Sesten Zakazaka
JF-Expert Member
- Sep 10, 2017
- 10,561
- 19,056
Ulikua ni mchezo maridhawa wenye taratibu na kanuni zilizosukwa vizuri sana. Kuna kiduara kinachorwa zikawekwa gololi zikiitwa kwenye mchezo "mali", ambazo wachezaji wote wanachangia kwa idadi sawa kinaitwa KIDU. Mbele ya kidu kama mita nne au tano unachorwa msatati mrefu ambapo wachezaji watarusha gololi zenye ukubwa tofauti na zile walizowekwa kwenye kidu ili kuamua nani atakua wakwanza kucheza, gololi hizo tofauti zinaitwa BENTO.
Wakati wa kurusha bento kwenye ule mstari mnakua wote mmesimama usawa wa kidu na yule ambae bento lake litaukaribia zaidi mstari bila kuuvuka ndio anaanza kucheza. Bento likivuka mstari unaambiwa umetoka PAKE na kama kutakua hakuna aliyetoka pake basi wewe utakua wa mwisho kucheza. Wakati wa kucheza unarusha bento kuelekea kwenye kidu ili ule "mali" kwa kuzipiga gololi zitoke nje ya duara la kidu. Ukifanikiwa kuzitoa basi unaendelea wewe kucheza hadi umalize mali zote au ukose ndio aje mwingine. Bento likikwama kwenye kidu unaambiwa ume SITI na unarudisha kwenye kidu mali zote ulizokula. Pia unaweza usirushe bento moja kwa moja kwenye kidu kutokana na umbali hivo ukalirusha tu karibu na kidu halafu akasubiri mwingine acheze ili akikosa wewe uwe karibu na mali, hiyo inaitwa ume CHUNGI. Lakini anaekufatia kucheza atakua pamoja na kukusudia kupiga kwenye kidu pia atakua analenga bento lako na akikugonga anachukua mali zote ulizokula. Hii inaitwa KUTINYA au KUTINYISHWA
Pia kabda hujacheza hakikisha una nuia kwanza maneno yafutayo , "KIDU NA MALI NA BENTO VYOTEVYOTE" halafu unaendelea kucheza vinginevyo una tinya mali zote kama huja nuia. Kama umekula mali za kutosha na hutaki tena kuendelea na mchezo unasema SALATI na wenzako ama wanaendelea au wanagawana mali zilizobakia
Nimekaa kwenye mapumziko haya ya mwisho wa mwaka nikaona watoto wanachezea toys zao ambazo kila kitu kiko inbuilt hakuna skill yoyote wanayotumia zaidi ya kujua ku oparate toys, nikajikuta najiwazia tu tulipotoka. Lakini wakati ukuta, kila zama na kitabu chake na huu ni wakati wao
Wakati wa kurusha bento kwenye ule mstari mnakua wote mmesimama usawa wa kidu na yule ambae bento lake litaukaribia zaidi mstari bila kuuvuka ndio anaanza kucheza. Bento likivuka mstari unaambiwa umetoka PAKE na kama kutakua hakuna aliyetoka pake basi wewe utakua wa mwisho kucheza. Wakati wa kucheza unarusha bento kuelekea kwenye kidu ili ule "mali" kwa kuzipiga gololi zitoke nje ya duara la kidu. Ukifanikiwa kuzitoa basi unaendelea wewe kucheza hadi umalize mali zote au ukose ndio aje mwingine. Bento likikwama kwenye kidu unaambiwa ume SITI na unarudisha kwenye kidu mali zote ulizokula. Pia unaweza usirushe bento moja kwa moja kwenye kidu kutokana na umbali hivo ukalirusha tu karibu na kidu halafu akasubiri mwingine acheze ili akikosa wewe uwe karibu na mali, hiyo inaitwa ume CHUNGI. Lakini anaekufatia kucheza atakua pamoja na kukusudia kupiga kwenye kidu pia atakua analenga bento lako na akikugonga anachukua mali zote ulizokula. Hii inaitwa KUTINYA au KUTINYISHWA
Pia kabda hujacheza hakikisha una nuia kwanza maneno yafutayo , "KIDU NA MALI NA BENTO VYOTEVYOTE" halafu unaendelea kucheza vinginevyo una tinya mali zote kama huja nuia. Kama umekula mali za kutosha na hutaki tena kuendelea na mchezo unasema SALATI na wenzako ama wanaendelea au wanagawana mali zilizobakia
Nimekaa kwenye mapumziko haya ya mwisho wa mwaka nikaona watoto wanachezea toys zao ambazo kila kitu kiko inbuilt hakuna skill yoyote wanayotumia zaidi ya kujua ku oparate toys, nikajikuta najiwazia tu tulipotoka. Lakini wakati ukuta, kila zama na kitabu chake na huu ni wakati wao