Wanawake wametufanya tuwe na tamaa ya kulipiza kisasi

harder king

JF-Expert Member
Jan 21, 2017
3,970
6,898
Habari za mda huu wana JF bila shaka mpo poa,

Leo nimekuja na uzi mpya japo naisi yaweza kua chanzo cha uzi nilizowahi kuleta hapa karibuni. Niliwai kuingia kwenye mahusiano na dada mmoja alikuja likizo kwa dada yake ilikua mwaka 2010 basi nikawa nimevutiwa nae nikaona siyo mbaya nikamtokea, bila hiana akanikubalia tukawa kwenye mahusiano kama wachumba na lengo baada ya masomo tuje tuoane.

Alirudi kwao kuendelea na shule kipindi hicho alikua yupo from2 tangu hapo hatukuonana tena zaidi ya mawasiliano ya kwenye simu japo alikua mbali lakini tulikua karibu kimawasiliano kiasi kwamba kila mmoja hakuona madhara ya long distance, tuliendelea hivyo hadi alipofika form4.

Mambo yalianza kubadilika ilipokua imebak mwezi mmoja kufanya mitihani ya kumaliza frm4, ikawa nikituma msg hazijibiwi kwa wakati, ukipiga simu haipokelewi, ikitokea akijibu msg ni usiku wakati mwanzoni ilikua mda wote anapatikana(hapa msiniulize alikua anatumiaje simu darasani taratibu za shule yao czijui)basi ilipita kama wiki mbili hapatikani kabisa kwenye simu.

Ilikua wakati mgumu kwangu maana mtu nimemsubiri kwa miaka mi3 na tulishakubaliana akimaliza frm4 atakuja na kama ataendelea na olevel tutaendela kuvuta mda, ila ilikua lazima tuonane baada ya 4m4, wiki mbili zilivyoisha dada yake ambae yupo karibu na ninakofanyia kazi alinipigia simu akanambia vipi unajua R aliko maana ametoroka nyumbani na inasemekana yupo kwako, nikamwambia ata mawasiliano nae sina.

Basi hapo nikawa njia panda, mtu nlie msubiria kwa mda wote kayeyuka ghafla, siku tatu badae mtoto karudi hewani kanipigia ila hawamu hii akiwa anaongea kwa uzuni, eti kwao hawampendi na aliamua kutoroka na mama mmoja kwenda Morogoro kufanya kazi ila alipofika akakuta yule mama ni mamapoa na anataka na yeye awe dada poa, kwa hiyo anaomba nimtumie nauli harudi nyumbani akafanye mtihani, nilijisikia vibaya kwa alivyonielezea maana kama ni kutengeneza maneno aliweza na yakaniteka kweli.

Akanambia nauli ni elf 40 hadi kufika, nikajikakamua nikamtumia, nakumbuka nilituma mida ya saa nne asubui ilipo fika saa5 usiku dada yake alinipigia simu akanambia ndugu zake wamempigia simu kua hali yake ni mbaya amelezwa hospital ya Mwananyamala baada ya kufanya abortion.

Iliniuma sana nilishindwa kumwambia kama alinidanganya yupo Moro kilicho niuma zaidi ni kwamba hela niliyoambiwa ni ya nauli ndio ilitumika ku abort, sikutaka kujua hali yake tena nilikaa kimya nikiugulia maumivu ya moyo, baada ya siku 2 nilitumiwa msg na mtu aliejiita dada yake akidai ndugu yao alikua na uvimbe tumboni amefanyiwa oparation na hawana fedha za kulipa na wanaomba msaada wangu, nilimwambia amtafute aliempa ndugu yao hiyo mimba ndio amweleze huo upuuzi alijitaidi kunibishia siyo mimba ila ukweli nilishaujua.

