Wanafunzi shule za msingi na sekondari wapangiwe shule za maeneo wanayoishi

MKWEAMINAZI

JF-Expert Member
May 28, 2023
930
1,299
Wadau nawasabahi,

Katika hali ya kutisha na kustaajabisha ni kawaida kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari za jiji la Dar kuwaona usiku wakiwa katika uniforms zao na mabegi yao migongoni wakiwa barabarani na kwenye vituo vya daladala na mabasi ya Mwendokasi wakigombania usafiri.

Nimekuwa najiuliza maswali yafuatayo:

1. Je, tatizo ni muda wa kutoka shuleni ndio mbovu?

2. Je, shule na makwao ni mbali?

3. Kwanini Serikali isiwapangie kwa lazima shule za karibu na maeneo wanayoishi ili wasihangaike na usafiri?

4. Je, ni wazazi ndio wanawahamishia wanafunzi shule za mbali na makazi yao au serikali?

5. Je, daladala na mabasi ya Mwendokasi hayataki kuwachukuwa wanafunzi vituoni ndio maana wanachelewa mpaka huo usiku?

Wakati umefika kwa Waziri mwenye dhamana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam wakishirikiana na Serikali kufanya maamuzi magumu katika hili tatizo, kwani madhara yake ni makubwa sana kwa wanafunzi wetu ukizingatia kuna wanafunzi wa shule za msingi wengi wao umri ni mdogo sana na ubakaji na ulawiti umeshamiri sana katika jiji hili.

20230704_074155.jpg
 
Wadau nawasabahi.Katika hali ya kutisha na kustabisha ni kawaida kwa WANAFUNZI wa Shule za Msingi na SEKONDARI za JIJI la DSM kuwaona USIKU WAKIWA ktk UNIFORMS zao na MABEGI yao MIGONGONI WAKIWA BARABARANI na Kwenye VITUO vya DALADALA na Mabus ya MWENDOKASI wakigombania USAFIRI .
Tatizo makao si ya kudumu. Unakuta nyumba ni za kupanga, leo unahamia huku, kesho kule.
 
Wazazi ndio sababu unakuta mtu anaishi Kimara mtoto anampeleka shule ya msingi bunge magogoni kule

Wa secondary kama kamakawida mtu Ankara goba mtoto anamuhamisha shule anampeleka tambaza what next?

Pia swala la muda kuna baadhi ya watoto wanabaki shule kwaajili ya masomo ya ziada
 
Kurubuniwa ni rahisi sana.Poor this generation.
 
Wazazi hawana makazi ya kudumu, kwa mwaka mtu kashahama mala 2. Sasa hapo ai utahamisha mtoto mpaka uchoke.
 
Katika kitu ubinafsi naweka pembeni ni shule za watoto wangu. Wakiwa wadogo shule lazima iwe karibu na nyumbani. Wakiwa wakubwa ni boarding
 
Back
Top Bottom