Wana MMU: Nifanye nini kumsaidia huyu bibie? Analia, hataki kula

habari ya hapa

JF-Expert Member
Dec 20, 2012
12,791
8,748
Habari zenu mabibi na mabwana, ni imani yangu kuwa mu wazima kiroho na kimwili

Nimetembelewa na rafiki yangu yapata wiki moja na zaidi, akitokea Mereran Arusha, urafiki wetu umekuwa ni undugu sasa, tumejiwekea tabia ya kutembeleana kila mmoja anapopata wasaa.

Rafiki yangu yupo katika kipindi cha mpito kwenye mahusiano yake, tangu aje nimekuwa na kibarua kizito cha kumfariji ili awe katika mazingira mazuri, japo sijafanikiwa mpaka sasa, muda mwingi ni MTU mwenye mawazo, amekuwa ni mwenye machozi kila wakati hata chakula hali vizuri hadi mpigiane makelele.

Anamapenzi ya kweli na mtu wake na wapo kwenye mahusiano yapata miaka mitano sasa lakini huyo mwenzie tayari alikuwa na familia sasa huyo shemeji sijui kapata mwingine au ameamua tu kubaki njia kuu? Mimi na weye hatujui, basi kwa rafiki yangu ni tafarani, anahuzunika sana, kingine rafiki yangu alimuazima pesa huyo mpenzi wake 3.8 milion na hataki kuzirudisha kwa madai kuwa kile alichoplan kukifanya kilikwama, kwa kweli rafiki yangu anapata shida sana.

Huyu mtu analia muda mwingi, presha inapanda kila wakati, nimsaidieje maana nimefika mwisho wa akili zangu, nina mgonjwa KCMC natakiwa kusafiri kama siku kadhaa hivi, nitamuachaje na hali yake hii?
 
Pole sana kwa unachopitia.

Kwani kinachomuumiza ni pesa au kukosa penzi.

Kama ni pesa basi atumie taratibu za kushawishi akigonga mwamba atafute ushahidi wa kuweza kujitosheleza aende kwenye vyombo Dora
 
Pole sana kwa unachopitia.

Kwani kinachomuumiza ni pesa au kukosa penzi.

Kama ni pesa basi atumie taratibu za kushawishi akigonga mwamba atafute ushahidi wa kuweza kujitosheleza aende kwenye vyombo Dora
Nilichokiona kikubwa ni kumkosa huyo MTU,
 
Kuwa nae makini alafu kama yuko na mwanaume wa mtu mwingine hata wakwako hatashindwa kutoka nae,
Kama vip muunganishe na rafiki yako mwingine wakiume ajione na yeye anathaminiwa. Kuhusu pesa hamna namna labda kama waliandikishana
 
Huyo mpenzi wake ana familia ukimanisha ana mumewe na watoto wake? na yeye akaenda kujipachika hapo hapo eeh au sijaelewa vizuri?
 
Kuwa nae makini alafu kama yuko na mwanaume wa mtu mwingine hata wakwako hatashindwa kutoka nae,
Kama vip muunganishe na rafiki yako mwingine wakiume ajione na yeye anathaminiwa. Kuhusu pesa hamna namna labda kama waliandikishana
Walipeana kimahaba wale sidhan km waliandikishana pahala
 
Kuhusu pesa itabidi uungwana wa aliepewa pesa hizo kuzirejesha na na ikiwa hati ya mapokeo ya pesa (risiti au mikataba yoyote) atake msaada ofisi za mitaa au polisi! kama hana chochote jaribu hili hapa chini!
 
Habari zenu mabibi na mabwana, ni imani yangu kuwa mu wazima kiroho na kimwili

Nimetembelewa na rafiki yangu yapata wikimoja na zaidi, akitokea mereran arusha, urafiki wetu umekuwa ni undugu sasa, tumejiwekea tabia ya kutembeleana kila mmoja anapopata wasaa.

