Wanawake acheni imani potofu dhidi yetu

Wanawake acheni imani potofu dhidi yetu

Pull up

Member
Joined
May 19, 2015
Posts
22
Reaction score
6
Habari wana JF,

Nimekuwa nikifuatilia mijadala mbalimbali na mchango wa wadau wa mtandao huu na kuona busara zikitoka kwenu kusaidia wale wanaohtaji ushauri. Mimi nina langu linanikera, hili linafanywa na akina dada wengi mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 27 ni askari wa JWTZ, nimejiunga mwaka 2008.

Katika kusaka maisha nilibahatika kukutana na binti mmoja ambae tulianza mahusiano takribani miaka 3 iliyopita, kwa bahati nzuri au mbaya nikawa nimempa ujauzito, kwa kuwa nilikuwa nampenda nikaamua kwenda kwao na kutoa posa ili nipangiwe mahari. Nashukuru Mungu mambo yakaenda sawia.

Kwa kipindi hiko yy alikuwa anaishi kwao (nje ya mkoa niliopo mm), basi baada ya kutoa posa nikapangiwa mahari nikaambiwa nikijikamilisha niipeleke ila wakasema nimchukue nikakae nae kwani mimba natakiwa niilee mwenyewe basi nikamchukua binti wa watu mpka kwang tukaanza maisha. Muda wa kujifungua ulipokarbia nikampeleka kwao na akajifungua salama, nikamrudisha ili tulee mwana.. Tukakaa pamoja mpka mtoto wetu akafikisha miez tisa.

TATIZO LIKAJA HAPA:
Tangu kipindi nianze kuishi na huyu mwenzangu ugomvi wangu mimi na yeye ni kutokuniamini mm kwa kigezo "nyinyi wanajeshi nasikia hamjatulia" kauli hyo ikiambatana na wivu uliopitiliza, kiasi kwamba akikupgia simu hata uwe kazini ukawa unatumika basi ujiandae kujibu ulikuwa unaongea na nani na ukirudi nyumbani unakuta kanuna hivyo umbembeleze ili muende sawa na kiukweli ndugu zangu mimi sio mchepukaji hata kidogo pia tangu niwe nae hajawahi kunifumania wala kuona napigiwa simu tatanishi, wala sieleweki mipasiwedi kwenye simu yangu.

Hapa nilipo nahisi tunakoelekea mimi ntashindwa kuendelea nae ila kinachoniuma ni mtoto wang na ukizingatia mm ctaki kuzaa na wanawake zaidi ya huyu. Kwasasa yupo kwao kaenda msibani na hatuna maelewano kisa profile picture ya wasap nimemuweka dadangu (mtoto wa mama yake na kakaangu tuliye kutana kwa baba) yuko form six Tanga, yeye anadai hamjui hvyo ni kimada wangu. Nimejarbu kumtumia nambari ampgie hataki, basi nikamwambia asome status niliandika "I miss u my lovely sister" anadai haijalishi.

Jamani nawaombeni kina dada mjue kuwa si kila mtu ni malaya na hakuna kipindi nilichoona jeshini wanafundisha kutongoza hii ni mtu mwenyewe. Pia wadau mnisaidie mawazo nifanye nini na uhusiano huu maana natumika sana, sasa naona mbeleko inachanika niliyembeba anarukaruka mgongoni kutwa kubembeleza tu.
 
Pole mkuu ila nachoona hapo huyo anahitaji kugegedwa kwani tangia ajifungue umepiga mzigo?..km umepiga basi kuwa mpole endelea kusema ukweli juu ya maswali yk kwani huo ni udhaifu wake
 
Pole mkuu ila nachoona hapo huyo anahitaji kugegedwa kwani tangia ajifungue umepiga mzigo?..km umepiga basi kuwa mpole endelea kusema ukweli juu ya maswali yk kwani huo ni udhaifu wake

Kama ni unyumba napewa Bro.. Ila nadhan hujakutana na masaibu kama yang, siku yakikukuta usisahau kunipa hai.. Asante kwa ushauri wako
 
mkuu bora huyo wako wangu anadaigi tuachane kabisa
ila badae nilikuja kugundua ni wivu wake tu.
Kwa ushauri wng we mfanyie vi2 ambavyo yemwenyewe akiviona vina mpendeza in short we msikìlize tuu

asante
 
ila na ninyi ni wazinzi sana..kwenye mia ni mmoja tu...nawaonaga hata wenzako wa Mtabila,,,wanavyofakamia mademu vimeo wa kasulu......
 
Nasikia ninyi wajeda ni watu wa 3 W[SUB]s[/SUB]--War, Wine, Women
Labda niulize.....ni kwanini huwa ,mnahusishwa sana na uchepukaji?
 
Nasikia ninyi wajeda ni watu wa 3 W[SUB]s[/SUB]--War, Wine, Women
Labda niulize.....ni kwanini huwa ,mnahusishwa sana na uchepukaji?

Ni kweli hyo police wao wana Nyakubi..yaani Nyama,,,k,,,na bia
 
kaka, wivu katika mapenzi ni jambo la kawaida ila ukizidi unaboa mwambie mapenzi ni ya watu wawili tu ya nje ayaache kama yalivyo labda ayathibitishe kwa macho yake mwenyewe ndo ayaamini.......................!!
 
Wivu muhimu
Ndio uzoee akinunua muache atacheka mwenyewe
 
pole sana. hawa wanawake mara nyingine inabidi ushirikishe ndugu zake ili wamuonye hasa pale hali inapokuwa ngumu. hii inakuweka upande salama (safe side) hata ukimpiga chini nduguze wajue kuwa binti yao ndio chanzo cha matatizo. Nimeshudia wanawake wakibadilika kitabia hasa baada ya kukalishwa kikao na ndugu zake na kuonywa kwa tabia zao mbaya. Unaweza kujaribu hii, pengine itakusaidia

hata hivyo ongeza muda wa gwaride kunako six by six maana hofu yake ni hio kwamba unacheza gwaride nje. Pigisha kwata haswa mpaka ajione kwamba kwa gwaride hilo lazima atakuwa yupo peeke yake. lakini kama unarudi kazin unafika unalala unamuangalia tu, ujue unajiongezea matatizo wewe mwenyewe
 
Pole sana mkuu,huyo mwanamke si muelewa na amejaa wivu wa kijinga ndio maana hata ukimuelewesha haelewi sasahv akinuna mwache then mwambie afanye anachotaka ikiwa unambembeleza ila haelekei.
 
hayo mambo yakuwekana kwenye profile mara huyu jiran yangu, mara shangazi yake bibi yake yule dada angu wa salon tulishare mama mkubwa, siyapendi aisee. umemaliza picha za mkeo zote na za mtoto, zako, ndugu zako, na za quote mbali mbali hadi uweke picha ambazo mwenzio hawafahamu, Wallah!!! ningekuwa huyo mkeo na ujeda wako ningekung'oa meno na kijiko.
 
Jaribu kutafuta rafiki yake wa karibu au dada yake kama anaye umweleze tatizo,pengine wanaweza kumshauri na ikasaidia,maana kwa wewe imesha shindikana kwani hakuamini kutokana na wivu wake uliopitiliza.
Asikwambie mtu,wivu wa mwanamke ukipitiliza ,hakika amani hutoweka ndani .nasema hivyo kwani nina experience na hilo tatizo.
 
mkuu bora huyo wako wangu anadaigi tuachane kabisa
ila badae nilikuja kugundua ni wivu wake tu.
Kwa ushauri wng we mfanyie vi2 ambavyo yemwenyewe akiviona vina mpendeza in short we msikìlize tuu

asante

Nimejitahd kumfanyia kila anachopenda na kuprove kila anachokisuspect ili tuende sawa lakin ndo anazid
 
hayo mambo yakuwekana kwenye profile mara huyu jiran yangu, mara shangazi yake bibi yake yule dada angu wa salon tulishare mama mkubwa, siyapendi aisee. umemaliza picha za mkeo zote na za mtoto, zako, ndugu zako, na za quote mbali mbali hadi uweke picha ambazo mwenzio hawafahamu, Wallah!!! ningekuwa huyo mkeo na ujeda wako ningekung'oa meno na kijiko.

Asante dada kwa maneno yako
 
Jaribu kutafuta rafiki yake wa karibu au dada yake kama anaye umweleze tatizo,pengine wanaweza kumshauri na ikasaidia,maana kwa wewe imesha shindikana kwani hakuamini kutokana na wivu wake uliopitiliza.
Asikwambie mtu,wivu wa mwanamke ukipitiliza ,hakika amani hutoweka ndani .nasema hivyo kwani nina experience na hilo tatizo.

Nimefanya yote hayo... Samaki huyu hakunjiki Bro
 
Back
Top Bottom