Wanawake kuweni makini sana na wanaume

Wanawake kuweni makini sana na wanaume

Don 01

Member
Joined
Feb 23, 2017
Posts
27
Reaction score
24
Habari zenu wana janvi,

Imebidi uzi huu niwashirikishe maana ni kitu ambacho hata mimi kimeniuma sana baada ya kutokea. Sisi ni binadamu na huruma mwenyezi Mungu alituwekea katika nafsi zetu japo wapo binadamu wasiokuwa na huruma hata chembe.

Kuna jamaa mmoja alikuwa na mahusiano na binti fulani kwa mda wa mwaka mmoja hivi na binti alimtambulisha kijana na taratibu za ndoa zilianza. Kijana alikuwa siyo mkweli kwa binti, maana alimdanganya binti mambo mengi sana yaani asilimia 80 ilikuwa ni uongo.

Binti alikuja kugundua kuwa aliyoambiwa na huyo kijana ni uongo mtupu siku chache kabla ya ndoa. Binti alilia sana na akailaumu nafsi yake kwanini hakuwa mdadisi wa kina ili kujua kama aliyoambiwa ni kweli au laah. Binti aliamua kuachana na mchakato wa ndoa na waliochanga walirudishiwa chao, japo Mchungaji alimshauri binti asamehe mchakato uendelee lakini binti alikataa katakata.

Ndugu wanajanvi hususani wanawake mnapenda sana kuolewa maana nahisi mtu anapooa au kuolewa huongeza heshima fulani katika jamii.

Nawaombeni muwe mnachunguzana kwa kina, muulize kwao wapi, mkoa gani, wilaya gani, kijiji gani, nia na madhumuni ni kupajua kwao pamoja na kufanya uchunguzi kimyakimya bila hata yeye kujua.

Hiyo itakusaidia sana wewe kujuwa hali halisi ya mwenza wako pamoja na kujiridhisha aliyokwambia kuhusu yeye na familia yao ni kweli au sanaa tupu.

Hakuna majaribio ya kuoa au kuolewa, tusiziache mila zetu tukaiga zaidi ya wazungu, maana utasikia oooh unataka kuoa familia yangu au unataka kunioa mimi, binadamu wa dunia ya leo wametawaliwa na tamaa na ubinafsi, bila kumjua vyema unayemuoa au anayekuoa ni kupeleka aibu na fedheha kwenye familia yako kama ilivyotokea kwa huyu mwenzetu. Familia imealika ndugu, jamaa na marafiki mwisho wa siku sijuwi mnawaambiaje wageni waalikwa, ni aibu sana na inaumiza sana.

Tutafakari kwa kina sana na tuchunguzane kwa kina sana kabla ya kupelekana kwenye familia zetu.
 
Wanawake wengi wanapenda kuambiwa maneno matamu. Bila hivyo humpati.

Nafikiri ndicho kinachowaponza wengi.
 
560b060c41a9a240a2d5320ca5200d0f.jpg


Nauza hivi vitabu
 
Habari zenu wana janvi., imebidi uzi huu niwashirikishe maana ni kitu ambacho hata mim kimeniuma sana baada ya kutokea. Sis ni binadam na huruma mwenyezi Mungu alituwekea katika nafsi zetu japo wapo binadamu wasiokuwa na huruma hata Chembe.
Kuna jamaa mmoja alikuwa na mahusiano na binti flan kwa mda wa mwaka mmoja hiv, na binti alimtambulisha kijana na taratibu za ndoa zilianza.
Kijana alikuwa siyo mkweli kwa binti., maana alimdanganya binti mambo mengi saaan yaani asilimia 80 ilikuwa ni uongo.
Binti alikuja kugundua kuwa aliyoambiwa na huyo kijana ni uongo mtupu siku chache kabla ya ndoa. Binti alilia saana na akailaum nafsi yake kwa nin hakuwa mdadisi wa kina ili kujua kama aliyoambiwa ni kweli au laah., Binti aliamua kuachana na mchakato wa ndoa na waliochanga walirudishiwa Chao japo Mchungaji alimshauri binti asamehe mchakato uendelee lakin binti alikataa katakata.
Ndugu wana janvi hususani wanawake., mnapenda sana kuolewa maana nahisi mtu anapooa au kuolewa huongeza heshima flani katika jamii.
Nawaombeni muwe mnachunguzana kwa kina., muulize kwao wapi, mkoa gani, wilaya gani, kijiji gani., nia na madhumuni ni kupajuwa kwao pamoja na kufanya uchunguzi kimyakimya bila hata yeye kujua. Hiyo itakusaidia sana wew kujuwa hali halisi ya mwenza wako pamoja na kujiridhisha aliyokwambia kuhusu yeye na familia yao ni kweli au sanaa tupu.
Hakuna majaribio ya kuoa au kuolewa, tusiziache mila zetu tukaiga zaidi ya wazungu., maana utasikia oooh unataka kuoa familia yangu au unataka kunioa mim.,
Binadamu wa dunia ya leo wametawaliwa na tamaa na ubinafsi., bila kumjua vyema unayemuoa au anayekuoa ni kupeleka aibu na fedheha kwenye familia yako kama ilivyotokea kwa huyu mwenzetu.
Familia imealika ndugu, jamaa na marafiki mwisho wa siku sijuwi mnawaambiaje wageni waalikwa., ni aibu saaana na inaumiza saaana.
Tutafakari kwa kina sana na tuchunguzane kwa kina saaana kabla ya kupelekana kwenye familia zetu.
Zamani wazazi walikuwa ndiyo wanachagulia vijana wao wachumba na hasa hasa walikuwa wanahitaji vijana wao waoe au kuolewa sehemu wanazotoka.
Hii ilionekana kama ni ubaguzi lakini ukiangalia kwa undani wazazi walikuwa wanataka kujiliridhisha kwamba mtoto wao anoa au anaolewa katika mikono salama.
Maana walikuwa wanaangalia koo anazotoka bint au mvulana je hazina tatizo lolote? Kama; je koo husika haina asili ya magonjwa ya kuambukiza, hawana asili ya wizi, hawana asili ya uongo?
Na mambo mengi yanayofanana na hayo.
Lakini leo vijana wanamuangalia mtu kwa utashati wake pesa zake uwezo wake wa kujieleza vitu ambavyo kimsingi siyo sifa ya ndoa pole yake kijana.
 
