Wanaomsakama Rais waache mara moja

Wanaomsakama Rais waache mara moja

AUGUSTINO CHIWINGA

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2017
Posts
222
Reaction score
695
Limeibuka kundi la wakosoaji na wasakamaji wasio na nyuzi za mashiko za hoja wanaobeza na kubagaza kila tendo jema ambalo Mh.Rais analivujia jasho kwa ajili ya Watanzania.

Wanafanya upotoshaji wa dhahiri kubwa ikiwa ni mbio za Urais 2025, kutaka kuonesha kama Rais anakosea na amesababisha ugumu wa maisha ilihali sio kweli.

Hakuna asiyejua namna sekta za uchumi na uzalishaji mali duniani kote zilivyoathirika na maradho ya UVIKO -19 kabla hakujapoa likaibuka janga lingine la vita vya wakubwa wa Dunia wa Urusi na Ukraine ambayo imetikisa ustawi wa uchumi Duniani kote.

Hivyo katikati ya majanga hayo makubwa unahitaji kuwa na akili zenye ubunifu na kunyambulika kama za Mh.Samia Suluhu Hassan.

Nilichogundua yeye Mh.Rais akili yake inafanya kazi mara 30 zaidi ya wakosoaji waliojazana huko kwenye mitandao.
Watakuja kumuelewa hapo baadae na watatamani kumuomba radhi lakini watakua tayari wameshachelewa.

Wote mnaomsakama Mh.Rais mtendeeni haki kwa kuacha mara moja tabia hiyo mbaya Hakuna kiongozi wa nchi anayefurahia wananchi wake wapate changamoto .Hatua zote anazochukua ni kwa ajili ya kupambana na na kurudisha (Restoration) ya vitu kwenye hali ya kawaida.
Tumtie moyo wa ushujaa Mama yetu.
 
Wauunga Mkono na Wakosoaji lazima wawepo,wakikosekana siyo afya bora bali bora afya.
 
Bora raisi samia mara 200 kuliko aliyeitwa raisi fedhuli wa watanzania MAGUFULI. Yule alikuwa mtu mbaya kwa nchi yangu TZ
asante mungu kwa ukuu wako
 
Bora raisi samia mara 200 kuliko aliyeitwa raisi fedhuli wa watanzania MAGUFULI. Yule alikuwa mtu mbaya kwa nchi yangu TZ
asante mungu kwa ukuu wako
Naona mkuu wa mashetani unachuki kuu
 
Limeibuka kundi la wakosoaji na wasakamaji wasio na nyuzi za mashiko za hoja wanaobeza na kubagaza kila tendo jema ambalo Mh.Rais analivujia jasho kwa ajili ya Watanzania.

Wanafanya upotoshaji wa dhahiri kubwa ikiwa ni mbio za Urais 2025, kutaka kuonesha kama Rais anakosea na amesababisha ugumu wa maisha ilihali sio kweli.

Hakuna asiyejua namna sekta za uchumi na uzalishaji mali duniani kote zilivyoathirika na maradho ya UVIKO -19 kabla hakujapoa likaibuka janga lingine la vita vya wakubwa wa Dunia wa Urusi na Ukraine ambayo imetikisa ustawi wa uchumi Duniani kote.

Hivyo katikati ya majanga hayo makubwa unahitaji kuwa na akili zenye ubunifu na kunyambulika kama za Mh.Samia Suluhu Hassan.

Nilichogundua yeye Mh.Rais akili yake inafanya kazi mara 30 zaidi ya wakosoaji waliojazana huko kwenye mitandao.
Watakuja kumuelewa hapo baadae na watatamani kumuomba radhi lakini watakua tayari wameshachelewa.

Wote mnaomsakama Mh.Rais mtendeeni haki kwa kuacha mara moja tabia hiyo mbaya Hakuna kiongozi wa nchi anayefurahia wananchi wake wapate changamoto .Hatua zote anazochukua ni kwa ajili ya kupambana na na kurudisha (Restoration) ya vitu kwenye hali ya kawaida.
Tumtie moyo wa ushujaa Mama yetu.
Mwambie ili asikosolewe auachie Urais.
 
Huna mamlaka ya kuwazuia watu kusema. Kiongozi mzuri ni yule anayekubali pia mawazo mbadala (kukosolewa na wapinzani wake)
 
Back
Top Bottom