Nlikata mawasiliano nae nikafuta hadi namba zake, baada ya miezi mi 4 alinitafuta akitaka turudishe husiano wetu kwani shetani alimpitia, nilimuliza mimba uliotoa ilikua ya nani kanambia ni ya mwalimu aliekua anafundisha shuleni kwao, nilimkatalia nikamkatia simu, baadae alikuja kwa dada yake ambae kikazi tupo karibu na alitumia mda mwingi kuniomba msamaha na kuniomba turufishe uhusiano, kiukwel niseme mapenzi ni upofu maana juhudi zake zilizaa matunda na tukarudiana ila sikua na imani nae tena.

Kuna siku dada yake alinifuata kanambia huyu mtu hakufai tena tafuta mtu mwingine huyu atakupotezea mda tu na alinipa sababu nyingi na kweli haikupita mda kuna jamaa alikua anafanya TANESCO alimuhonga simu nadhani ata papuchi alikula huku mimi nikiendelea kusubiri meli airport.

Niliamua kuachana nae mazima, maisha yalienda nikaja pata habari aliolewa na jamaa flani huko kwao na walikua na mtoto mmoja, kuna siku alinipigia simu akanieleza nukamwambia hongera ila utulie na ukumbuke huna kitu kwangu na huna haja ya kua na namba zangu wakati zako nishafutiaga mbali.

Baada ya hapo nilikuja kua na mahusiano na mdada mwingine niliesomaga nae primary wakati huo alikua ametoka Moshi kuja kusoma chuo cha unesi Manyara, tulianza kidogo kidogo na badae tukawa wachumba, huyu nae hakuonyesha ile deep relationship mara nyingi mimi ndio nilikua namtafuta, nakumbuka kuna siku nilienda kumtembelea chuoni nilipata ajali mbaya namshukuru Mungu haikua na madhara makubwa kwangu, ilibidi nihairishe safari na nikachukua lodge nikalala, asubui nikajianda nikamnunulia vitu vingine maana nilivyokuja navyo viliharika baada ya ajali, nilipofika chuoni nilimtuma rafiki yake akamuite ilichukua mda na alikuja kama vile kalazimishwa wala hakunipa pole kwa ile ajali.

Tulipeana salam na akanambia kuna kazi ameacha wordini anarudi kuifanya nikampa nilicho mletea ila nlijisikia vibaya sana maana hakua kama siku zingine nilimuliza kwanini akanambia yupo sawa nisiwe na wasi wasi, siku zilienda na akakaribia kumaliza chuo baada ya miaka mi2, alipomaliza aliniaga kua anaenda nyumbani na atakuja kwangu wakati wa kuja kuchukua cheti chuoni, alipoenda kwao mawasiliano yakawa kama ya yule mwingine ikawa ndio kuachana kwenye mataa.

Maisha kama kawaida yalisonga na baadae nikampata msichana karibu na mtaa niliokua naishi huyu sikua na mpango wa kumuoa tena maana nilishaumizwa vya kutosha nlishaamua dawa ni kula papuchi na kutembea mbele, alikua karibu sana na mimi nakumbuka ilifika mahali nampa hadi funguo za nyumba akanifanyie usafi(nilikua napanga ila tiari nilishakua na nyumba ya room mbili za kishkaji).

Basi nikaona hiyo ndio chance tena kwangu, kiukweli alikua mjanja na alishajua njama zangu ilikua kila akija kuchukua funguo anampitia mdogo wake wanaenda wote, nilitafuta mbinu za kumgegeda lakini sikuweza nae alikazia nimuoe ndio anipe, baada ya mda alinambia amepata nafasi ya kwenda Dodoma kusoma, hapo sikua na haja ya kua msndikizaji tena alipoondoka ikawa mwisho wetu.

Baadae nilikuja ingia kwenye ujusiano mwingine na tuliamua kuishi pamoja japo akuwa na vigezo nlivyovitaka ila nlijipa moyo atabadilika na kua na vigezo nnavyovitaka japo haikua ivyo hadi sasa, kiukweli kumbadilisha mtu mliekutana ukubwani ni kazi, nakumbuka kuna siku nipo na dada wa yule msichana wa kwanza akawa ananipa story zake kua alishaachana na jamaa yake na yupo Dar kwa ndugu zake na mimi nilikua na safar za Dar mara kwa mara nikaona huu ndio mda wa kujipunguzia machungu.

