Wanaopiga risasi wananchi hifadhini waonywa

Wanaopiga risasi wananchi hifadhini waonywa

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,881
Reaction score
6,374
Serikali imepiga marufuku na kuwaonya watumishi wa Idara ya Wanyamapori wanaopiga risasi watu wanaowakamata wakifanya shughuli mbalimbali ikiwemo ujangili katika higadhi za taifa, kuacha na badala yake watumie sheria kukabiliana nao

Kadhalika, watumishi wa idara mbalimbali zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii, wametakiwa kubadilika na kuachana na vitendo vya rushwa.

Agizo hilo lilitolewa mwishoni mwa wiki iliyopita na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja, alipokutana na watumishi wa idara mbalimbali zilizo chini ya wizara hiyo katika Chuo cha Wanyamapori cha Pasiansi, jijini Mwanza.

Akizungumza na watumishi hao, Masanja alisema kuna malalamiko mengi katika baadhi ya hifadhi kwa maaskari kuwapiga risasi na kuwaua watu wanaowakuta ndani ya hifadhi na kuonya kuanzia sasa waache.

"Nimepata malalamiko mengi ya askari wetu wa wanyamapori kuwapiga risasi na kuwafanyia vitendo vibaya watu wanaowakuta ndani ya hifadhi, sasa vitendo hivi mviache,” alisema.

Chanzo: IPP Media
 
Kweli kabisa waache ama wapunguze hii tabia
 
Maelefu ya raia wamepigwa risasi kwenye hifadhi ya Rubondo National Park katika utawala wote wa Serikali ya awamu ya tano, eti leo ndipo wanapata malalamiko! Ni maigizo tu!
 
Kumbe ni Tundu Lisu a.k.a "ni yeye" alikua mkweli wakati wa kampeni alilisemea sana hili.
 
Serikali imepiga marufuku na kuwaonya watumishi wa Idara ya Wanyamapori wanaopiga risasi watu wanaowakamata wakifanya shughuli mbalimbali ikiwemo ujangili katika higadhi za taifa, kuacha na badala yake watumie sheria kukabiliana nao

Kadhalika, watumishi wa idara mbalimbali zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii, wametakiwa kubadilika na kuachana na vitendo vya rushwa.

Agizo hilo lilitolewa mwishoni mwa wiki iliyopita na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja, alipokutana na watumishi wa idara mbalimbali zilizo chini ya wizara hiyo katika Chuo cha Wanyamapori cha Pasiansi, jijini Mwanza.

Akizungumza na watumishi hao, Masanja alisema kuna malalamiko mengi katika baadhi ya hifadhi kwa maaskari kuwapiga risasi na kuwaua watu wanaowakuta ndani ya hifadhi na kuonya kuanzia sasa waache.

"Nimepata malalamiko mengi ya askari wetu wa wanyamapori kuwapiga risasi na kuwafanyia vitendo vibaya watu wanaowakuta ndani ya hifadhi, sasa vitendo hivi mviache,” alisema.

Chanzo: IPP Media
Kwa kuwa serikali imejua kwa tamko hili la kuwakataza Askari wa TANAPA kuua watu katika mapori, Ni wakati muafaka wa serikali kuunda time kuchungiza madhila yaliyosababishwa na tabia hii ya kupiga watu risasi hovyo. Tungependa kujua ni Watanzania wangapi wameuawa, wangapi wamelemazwa na familia ngapi zimeathirika na ukatili huu. Mwisho, serikali iombe radhi na kuwalipa fidia wale wote walioathiriwa na ukatili huu wa vyombo vyake.
 
Back
Top Bottom