Rafiki yangu yupo ktk kipindi cha mpito kwenye mahusiano yake, tangu aje nimekuwa na kibarua kizito cha kumfariji ili awe ktk mazingira mazuri, japo sijafanikiwa mpaka sasa, muda mwingi ni MTU mwenye mawazo, amekuwa ni mwenye machozi kila wakati hata chakula hali vizuri hadi mpigiane makelele.

Anamapenzi ya kweli na MTU wake na wapo kwenye mahusiano yapata miaka mitano sasa lkn huyo mwenzie tayari alikuwa na familia sasa huyo Shemeji sijui kapata mwingine au ameamua tu kubaki njia kuu? Me na weye hatujui, basi kwa rafiki yangu ni tafarani, anahuzunika sana, kingine rafiki yangu alimuazima pesa huyo mpenzi wake 3.8milion na hataki kuzirudisha kwa madai kuwa kile alichoplan kukifanya kilikwama, kwa kweli rafiki yangu anapata shida sana.

Huyu MTU analia muda mwingi, presha inapanda kila wakati, nimsaidieje maana nimefika mwisho Wa akili zangu, Nina mgonjwa KCMC natakiwa kusafiri km siku kadhaa hivi, nitamuachaje na hali yake hii?

Binamu nitafute chemba tumsaidie huyu binamu yetu
 
Ndo hivyo mkuu ana familia yaani mke na watoto,
kwahiyo yeye hana Mume lakini yuko na mume wa mtu kwa mda wa miaka m5? mwambie sio rizki yake sio rahisi kukubali lakini mwambie mda unakwenda na asipoteze asipopendwa wala pasipokua na mafanikio,sababau unapolima unategemea mavuno yeye hapo anategemea nini wakati mtu ana mumewe? hata dini yake ingeruhusu awe mke wa pili lakini jee
anaweza kuhimili tafrani ya uke wenza?
 
Omba Mungu atakujibu! Ni vizuri kuwafikiria na wenzako wa kiroho zaidi kupata msaada wa maombi zaidi! Nitajitahidi kukuombea lkn pia kumbuka kuomba sana!!
Amen kiongozi barikiwa sana, naomba sana naamini Mungu afanya njia
 
Kuhusu pesa itabidi uungwana wa aliepewa pesa hizo kuzirejesha na na ikiwa hati ya mapokeo ya pesa (risiti au mikataba yoyote) atake msaada ofisi za mitaa au polisi! kama hana chochote jaribu hili hapa chini!
Mkuu hakuna risiti zozote zinoonesha MTU kuazimwa pesa, kwani walikopeshana kimapenzi, km ulivyosema mkopeshwaji awe muungwana tu arejeshe, umesema nijaribu nini
 
Kama hanabushahidi wa kupeana hela basi amtumie msg kama hii "Habari, milion 4 zangu utanipa lini?" akijibu hiyo msg unaweza kuitumia kama ushahidi polisi! mtumie msg itakayo mfanya ajibu msg yako positive! akijibu basi nenda polisi maramoja ushahidi unao!!
 
Mkuu hakuna risiti zozote zinoonesha MTU kuazimwa pesa, kwani walikopeshana kimapenzi, km ulivyosema mkopeshwaji awe muungwana tu arejeshe, umesema nijaribu nini
Nimeandika hivi "mwambie amtumie mdeni wake msg inayosema "Habari, million 4 zangu utanipa lini?" Yule jamaa akiijibubile msg positive ushahidi ameupata autunie polisi!"
 
Lol hapo anamiss pesa zake tu...amtishie kumwambia mkewe maybe itasaidia.

Zaidi ya hapo asahau tu kwani ana miaka 12 jamani?
 
"...Nina mgonjwa KCMC natakiwa kusafiri km siku kadhaa hivi, nitamuachaje na hali yake hii?.."
Pole kwa rafiki yako na kwako pia. Nimesoma kwa umakini na nimegundua kuwa kilio chake na msongo WA mawazo alionao utapita, maana umeweza kukaa naye kwa wiki mbili hapo.
Kwangu naona changamoto ni hiyo paragraph ya mwisho ambayo "nimequote" hapo juu.
Unahitaji mtu wa kuishi na rafiki yako utakapokuwa haipo ama?!
 
Back
Top Bottom