinu kama stendi. Kinachokera ni hili kundi la wapigadebe.

Mfano pale stedi mpya ya Nyamhongolo Mwanza, yaani ukishuka tu kwenye Hiace zinazotoka mjini, unaweza kupokelewa na wapigadebe hata 10 wakikuuliza Musoma, Tarime, Sirari, Bariadi n.k.

Kero kubwa sana hii. Imagine umetoka zako huko ulikotoka na unapoenda unapafahamu na hata usafiri wa kwenda unakoenda unaufahamu mathalan majina ya magari yanayoenda unakoelekea.

Anatokea mtu anakuuliza unakoenda? Stupid! Wametushinda?
 
Nishawah pigwa Kwa sababu ya kukatia tiketi vichochoroni
 
Lakini wanasaidia Sana Kama ni mgeni wa eneo na usiwe na mzigo la sivyo utaona yule kachukua begi mwingine kipeto na mwingine mtoto.
 
Wapiga debe ndio roho ya wenye mabasi especially yale mabasi yasio na majina makubwa.

Mfano mi sahivi ukiniuliza gari la kwenda Dodoma nitasema Shabiby na Kimbinyiko tu kwasababu ndio yana majina makubwa.

Ila abiria akifika pale wapiga debe wanawapeleka kwenye yale majina madogo hafu wanapata kamisheni.
 
Wakale wapi,wakiiba wachomwe....wanajitafutia pia kero.Bhana,hutaki waambie sitaki hawamgandi MTU Mwenye msimamo
 
Nimepiga debe sana, nimeibia watu sana, nimetukana matusi sana kipindi napiga debe, na sabatoni natia timu kila jumamosi. Mbinguni pia nitatia timu ....
 
Hii kero nimekutana nayo jana stendi mbezi Luis madalali wamening'ang'ania naenda mkoa gani na nilikua na mtoto(8) wakawa wanamvuta nikawaambia sisafiri kuweni wastaarabu nikamshika mkono mwanangu tuondoke aloo! Nimetukanwa hata kosa langu silijui
 
Back
Top Bottom