WanaCHADEMA: Charity begins at home!!

WanaCHADEMA: Charity begins at home!!

TEKNOLOJIA

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2014
Posts
4,305
Reaction score
2,563
CCM kama chama tawala kilichokaa madarakani kwa zaidi ya miaka 50 hakijafanya makubwa sana kwa nchi hii kiasi cha sisi Wananchi kujivunia.

Chini ya utawala CCM maendeleo katika nchi hii yamekuwa ni ya taratibu mno kama mwendo wa konokono.Inashangaza kuona baadhi ya nchi zilizotoka matatizoni kama Rwanda na Angola tayari zinafanya vizuri kiuchumi kuliko sisi tulioishi kwenye amani tangu uhuru.

Naam Watanzania tumekubali sasa kuwa CCM hawana jipya tena,Tumeweka akili na mawazo yetu kwa Chama mbadala ambacho ni CHADEMA.CHADEMA wanasema kwamba CCM ndiyo chanzo cha madhila yanayowakabili Wananchi,Kiasi fulani ni kweli na kwa kiasi fulani Wananchi pia tunastahili lawama.

Ninachowasihi Watanzania tuanze kuwapima CHADEMA kwenye mambo kama haya;Kujenga jengo la Makao makuu lenye hadhi inayoendana na jina la Chama pamoja na namna watakavyokuwa wanaendesha shughuli za Chama chao kisayansi na kitaalaamu zaidi ili kuonyesha matumaini kwa Watanzania ni aina gani ya mabadiliko watayaleta wakipewa madaraka ya kuongoza nchi.
 
hayo unayo yawaza waliwaza kina mrema.mapalala,lipumba,seif babu slaa kitambo sana na bado wamesanda utakuwa wewe mchovu mwenye id fake tena jf
 
Huu ni wakati wa kujenga chama sio kujenga Majengo ya chama. Hebu fuatilia historia ya TANU tangu mwaka 1954 ilikuwa haina jengo la maana zaidi ya kijengo kidogo pale Lumumba na kipo mpaka leo kama hakijabomolewa. Haya majengo mengine tumeyajenga sisi wananchi baada ya UHURU kwa kulazimishwa kuchanga na kukatwa fedha zetu kwenye mazao tuliokuwa tunauza. UHURU kwanza kutokana na kujenga chama mjengo baadae kwani usipokuwa na jengo lako hakukuzuui kujenga chama kama wewe ulie kwenye nyumba ya kupanga lakini umefanya maendeleo kibaao.
 
Yeriko Amekuwa busy kutumia multiple id kuleta na kuchangia mada,jumamosi aliumbuka baada ya kusahau kuhama id, akajikuta analeta thread,akamsifu mtoa mada, kisha anajiomba contact hapo nikathibitisha madhara ya bange na gongo kwa bavicha wengi
 
Kwa hiyo unaomba huruma ya tz zuzu we umeona nchi hii ni ya kujaribiwa? Zuzu mkubwa mwenye sera ndio tunaemchaguwa sisi wa tz sio mandamano na vurugu zuzu kubwa jinga!
 
hela za sabodo zilizotolewa kujenga makao makuu ya chama, mbowe na slaa wameshazila
 
hayo ni maobi yako ndungu sio ya watanzania......jiongoleee binafsi usiongelee watanzania....
 
Yeriko Amekuwa busy kutumia multiple id kuleta na kuchangia mada,jumamosi aliumbuka baada ya kusahau kuhama id, akajikuta analeta thread,akamsifu mtoa mada, kisha anajiomba contact hapo nikathibitisha madhara ya bange na gongo kwa bavicha wengi

Kale kajamaa sijui kama matatizo gani aisee anatafuta umaarufu kwa nguvu...

chadema inauliwa na watu aina ya Yericko Nyerere
 
Last edited by a moderator:
Huu ni wakati wa kujenga chama sio kujenga Majengo ya chama. Hebu fuatilia historia ya TANU tangu mwaka 1954 ilikuwa haina jengo la maana zaidi ya kijengo kidogo pale Lumumba na kipo mpaka leo kama hakijabomolewa. Haya majengo mengine tumeyajenga sisi wananchi baada ya UHURU kwa kulazimishwa kuchanga na kukatwa fedha zetu kwenye mazao tuliokuwa tunauza. UHURU kwanza kutokana na kujenga chama mjengo baadae kwani usipokuwa na jengo lako hakukuzuui kujenga chama kama wewe ulie kwenye nyumba ya kupanga lakini umefanya maendeleo kibaao.

