Zaidi ya watu wa5 wameshakueleza kwamba jamaa
hana time na wewe na ameshachumbia.mtu
mwingine hukuamini...Mungu sio Mwigulu
Nchemba,siku 1 akiwa kwenye mishemishe za
kuchepuka Simu yake ikajipiga ukamsikia anaongea
na msichana.mwingine...na baada ya muda ukawasikia wanapiga Kwinchi Kwinchi Live wakati
alikuaga muda huo yuko kwenye kikao cha
harusi....Munguakaamua kukuonyesha kitu
live..Ulipomuuliza akaruka futi elfu6 kwamba
unamsingizia.Una kila ushahidi kwamba huyo jamaa
nikimeo ila kwa sababu akili yako ina Ujibwa Ulezi uliochanganywa na Alizeti UKAMSAMEHESasa leo
amekuoa na tabia zilezile walizokuonya rafiki zako
zimeendelea,unashinda unalia na kuimba Pambio la
BWANA TENDA MUUJIZA USIACHE MWAKA HUU
UPITE.Alishatenda Muujiza kukuonyesha ushahidi
hukutaka kumsikia,Ukapenda zaidi Matarumbeta ya Harusi bila Kujali Ndoa itakuwaje...Pole,Hakuna
Muujiza hapo,jipigie matarumbeta kwa
Kujitendeamuujiza.Kamwe usidharau Mungu
akikuonyesha Clear Signs kwamba mtu uliyenaye ni
shida.Using'ang'anie kuwa Mjumbe wa Bunge la
Katiba kama Unahisi Posho haitoshi..AchiaNgazi...Heri ukose Harusi leo ujiandae kwa Ndoa bora ya
Keshokutwa.