Wana CCM tusijenge chuki baina yetu na watanzania

Wana CCM tusijenge chuki baina yetu na watanzania

TumainiEl

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
7,267
Reaction score
14,275
Jamani kuna wana ccm wanaeneza chuki ambayo mm nasema tusipo simama kama chama nakuonyana kwenye milango ya vyumba vya ndani itatusumbua sana kama chama huko tuendako. Nilazima tujuwe rais anasehem yake wakati wasaidiz wanasehem yao.

Chuki huleta hasira, chuki huleta uchungu, chuki huleta vita. Wapo watu wachache sana wanaleta chuki na kumfanya Rais aonekane kama sio kitu na yeye ndie mfadhili wa chuki.

Mimi nakataa nakataa tena kwa herufi kubwa.
CCM ni chama mama embu tuwe mfano. Tiss mulika mangi meza viongozi.
 
Kama mwenyekiti anaonyesha chuki hadharani unafikiri makada wafanye nini
Mwanzo wa ngoma ni lele nyie komaeni kuwatia ndani wapinzani iyo chuki mnayoipanda ikizaa matunda msichukie nazani unakumbuka kipindi cha uchaguzi ulikuwa ukivaa nguo ya kijani ni shida
 
CCM wakimuona mpinzani wanamtamani hata wamuue tu kwasababu amekosoa au ameshauri serikali.

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Haya mambo yanayofanywa na serikali ya CCM ya awamu ya 5 ya kuleta mpasuko kwenye Taifa letu naamini wanaccm wengi wako against nalo.....

Ispokuwa kwa wanaccm wachache, akiwemo Mkuu wa nchi mwenyewe ambaye analishabikia sana jambo hili la mpasuko wa Taifa letu.

Nasema wanaccm wengi hawaridhiki nayo kwa kuwa kama Taifa tuliopokea urithi toka kwa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ya kuwa na Taifa, lenye Umoja na lisilo na ubaguzi wowote wa itikadi za dini, ukabila wala itikadi za kisiasa.

Kwa hiyo haya mambo yanayofanyika na serikali ya CCM ya awamu ya 5 kutumia vyombo vyake vya dola kuhakikisha kuwa vyama vya upinzani havifanyi shughuli zake za kisiasa, ni jambo la hatari sana na linapaswa kukemewa kwa nguvu zote na watanzania wanaopenda kuliona Taifa hili haliingii kwenye Machafuko ya wenyewe kwa wenyewe.
 
Wewe ni nani atakuamini tena humu , maandiko yako ya chuki za kishamba uliyoyaweka humu unadhani tumesahau ?

Ni Mwenyekiti wenu aliyemuagiza Ndugai kuwakomesha wapinzani bungeni , huku yeye akijipa kazi ya kuwakomesha huku nje kwa kulitumia jeshi la polisi atakavyo , unajisahaulisha makusudi ili iweje ?

Endeleeni na siasa zenu za kinyama tuone mwisho wenu .
 
Jamani kuna wana ccm wanaeneza chuki ambayo mm nasema tusipo simama kama chama nakuonyana kwenye milango ya vyumba vya ndani itatusumbua sana kama chama huko tuendako. Nilazima tujuwe rais anasehem yake wakati wasaidiz wanasehem yao.
Chuki huleta hasira, chuki huleta uchungu, chuki huleta vita. Wapo watu wachache sana wanaleta chuki na kumfanya Rais aonekane kama sio kitu na yeye ndie mfadhili wa chuki. Mm nakataa nakataa tena kwa herufi kubwa.
Ccm ni chama mama embu tuwe mfano. Tiss mulika mangi meza viongozi.

Hoja yako ingekuwa na ' mashiko ' zaidi kama tu ungetaja hizo so called ' chuki ' zako zinazoenezwa na wana CCM ambao umeshawatuhumu katika maelezo yako.
 
Haya mambo yanayofanywa na serikali ya CCM ya awamu ya 5 ya kuleta mpasuko kwenye Taifa letu naamini wanaccm wengi wako against nalo.

Nasema wanaccm wengi hawaridhiki nayo kwa kuwa kama Taifa tuliopokea urithi toka kwa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ya kuwa na Taifa, lenye Umoja na kisilo na ubaguzi wowote wa itikadi za dini, ukabila wala itikadi za kisiasa.