Nlimuomba namba na alinipa siku nikiwa Dar nikamcheki wala hakua mbishi alikuja niliko na nikafanya kile anachokipendaga shetani, nilishapanga kuwarudia ma x wote walio nitenda kwa ajili ya papuchi zao tu ila badae nilikuja mrudia Mungu na kubatilisha mpango huo.

Japo kwa sasa nahisi ile roho inanifuata kwa mbali baada ya mitikisiko ya matherhouse wangu, lengo la uzi huu siyo kusimulia yalionitokea, hapana baada ya kumaliza kusoma siyo mbaya ukaniachia ushauri utakaonisaidia kisikologia maana nikiwaza niliopitia na ninayopitia naona kama the same way.
 
16465258_979640912167227_6674285345833484288_n.jpg
 
Pole sana ,ndio maisha yalivo,muhimu concentrate na maisha yako na shughul zako,binadamu tumeumbiwa mitihan iyo ni moja wapo,muhim sahau yote ya nyuma na move on ,look forward yaliopita yashapita.muhimu umzima wa afya basi ushukuru.hayo mengine yote ni mapito ya dunia haina haja ya kiyaweka kichwan yakakuongezea mzigo kichwan,hamna binadam aliekamilika.
 
Kwanini upoteze muda na nguvu yako kulipiza kisasi? Ulipize kisasi ili iweje? Umetendwa chukua 50 zako endelea na maisha yako badala ya kuanza kukaa chini kupoteza muda chungu nzima wa kufikiria namna ya kulipiza kisasi.
 
Kaa tulia,....kimsing ushecheza saana. Tafuta mtu atleast atakae kuwa na vigezo unavyotaka sio lazima viwe vyote....

Umri unaenda, Magonjwa....

Shika njia ya imani
 
Actually umeathirika kisaikolojia kwa kiasi fulani.Ninakulaumu kwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanafunzi wa form two.Hata hivyo kuna kosa la kiufundi ulilifanya.Mtoto wa kidato cha pili uwekeane ahadi za kuoana!?Ana safari ndefu.Bado hajakutana na watu tofauti na wewe,bado hajakutana na pilikapilika za mapenzi...
Tatizo naloliona kwako ulikuwa unaingia mazima mazima kwenye mahusiano.Na kila uliyekutana naye ulitamani awe the woman of your life!
Mapenzi hayako hivyo.Tena una bahati ukutoa hela yako kumsomesha mtu.Tungekuwa tunaongea mengine muda huu(mchumba hasomeshwi).
Tuliza akili yako,mwenzi wako atakuja automatically.Tatizo vigezo mnavyokuwa mnajiwekea.Oho...nataka awe msomi,awe mfanyakazi wa kuajiriwa serikalini au kwenye mashirika,nataka awe hivi au vile.Kumbuka naye ana vigezo vyake.
 
Pole sana ,ndio maisha yalivo,muhimu concentrate na maisha yako na shughul zako,binadamu tumeumbiwa mitihan iyo ni moja wapo,muhim sahau yote ya nyuma na move on ,look forward yaliopita yashapita.muhimu umzima wa afya basi ushukuru.hayo mengine yote ni mapito ya dunia haina haja ya kiyaweka kichwan yakakuongezea mzigo kichwan,hamna binadam aliekamilika.
Nashukukuru mkuu
 