Mademu siku zote watabaki kuangalia vifua ,pesa ,mavaz , simu , N.k. yaan hawa wao wanaangalia ile Outermost Shell ya Atom .wao wanawaza ivi ,Je huyu anaweza kunipeleka club ?? Ataweza ninunulia pombe ?? Navipi kuhusu kunivalisha ??? Je nikitoka naye marafiki zangu watasemaje ??? Je anakifua cha mapenzi ???
Huyu ukiwa naye haangaiki kukujua kindakindaki ,nakukupa uchi ni sekunde tu ...nahawa niwapotezaji ,wanakujaga kushituka Wakati ambao MUDA umewaacha ,alafu ndo anaanza kutafuta mume mwema

Mwanamke yeye atataka aelewe An Atom ni nini???? Je Atom ndio smallest particle at all or not ??. Je huyu mwanamme anaweza kunipa ulinzi ??? Nikweli hana pesa ila Je Anaakili ya utafutaji ?? Nikweli anaamini ktk mafanikio ?? Je nimwanamme ambaye anaweza kuniogoza na kunishauri ktk changamoto zangu n.k n.k n.k. huyu hawezi kukupa Uchi km Hajakujua kindaki ndaki

Kurahisisha mambo niseme ,Mademu wataendelea kutumiwa kwasababu wanaendeshwa na Hormone And Wanawake hawawezi kupoteza sababu wanatumia akili.
 
Sawa Mkuu. Ila na nyie wanaume mtu una nia naye ya dhati unamdanganya wa nini huoni mwisho wa siku mbali na aibu ambayo atakumbana nayo mwanamke na wewe pia utakuwa umejiaribia mwenyewe.

Hapa kila upande umekuelewa yaani sisi wadanganywaji na hao wadanganyaji. Abadan uongo si mzuri.
 
Kuwa specific huyo binti alidanganywa nini??
Kuhusu mali??
Au family background?
Au jamaa alikua na mke mwingine?
 
Habari zenu wana janvi., imebidi uzi huu niwashirikishe maana ni kitu ambacho hata mim kimeniuma sana baada ya kutokea. Sis ni binadam na huruma mwenyezi Mungu alituwekea katika nafsi zetu japo wapo binadamu wasiokuwa na huruma hata Chembe.
Kuna jamaa mmoja alikuwa na mahusiano na binti flan kwa mda wa mwaka mmoja hiv, na binti alimtambulisha kijana na taratibu za ndoa zilianza.
Kijana alikuwa siyo mkweli kwa binti., maana alimdanganya binti mambo mengi saaan yaani asilimia 80 ilikuwa ni uongo.
Binti alikuja kugundua kuwa aliyoambiwa na huyo kijana ni uongo mtupu siku chache kabla ya ndoa. Binti alilia saana na akailaum nafsi yake kwa nin hakuwa mdadisi wa kina ili kujua kama aliyoambiwa ni kweli au laah., Binti aliamua kuachana na mchakato wa ndoa na waliochanga walirudishiwa Chao japo Mchungaji alimshauri binti asamehe mchakato uendelee lakin binti alikataa katakata.
Ndugu wana janvi hususani wanawake., mnapenda sana kuolewa maana nahisi mtu anapooa au kuolewa huongeza heshima flani katika jamii.
Nawaombeni muwe mnachunguzana kwa kina., muulize kwao wapi, mkoa gani, wilaya gani, kijiji gani., nia na madhumuni ni kupajuwa kwao pamoja na kufanya uchunguzi kimyakimya bila hata yeye kujua. Hiyo itakusaidia sana wew kujuwa hali halisi ya mwenza wako pamoja na kujiridhisha aliyokwambia kuhusu yeye na familia yao ni kweli au sanaa tupu.
Hakuna majaribio ya kuoa au kuolewa, tusiziache mila zetu tukaiga zaidi ya wazungu., maana utasikia oooh unataka kuoa familia yangu au unataka kunioa mim.,
Binadamu wa dunia ya leo wametawaliwa na tamaa na ubinafsi., bila kumjua vyema unayemuoa au anayekuoa ni kupeleka aibu na fedheha kwenye familia yako kama ilivyotokea kwa huyu mwenzetu.
Familia imealika ndugu, jamaa na marafiki mwisho wa siku sijuwi mnawaambiaje wageni waalikwa., ni aibu saaana na inaumiza saaana.
Tutafakari kwa kina sana na tuchunguzane kwa kina saaana kabla ya kupelekana kwenye familia zetu.
Eleza vizuri kitu ambacho binti alidanganywa
 
Back
Top Bottom