Wanawake mabikra tukutane hapa

galatia

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2016
Posts
342
Reaction score
829
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza

Nawaalika mabikra wote tuliopo MMU tukutane hapa tupeane uzoefu, lengo kubadirishana mbinu zilizotusaidia kuutunza usichana wetu mpaka leo hii.

Binafsi nilifanikiwa kuutunza usichana wangu kwa kuzingatia maagizo ya wazazi wangu, pamoja na hilo pia niliweka nia kutokumkubalia mwanaume yoyote atakaye nitaka kimapenzi.

Changamoto nilizokutana nazo kwa uamuzi huo ni nyingi sana, wasichana wenzangu walinicheka na kuniambia nakosa raha duniani.

Wavulana walifika mahali wakawa wananiogopa sana kutokana na majibu yangu.
Nilitengwa ktk mambo kadhaa na waliyokuwa rafiki zangu. Nilionekana kama mwanamke asiye na hisia na mengine mengi tu lakini hayakuniyumbisha.

Nafurahia maamuzi yangu sijawahi kuyajutia kamwe. Na nitaendelea na msimamo wangu mpaka nitakapofunga ndoa.

Karibuni.
 
Hili neno limebadilishwa maana yake na BAKITA?
 
Hongera ni adim sana saiz kukuta wanawake kama wewe. Haya sasa kati ya 10 tyar una trophy 2 za bure za kuitwa mke mwema kazana mamaa.
 
Ukiwa na hofu na Mungu na kama ulipata malezi mema utajitunza tu kwa ajili ya kupata radhi za Mungu.

Usijitunze kwa ajili ya mume..wanaume hawana maana..ukiwa bikra atakuita gogo hujui kitu ukiwa mtundu atakuita malaya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…