WAPI TAIFA LINAELEKEA

expirience man

JF-Expert Member
Nov 16, 2013
212
90
Binafsi nachoshwa sana jinsi mambo vile yanakwenda! wakati bado hatujajua hatma ya Ben Focus saanane nini kimemtolkea, siku si nyingi mara tukasikia Ney wa mitego amekamatwa na baadae kuachiwa kwa tamko la Mh Rais John Magufuli. Lakini bado wakati Ney \akituambia kuwa yu na mashaka makuu juu ya usalama wa maisha yake, mara msanii mwingine MUSA IBRAHIM maarufu kama ROMA MKATOLIKI tukapata habari katekwa na watu wasiojulikana.
Mkuu wa mkoa wa DSM baada ya kufuatwa na na wasaniii kumuomba awasaidie kutia nguvu kwenye kumtafuta Roma akawaahidi kuwa atapatikana kabla ya jpili. Sio lengo langu kumtuhumu yeyote ktk haya kwa kluwa naaminbi vyombo vya ulinzi na usalaama vinafanya kazi yake ipasavyo kutulinda raia, lakini hapa kluna sintofahamu nyingi sana na maswali kibao tunayapata kama raia linapokuja suala la usaalama wetu kama kM rai wa nchi. Inakuwaje mtu anatekwa halafui wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama wa raia na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wanagongana kauli. Mmoja anasema atapatikana kabla ya jpili huku mwingine akisema hawezi kusema kwa kuwa ni suala la upelelezi ningumu kujua atapatikana lini.na kweli leo jmosi Roma AMEPATIKANA.
kama wananchi wapenda amani , uhuru wa kueleza mawazo yetu na tunaamini ktk demokrasia ya kweli tena ktk zama kama hizi za uwazi tunapata taabu sana kuona watu wanapotea kiaina tena wanapoonekana wana mawazo tofauti wa walio kwenye nyadhifa. Hapa kuna jambo la kuiambia serikali yetu pendwa tulioichagua kjuwa ili kuwatoa wananchi mashaka kluwa inahusika kwa namna yeyote juu ya kutoweka kwa raia wake, inapaswa kuimarisha ulinzi maana inaweza kuwa maadui nwaserikali wanatumia udhaifu mdogo tu ktk serikali wa kuminya uhuru wa habari kuteka watu ili serikali ichukiwe hata kama serikali haihusiki kwa namna yeyote.
Tutoe raia kwa vyombo vya ulinzi na usalama kuwa jukumu la kulinda usalama wa raia liko mikononi m,wao tukishirikiana na sisi wananchi. Tukubali kukosolewa ili kuijenga nchibyet na ukosoaji ulenge kwenye nia njema ya kujenga zaidi kuliko kuumbua au kudharirisha mtu ama taasisi anayoiongoza.
 
Yaani in short hizi drama za nchi yangu zinanifanya naanza kukosa mapenzi nayo maana kila siku hiki mala kile ifike point tujikite na harakati za maendeleo sio hizi harakati za kuzungumzia mtu mmoja mmoja na kukosa focus taifa kama taifa.
 
Bashite anaanza kutuzoeza mambo ya utekaji, baadae watapotezwa viongozi wakubwa wa upinzani.
 
Umeandika weeeeeeee

Mwisho wa siku Kamanda Sirro kawaambia acheni haya ya kudakua kidakua kama vile ni kazi yenu.

Sikufichi nimekusoma hadi karibu na mwisho na kuona, hujafikiria bali umedakua yanayosambaa yaliyojaa vioja na kuyaunga. Halafu eti


Na ni nyie wafata mikumbo ya yanayoanzishwa na wachache kwa salahi yao binafsi na madawa, ndio mnataka kupeleka nchi pabaya. Shukurani kwa Mhe. JPM yupo hatua 5 mbele.

Makonda oyeeeeee
 
Back
Top Bottom