Wanawake, msing'ang'anie wanaume ambao hawawataki

STUNTER

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2015
Posts
13,077
Reaction score
17,262
Zaidi ya watu wa 5 wameshakueleza kwamba jamaa hana time na wewe na ameshachumbia mtu mwingine hukuamini. Mungu sio Mwigulu Nchemba, siku 1 akiwa kwenye mishemishe za kuchepuka simu yake ikajipiga ukamsikia anaongea na msichana mwingine na baada ya muda ukawasikia wanapiga kwinchi kwinchi Live wakati alikuaga muda huo yuko kwenye kikao cha harusi. Mungu akaamua kukuonyesha kitu live.

Ulipomuuliza akaruka futi elfu 6 kwamba unamsingizia una kila ushahidi kwamba huyo jamaa ni kimeo ila kwa sababu akili yako ina ujibwa ulezi uliochanganywa na alizeti ukamsamehe, sasa leo amekuoa na tabia zilezile walizokuonya rafiki zako zimeendelea, unashinda unalia na kuimba Pambio la bwana tenda miujiza usiaache mpaka mwaka huu upite.

Alishatenda muujiza kukuonyesha ushahidi hukutaka kumsikia, ukapenda zaidi matarumbeta ya harusi bila kujali ndoa itakuwaje. Pole hakuna muujiza hapo, jipigie matarumbeta kwa kujitendea muujiza. Kamwe usidharau Mungu akikuonyesha (clear Signs) kwamba mtu uliyenaye ni shida. Using'ang'anie kuwa mjumbe wa bunge la katiba kama unahisi posho haitoshi achia ngazi.

Heri ukose harusi leo ujiandae kwa ndoa bora ya keshokutwa.
 
We jamaa ni noumer!!!!
 
"Mungu sio Mwigulu Nchemba ........." mi hapo tu huko kwingine watajijua wenyewe mademu.
 
"Mungu sio Mwigulu Nchemba ........." mi hapo tu huko kwingine watajijua wenyewe mademu.
[emoji2] [emoji2] [emoji2] . Lakini nadhani umeelewa hoja yake
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] we kaka tuache
tukiwang'ang'ania mnapiga kelele,tukiwaacha kelele
 
Ora upo mkuu, kung'ang'ania inafaa ikiwa unaona kesho yako ipo kwa huyo mwanaume na atakupatia furaha na Amani ktk maisha yako ya baadae, na sio king'aacho ni dhahabu.
 
Ora upo mkuu, kung'ang'ania inafaa ikiwa unaona kesho yako ipo kwa huyo mwanaume na atakupatia furaha na Amani ktk maisha yako ya baadae, na sio king'aacho ni dhahabu.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] we kaka tuache
tukiwang'ang'ania mnapiga kelele,tukiwaacha kelele
Kisu kimegusa mfupa
 
Kuna aina mbili za usaliti,
Kuna ambao ni wasiri na ambao sio wasiri
Sasa kwa ambao sio wasiri ndio ambao wake zao wanaimba Mungu fanya miujiza,
Mwanume shupavu ni yule ambaye anafanya usaliti lakini akitambua mke wake ndio nambari one
aisee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…