Wanahitajika vijana wawili haraka!

Wanahitajika vijana wawili haraka!

Joined
Jun 28, 2017
Posts
72
Reaction score
124
Habari!
Wanahitajika vijana wawili kwa ajili ya kufanya kazi ya masoko ya muda mfupi wa siku saba na malipo ni kwa siku
Elimu
Kuanzia kidato cha nne na kuendelea. Kujua kuongea Kiingereza kwa Ufasaha ni lazima
Majukumu
Kuitangaza bidhaa kwa kugawa vipeperushi na kuwapa maelezo wateja juu ya huduma ya fiber internet.
Eneo
Ni katika majengo yaliyokuwa tayari yameunganishwa na mfumo wa fiber internet. Maeneo hayo ni Upanga, Masaki, City center na Kariakoo.
Utekelezwaji wake
Watapangiwa jengo kutokana na ratiba ya siku hiyo katika eneo husika
Muda
Inatakiwa kufika mapema eneo/jengo lililopangwa kwa siku hiyo kuanzia saa moja asbh hadi saa nne unapumzika. Unarudi saa sita mchana hadi saa tisa unapumzika. Unakuja kuendelea saa kumi na moja jioni hadi saa mbili. Target ni kuwapata wateja wanaofanya kazi na kuishi katika majengo
Malipo
Shilingi 12,000 kwa siku. Gharama za chakula na nauli ofisi haihusiki nazo
Kuanza lini?
Kuanzia Jumatano ya tarehe 24.01.2018
Mawasiliano
Ofisi: Mariam tower, ghorofa ya nne, makutano ya mitaa ya Shaurimoyo na Lindi, Ilala, Dar es Salaam
email: iconsultbuzness@gmail.com
Simu:0659211222/0777777766/0755411455
 
Hela ndogo sana mkuu chai na chakula ni juu yake kweli kwa 12 elfu mh hatar
 
Hahahaha 12000/day! Hamna nauli wala pesa ya chakula..!? You must be kidding. Fanya mwenyewe Mkuu!
 
Wakuu nadhani ninyi mnalipwa kubwa kuliko hii..Acheni kejeli basi wanaoona inawalipa watafananya.
Hakuna itakaemlipa bosi! Hicho kiwango ni kidogo mno. Hapo hamna tofauti na Biashara ya utumwa. There is more to life than surviving. 12k is peanut kwa kazi inayoku-waste siku nzima. Mkuu! Wapeni usafiri na chakula then hiyo 12K inaweza kuwa fair.
12K that's close to 1000 Tsh per hour.
 
Hakuna itakaemlipa bosi! Hicho kiwango ni kidogo mno. Hapo hamna tofauti na Biashara ya utumwa. There is more to life than surviving. 12k is peanut kwa kazi inayoku-waste siku nzima. Mkuu! Wapeni usafiri na chakula then hiyo 12K inaweza kuwa fair.
12K that's close to 1000 Tsh per hour.

Sisi huku vibarua tunalipwa elfu nane kwa siku na kila kitu juu yako chakula, nauli etc. Kama nyie mwaiona ndogo,sisi inatutosha
 
Sisi huku vibarua tunalipwa elfu nane kwa siku na kila kitu juu yako chakula, nauli etc. Kama nyie mwaiona ndogo,sisi inatutosha
Sawa nenda kafanya! Lakini ninauhakika nyie vibarua mnaolipwa 8k hua mnajisemesha pale mnapokua mmebaki peke yenu.
 
Wakuu hebu jaribuni kupitia vibarua wanalipwa sh ngapi na inakuwa full time mosi, pili hebu tupitie ratiba ya kazi yenyewe ni masaa kama nane tu tena kwa interval. Kugawa vipeperushi na kumuelezea mtu na tena kuna muda kama una issue zako unaenda kufanya
Anyway, jaribu kuchunguza mtaani watu wanalipwaje hawa wa mabarabarani wanakuwa na vipeperushi au mabango. Ikizidi sana huwa elfu 10 na kila kitu juu yako. Mara nyingi ipo kwenye elfu 6 hadi elfu 8
 
Niliwahi kufanya kibarua wakati wa ujenzi Udom aisee per day ilikiwa 3000

Chakula nauli chai maji utajua wewe

Nilifanya siku moja tu
Huyu anaeidharau 12,000/= na kusema ndogo, wapo wengine hata hiyo kubwa sana wanapata hapa hapa Dar tena kwa kazi ngumu ya kuvuja jasho na kushinda juani.
 
2 asubuh mpaka 2 usiku masaa 12 ukigawa 12000 ina maana kwa kila saa mtu anapata 1000 kweli watu wanashida lakini sio muwanyonye kiasi hiki, hapo nauli + msosi ni juu yake, mkuu jaribu kufanya wewe uone adha yake, mtu mpaka anamaliza kazi anakuwa hata hata buku mfukoni aliyoitengeneza.
 
Sisi huku vibarua tunalipwa elfu nane kwa siku na kila kitu juu yako chakula, nauli etc. Kama nyie mwaiona ndogo,sisi inatutosha
Kuna kibarua gani anafanya kazi hadi saa mbili usiku?
Kibarua inajulikana day yake ni 10-15k na ratiba yake ataingia saa 2 akhsubuhi hadi saa 4 ataenda kupata chai then atarudi saa 5 hadi saa 7 ataenda kupata lunch ambapo atarudi saa 9 hadi saa 11 atafunga ofisi.

Ukihesabu masaa yake ya kufanya kazi hapo ni 6 tu tofauti na nyie.

Acheni kunyanyasa watu kisa tu hawana kitu.....hiyo kitu ni mbaya sana na sijui kama hata hicho mnachoenda kukifanya kama kitaenda kufanikiwa.
 
Back
Top Bottom