muzi
JF-Expert Member
- Jun 17, 2016
- 1,046
- 1,473
Ni jambo la wazi wanawake wengi wanaangikia kwenye dimbwi la mapenzi pasipokupenda kwa sababu mbalimbali. Kuna shoga zangu wanajikuta huko sababu ya mimba za bahati mbaya, wengine kama kiki ya kulazimisha kuolewa, wengine kujirahisisha ili kupendwa, wengine kisingizio cha kumkamata dume ili akuoe na sababu kadha wa kadha.
Sasa leo siangalii hayo, tuchukulie kama imetokea maana imepangwa/haijapangwa. Cha kushangaza baada ya kutokea hayo, wanawake wanajishahau kufanya lolote liwezekanalo ili sasa kuhalalisha mahusiano yawe rasmi kupitia kanisani, msikitini, serikalini au hata njia za jadi. Wanaume huwa wanatuchezea danadana sana kuwa ngoja maisha yakae kwenye mstari ndipo tuhalalisha swala la NDOA kwa kusingizia kujenga, kupata misingi imara ya kipato/kazi/ajira, wengine kununua gari na sababu zingine nyingi ili mradi akuchezee mpaka uzeeke.
Inaleta hasira sana nimekutana na shoga zangu wamezaa mtoto wa 1, 2, 3 mpaka wa 4 bado hajahalalisha ndoa. Hii ndo tunaisha uchumba SUGU. Uuuwiiiiii jamani sasa sijui tuwaweke kundi lipi, maana mwanamke kila mwaka unapanua tuu unatotoleshwa hata hufikirii kuweka ngumu swala la ndoa. Unaishi na mwanaume miaka 4, 5,7 hata wengine 10, sijui tuwaite wachumba sugu, nafikiri mtanisaidia jina zuri.
Unajua haya maisha yanapita kuna leo na kesho linaloweza kutokea mfano kifo, ajali na mengine yatakayokuondosha katika uimwengu huuu. Sasa kwa wale waumini wazuri wa dini kama ukifika hujaweka mambo mazuri ya ndoa inaleta shida kidogo kiimani, kwa watoto, kwa wazazi wako mke na jamii nzima kwa ujumla.
Wanawake tuamke jamani, hizi ahadi za kuahirisha ndoa kila mara zinatuweka pabaya, hata HESHIMA ya ndoa haipo wapendwa. Tusitake kufurahisha ulimwengu kwa ndoa/harusi za mamilioni kisa tu nionekane, tuangalie roho zetu na uondokapo duniani hao watoto utawaacha katika mazingira gani. Fanya sherehe simple that's all!
Shoga zangu Tupinge vikali Uchumba Sugu ni AIBU jamani, hata kama tulifanya makosa kuingia huko turekebishe hayo makosa, tunajisahau sana.
Hope nimesomeka vizuri.
Thanks and Take Care!
Sasa leo siangalii hayo, tuchukulie kama imetokea maana imepangwa/haijapangwa. Cha kushangaza baada ya kutokea hayo, wanawake wanajishahau kufanya lolote liwezekanalo ili sasa kuhalalisha mahusiano yawe rasmi kupitia kanisani, msikitini, serikalini au hata njia za jadi. Wanaume huwa wanatuchezea danadana sana kuwa ngoja maisha yakae kwenye mstari ndipo tuhalalisha swala la NDOA kwa kusingizia kujenga, kupata misingi imara ya kipato/kazi/ajira, wengine kununua gari na sababu zingine nyingi ili mradi akuchezee mpaka uzeeke.
Inaleta hasira sana nimekutana na shoga zangu wamezaa mtoto wa 1, 2, 3 mpaka wa 4 bado hajahalalisha ndoa. Hii ndo tunaisha uchumba SUGU. Uuuwiiiiii jamani sasa sijui tuwaweke kundi lipi, maana mwanamke kila mwaka unapanua tuu unatotoleshwa hata hufikirii kuweka ngumu swala la ndoa. Unaishi na mwanaume miaka 4, 5,7 hata wengine 10, sijui tuwaite wachumba sugu, nafikiri mtanisaidia jina zuri.
Unajua haya maisha yanapita kuna leo na kesho linaloweza kutokea mfano kifo, ajali na mengine yatakayokuondosha katika uimwengu huuu. Sasa kwa wale waumini wazuri wa dini kama ukifika hujaweka mambo mazuri ya ndoa inaleta shida kidogo kiimani, kwa watoto, kwa wazazi wako mke na jamii nzima kwa ujumla.
Wanawake tuamke jamani, hizi ahadi za kuahirisha ndoa kila mara zinatuweka pabaya, hata HESHIMA ya ndoa haipo wapendwa. Tusitake kufurahisha ulimwengu kwa ndoa/harusi za mamilioni kisa tu nionekane, tuangalie roho zetu na uondokapo duniani hao watoto utawaacha katika mazingira gani. Fanya sherehe simple that's all!
Shoga zangu Tupinge vikali Uchumba Sugu ni AIBU jamani, hata kama tulifanya makosa kuingia huko turekebishe hayo makosa, tunajisahau sana.
Hope nimesomeka vizuri.
Thanks and Take Care!