Wadau kumekuwa na ongezeko la wanawake wenye ndevu
na kwa ujumla wanawake hawa wamekuwa wanapata shida sana ikija swala la kuolewa.
Kijana wa kiume anapata shida kwenda kumtambulisha kwao wakati mwanamke ana ndevu kuzidi hata za baba mkwe.
Ebu tujuzane wadau, Hii mambo inasababishwa na nini? Je inamaana gani kwa mwanamke?
Wana wake wa aina hii wanasuti ya nne!
Tuelimishane ili tuwasaidie wadada wapate wachumba waolewe.
Ni tatizo la kihomoni. Wajuzi watadadavua zaidi.
Wapo walioolewa bila shida yoyote.
Tena mimi nawapenda sana sema baadhi yao hawana tabia njema kivile.
Nikimpata wa kufanana nami namchukua fasta ili wakija wavamizi/wezi wanajua kuna vidume viwili.
Kama sauti yake ni nyembamba lazima aiungurumishe. Vibaka watatoka nduki.
dah we jamaa umenifanya nicheke hapo kwenye kuwatambulisha. Ndevu na sauti nene labda ni ishu ya kibaolojia na pengine labda hormone hazijabalance, kuna mdau mmoja humu aliwai kusema wanawake wa dizain hiyo ndo ugonjwa wake... Ngoja aje hapa tujifunze kitu
Inasikitisha yani,unakuta ukimuona mtu pap unapanic huyu wa kike au kiume
Baadhi yao zimeota zimekua nyingii kabisaa,madawa ya hormone yale huwa hayasaidii Kwani?