Shirika la umeme Tanzania, Tanesco limekubaliwa ombi lake la kupandisha bei ya umeme kwa 40% kuanzia kesho. Hili ni pigo kubwa kwa wananchi wa kada zote, ingawa wenyewe wametupiga siasa eti ongezeko halitawagusa walalahoi. Ukweli ni kwamba ongezeko la bei ya umeme huchochea pia ongezeko la gharama za huduma mbali mbali ikiwemo afya, Elimu, mawasiliano, nk. kwa kuwa nyingi ya huduma hizo hutegemea nishati ya umeme. Pia huongeza hata bei ya mkaa maana ndo imekua kimbilio kwa kutoshikikika kwa bei ya umeme.
Wakati umefika kwa watanzania kuvaa ujasiri na kupambana na hawa watawala wetu ambao hawana huruma na Wananchi. Tuungane katika hili bila kujali itikadi. Kuna tetesi kwamba deni la dowans limeshalipwa kinyemela ndo maana wanataka kurudisha gharama kupitia kwa wananchi wanyonge. Tulipiga kelele kuhusu kuilipa Dowans, hivi sasa wako kimyaaaaa! Napendekeza maandamano makubwa ya kitaifa kupinga ongezeko hili. Katika hili naomba watanzania tulio wengi tuungane maana sote ni wahanga. Naomba kutoa hoja.