Ni aibu kwa vijana wa kizazi hiki kipya kutumia mambo au changamoto zilizopita kujibia hoja zinazohusu changamoto za karne hii.Ukweli ni kwamba Chadema tunahitaji ofisi za Makao makuu zenye hadhi inayoendana na umaarufu wa Chama chetu.Ebu tuwe wakweli jamani lile jengo ni aibu kubwa kumilikiwa na Chama kinachotaka kuchukua madaraka ya nchi na wala tusikimbilie kulinganisha historia ya TANU kwa sote tunajua TANU ya wakati ule na CHADEMA havifanani.
 
Kale kajamaa sijui kama matatizo gani aisee anatafuta umaarufu kwa nguvu...

chadema inauliwa na watu aina ya Yericko Nyerere
Mkuu wangu unanipasua mbavu huyu mpiga ripu ndiyo anailinda Chadema.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu wangu unanipasua mbavu huyu mpiga ripu ndiyo anailinda Chadema.


Ha ha ha

Kiuno kimebunuuuka utafikiri sio mlume...


Leo anatafutia umaarufu kwa kina Lowassa mjinga sana yule
 
SABODO kajitoa kuwajengea jengo, pesa ya ruzuku inashia DUBAI , lini watajenga jengo la makao makuu. Na je kujenga jengo la makao makuu ya CHAMA ni kipimo kwamba mkulima wa kata yangu ya Nyahongo kule Tarafani Nyancha atakuwa ana matumaini ya CHADEMA kumpelekea maendeleo?
 
Ni aibu kwa vijana wa kizazi hiki kipya kutumia mambo au changamoto zilizopita kujibia hoja zinazohusu changamoto za karne hii.Ukweli ni kwamba Chadema tunahitaji ofisi za Makao makuu zenye hadhi inayoendana na umaarufu wa Chama chetu.Ebu tuwe wakweli jamani lile jengo ni aibu kubwa kumilikiwa na Chama kinachotaka kuchukua madaraka ya nchi na wala tusikimbilie kulinganisha historia ya TANU kwa sote tunajua TANU ya wakati ule na CHADEMA havifanani.

Kitendo cha Kuruka na CHOPA tatu kwenye kampeni za kata moja huku document za chama zikiwa zinalala kwenye kiota cha ndege ni kipimo tosha kuwa CHADEMA ni SACCOSS na siyo chama. Wakati wa kampeni nikasikia HECHE anasema siku saba alizoruka angani na CHOPA amejionea umaskini mkubwa sana wa tanzania, nikajiuliza kelele ambazo viongozi wake wamekuwa wakipiga majukwaani kuwa nchi ni maskini wao waliona baada ya kupanda CHOPA au alitaka kuwatambishia wananchi kuwa na yeye siku hizi ni mtu wa CHOPA?
 
hayo unayo yawaza waliwaza kina mrema.mapalala,lipumba,seif babu slaa kitambo sana na bado wamesanda utakuwa wewe mchovu mwenye id fake tena jf

Mleta mada karibia naye ataitwa msaliti, anaanza kuchokonoa ujenzi wa Makao makuu?
 
Huu ni wakati wa kujenga chama sio kujenga Majengo ya chama. Hebu fuatilia historia ya TANU tangu mwaka 1954 ilikuwa haina jengo la maana zaidi ya kijengo kidogo pale Lumumba na kipo mpaka leo kama hakijabomolewa. Haya majengo mengine tumeyajenga sisi wananchi baada ya UHURU kwa kulazimishwa kuchanga na kukatwa fedha zetu kwenye mazao tuliokuwa tunauza. UHURU kwanza kutokana na kujenga chama mjengo baadae kwani usipokuwa na jengo lako hakukuzuui kujenga chama kama wewe ulie kwenye nyumba ya kupanga lakini umefanya maendeleo kibaao.

Hiki chama kinajengwa miaka nenda miaka rudi? kimekuwa kama wachezaji wa ARSENAL, kila msimu wanaitwa watoto.
 
Yeriko Amekuwa busy kutumia multiple id kuleta na kuchangia mada,jumamosi aliumbuka baada ya kusahau kuhama id, akajikuta analeta thread,akamsifu mtoa mada, kisha anajiomba contact hapo nikathibitisha madhara ya bange na gongo kwa bavicha wengi

Mzimu wa ZITTO unamtafuna.
 
Back
Top Bottom