lonyorengai
Member
- May 12, 2008
- 71
- 35
Nimekuwa nikisikia baadhi ya watu wakisema kuwa hawatakwenda kupiga kura. Wanatoa sababu nyingi ikiwemo dhana kwamba kumpigia mtu kura ni kumpatia ulaji. Wengine wamejawa na hofu ya fujo kutokea siku ya uchaguzi hivyo kuchagua kubaki nyumbani. Kuna maneno yanaenezwa pia kuwa watu wanunue mahitaji ya kutosha ya chakula kwa wiki mbili kwa kuwa vurugu zitatawala baada ya uchaguzi.
Nitoe ushauri kwa watz wenzangu mjitokeze kupiga kura kwa wingi ili kuleta mabadiliko ktk taifa letu. Tuna wajibu wa kidemokrasia wa kuchagua viongozi kwa kupiga kura. Usikubali kutiwa hofu na wasioitakia mema nchi hii kwa vitisho vya vurugu au fujo siku hiyo. Hata hivyo, huu ni ushindani na hakuna kurudi nyuma hata tupige kura.
Wajibika kwa ajili ya taifa letu. Usiache viongozi dhalimu waendelee kuwepo baada ya uchaguzi huu. Chagua kwa usahihi uikomboe nchi yako kutoka kwa walanguzi.
Na Mungu awabariki nyote mtakaopiga kura.
Piga kura, chagua kiongozi bora.
Nitoe ushauri kwa watz wenzangu mjitokeze kupiga kura kwa wingi ili kuleta mabadiliko ktk taifa letu. Tuna wajibu wa kidemokrasia wa kuchagua viongozi kwa kupiga kura. Usikubali kutiwa hofu na wasioitakia mema nchi hii kwa vitisho vya vurugu au fujo siku hiyo. Hata hivyo, huu ni ushindani na hakuna kurudi nyuma hata tupige kura.
Wajibika kwa ajili ya taifa letu. Usiache viongozi dhalimu waendelee kuwepo baada ya uchaguzi huu. Chagua kwa usahihi uikomboe nchi yako kutoka kwa walanguzi.
Na Mungu awabariki nyote mtakaopiga kura.
Piga kura, chagua kiongozi bora.