Actually umeathirika kisaikolojia kwa kiasi fulani.Ninakulaumu kwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanafunzi wa form two.Hata hivyo kuna kosa la kiufundi ulilifanya.Mtoto wa kidato cha pili uwekeane ahadi za kuoana!?Ana safari ndefu.Bado hajakutana na watu tofauti na wewe,bado hajakutana na pilikapilika za mapenzi...
Tatizo naloliona kwako ulikuwa unaingia mazima mazima kwenye mahusiano.Na kila uliyekutana naye ulitamani awe the woman of your life!
Mapenzi hayako hivyo.Tena una bahati ukutoa hela yako kumsomesha mtu.Tungekuwa tunaongea mengine muda huu(mchumba hasomeshwi).
Tuliza akili yako,mwenzi wako atakuja automatically.Tatizo vigezo mnavyokuwa mnajiwekea.Oho...nataka awe msomi,awe mfanyakazi wa kuajiriwa serikalini au kwenye mashirika,nataka awe hivi au vile.Kumbuka naye ana vigezo vyake.
Nmekuelewa mkuu,asante
 
Yeah,mi nadhani tumpe pole tu maana wanawake wengi siku hizi ni matapeli wazuri wa mahusiano,hawaaminiki gata kidogo! Mkiongea mipango asubuhi mchana akikutana na mwingine mipango ishaharibika,bado haijafika jioni.Ndivyo siku hizi walivyo.hawana misimamo
 
Sijui umri wako ila kama una tabia ya kupenda "wakike" utaumia sana tafuta wasichana wa umri wako

sio kila ukiona sketi dushe linakusimama.

Jiwekee malengo kuwa kamwe sitoweza kulala na mdada wa umri fulani

hii itakusaidia kukutana na mdada aliye tiyari.

Mm ni mwanamke ila tangu nikiwa mdogo nilijiwekea msimamo kuwa hata kwa dawa " sitoweza kuwa na mahusiano na under 30 boys" the same age? Ahaa wapi nilitamani mwanaume anizidi hata niaka 4 au tano na hilo nimefanikiwa ka %zotee

tafuta mdada ambae aliishaanza maisha anajua kutafuta pesa hana hulka na vitu vidogo vidogo trust me utafanikiwa wapo ambao wako tiyari kwa serious relationship.
 
Aah wapi......wote tamh9aa tu aisee,hamna cha mkubwa wala mdogo,tena afadhali ya mdogo kuliko mkubwa mwenye Experience!
 
Pole sana...
Kama umeumizwa kwenye uhusiani usikimbilie kuingia kwenye uhusiano mwingine haraka. Tuloa jipe mda wa ku-detox. Unaeza tafuta sex mates wa kutolea stress ila usitue moyo wako hapo. Kama unaweza kuepuka sex kabisa itakua vizuri... Kua bize na mambo mengine ya kukuletea maendeleo. Utampata mdada unaeona atakufaa alafu anza kua nae polepole.
 
Sijui umri wako ila kama una tabia ya kupenda "wakike" utaumia sana tafuta wasichana wa umri wako

sio kila ukiona sketi dushe linakusimama.

Jiwekee malengo kuwa kamwe sitoweza kulala na mdada wa umri fulani

hii itakusaidia kukutana na mdada aliye tiyari.

Mm ni mwanamke ila tangu nikiwa mdogo nilijiwekea msimamo kuwa hata kwa dawa " sitoweza kuwa na mahusiano na under 30 boys" the same age? Ahaa wapi nilitamani mwanaume anizidi hata niaka 4 au tano na hilo nimefanikiwa ka %zotee

tafuta mdada ambae aliishaanza maisha anajua kutafuta pesa hana hulka na vitu vidogo vidogo trust me utafanikiwa wapo ambao wako tiyari kwa serious relationship.

maybe mademu ambao mtoa mada aliwapenda hawakuwa wanampenda yeye kama alivowapenda wao luckyline
 
Mwanamke ni mtu wa kukaa nae kwa akili sana hata vitabu vya dini vinatuhimiza jambo hilo.

Take your time first, then usikubali kuendeshwa na tamaa/hamu za mwili kwa wakati huo, no jipe muda na pia usitake kwako jambo la mahusiano liwe "A Must do thing"
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom