Utangulizi,
Nchi hii ina wenyewe, watu wanatumia koti la kodi ili kuongeza mapato katika biashara zao. Mfano, Waziri Mkuu ana shares katika kampuni ya vodacom, wala sio siri, na mstaafu ana share kwenye Halotel, pia sio siri. Na wengine wengi waliopo serikalini na bungeni wana shares nyingi tu kwenye mitandao ya simu. Sio siri pia.
Wananchi hebu nendeni kwenye masoko ya hisa mfuatilie wamiliki wa hisa katika makampuni ya simu muone wanene wanavomiliki hisa huko, ndio mtaelewa kwamba hii nchi ina wenyewe wanaolinda matumbo yao.
Na uzuri kwenye maswala ya umiliki wa hisa kwenye Dar Es Salaam Stock Exchange pamoja na Brella sio siri, mambo yapo wazi kabisa na wala sio yakificho.
Tunajazana ujinga na upumbavu kukaa kuaminishana serikali ipo kwaajili ya wanyonge. Hakuna kitu kama hicho.
Swala La Mahakama,
Mahakama haiwezi kuingilia udhaifu wa sheria za nchi hii, kwasababu sheria zote zinazo husiana na Wizara zinawapa mamlaka Mawaziri kutunga "KANUNI (Sheria Ndogo)/MABADILIKO YA TOZO/MIENENDO YA WIZARA".
Pili, kabla ya budget ya Wizara Ya Fedha kupitishwa bungeni, lazima ipitie kwenye baraza la mawaziri ili waipitishe. Kama kuna mabadiliko au kuongezwa kwa kodi/tozo n.k basi lazima budget hio ipitishwe na baraza la mawaziri. So that is to say, huu upumbavu ulipitishwa na Baraza La Mawaziri hata kabla haujapelekwa bungeni ili wabunge waipitishe hii budget ya Mwigulu Mchemba.
Mahakama kazi yake kubwa ni "KUTAFSIRI SHERIA", sio kubadili sheria. Mtu akifanya kosa, na anapopelekwa kizimbani mahakama inakwenda kutafsiri sheria kutokana na ushahidi utakaopelekwa (Kwamba mshtakiwa kutokana na tafsiri ya sheria na ushahidi, ni kweli amevunja sheria au laaa).
Final,
Play By The Rules; The weak dont get to choose how they die, only the rich and powerful.
Endeleeni kuhuzunika/kulalamika/kupiga domo/kununa/wekeni gubu tuuuuu mpaka mpate majipu ya roho, ila hakuna kitu kitabadilika nchi hii. Mpaka wananchi akili ziwakae sawa na wajue umuhimu wa "KATIBA MPYA".