Wasalaam wanaJf. Naomba msaada juu ya Mwanzo 6:1-4. Ukisoma hii andiko unakutana na wanadamu, wana wa Mungu na Wanafili. Biblia inasema wana wa Mungu waliwaoa binti za binadamu na wakazaa nao. Muunganiko huu ulizaa majitu makubwa sana tena hodari walioitwa Wanefili.Suali langu ni kuwa hawa wana wa Mungu ni nani hasa, ni malaika au?
Mungu alichukizwa na matendo ya binadamu na akaamua kugharikisha watu wote isipokuwa familia moja watu wanane. Cha ajabu haya majitu makubwa wanaonekana kuwepo hata baada ya gharika. Ushahidi upo Hesabu 13:31-33. Hawa wana wa Anaki waliponaje kwenye gharika?
Mungu alichukizwa na matendo ya binadamu na akaamua kugharikisha watu wote isipokuwa familia moja watu wanane. Cha ajabu haya majitu makubwa wanaonekana kuwepo hata baada ya gharika. Ushahidi upo Hesabu 13:31-33. Hawa wana wa Anaki waliponaje kwenye gharika?