Kwa hiyo haya mambo yanayofanyika na serikali ya CCM ya awamu ya 5 kutumia vyombo vyake vya dola kuhakikisha kuwa vyama vya upinzani havifanyi shughuli zake za kisiasa, ni jambo la hatari sana na linapaswa kukemewa kwa nguvu zote na watanzania wanaopenda kuliona Taifa hili haliingii kwenye Machafuko ya wenyewe kwa wenyewe.
Lakini si huyu TumainiEl , huyu analo andiko humu likihamasisha wapinzani wamalizwe , leo anastuka nini tena ?
 
CCM wakimuona mpinzani wanamtamani hata wamuue tu kwasababu amekosoa au ameshauri serikali.

Post sent using JamiiForums mobile app
Mimi namshauri huyu mungu wa Tz awaweke ndani wapinzani wote abaki na misukule yake yote ya 'ndiyooo' waendelee kudanganyana
 
CCM wakimuona mpinzani wanamtamani hata wamuue tu kwasababu amekosoa au ameshauri serikali.

Post sent using JamiiForums mobile app
Mimi namshauri huyu mungu wa Tz awaweke ndani wapinzani wote abaki na misukule yake yote ya 'ndiyooo' waendelee kudanganyanya
 
Nimepitia comments za Facebook page ya gazeti la Mwananchi kuhusu habari ya kifo cha mke wa Mwakyembe,

Watu vifua vyao vimejaa chuki sana. Serikali iji tathmini la sivyo siku viongozi fulani fulani wakipotea duniani kutakuwa na furaha, shangwe na nderemo

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Nchi hii imekua si salama Kwa wapinzani kila kukicha wanakamatwa na kuvamiwa kwenye vikao vyao vya ndani. Wakati wana ccm wakiendelea na shuguli zao za kisiasa kama kawaida. Hakika inaudhi na inatia hasila na mkuu wa nchi yupo tu na yeye anasisitiza kuwashugulikia wapinzani nje ya bunge na kumwagiza spika kuwashugulikia ndani ya bungu. Kwaiyo mtukufu ndio anaeongoza mapambani ya kukabdamiza wapinzani. OK time will tell

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Nimepitia comments za Facebook page ya gazeti la Mwananchi kuhusu habari ya kifo cha mke wa Mwakyembe,

Watu vifua vyao vimejaa chuki sana. Serikali iji tathmini la sivyo siku viongozi fulani fulani wakipotea duniani kutakuwa na furaha, shangwe na nderemo

Post sent using JamiiForums mobile app
Kama wanaoshabikia upinzani hawatakiwi hapa Tz tena wakiwa hai, sasa Leo hii akifa huyu wa CCM lazima watu wafanye sherehe tena kubwa haswa.

Kuna wengine wanaomba waombewe sasa kila mtu anamuombea analotaka liwe
 
Acha kuwatuhumu wanaccm,mfadhiri mkuu wa chuki na visasi ni yule aliye juu,yeye ndiye aliyetoa maelekezo ya kuwapiga marufuku wabunge wa ccm wasiwajulie hali wapinzani wapatapo matatizo,alikemea hadharani kitendo cha mbunge wa ccm kutoa muda wake wa kuongea bungeni kwa mbunge wa upinzani.

Aliye juu ya ufalme alitamka hadharani kumshughulikia kila ampingaye ndani ya dk. 5,hataki kabisa kuguswa kwa namna yoyote ile huku akihoji waathirika wa tetemeko wamemkosea nini Mungu hadi majanga yote kuanzia Ukimwi, tetemeko,katerero, mto ngono na kila aina ya uchafu viwe kwao?

Usitafute kisingizio, kwa kauli ya aliye juu tena huku akituhakikishia kuwa yeye ndiye anayejua siri za nchi hii,alituambia kuwa masheikh wa uamsho ndiyo wanaofanya uhalifu huko kibiti na kwamba sare za JWT zilizokamatwa zina mafungamano na ugaidi wa kibiti.Hakuishia hapo,alihoji kwa nini wafe ccm tu? Kwa maoni yake ni kwamba mauwaji ya kibiti ni ya kiitikadi na kwamba kwa kauli yake anaamsha hisia za chuki za kiitikadi.

Ni upuuzi wa viwango vya kimakinikia kuwa na kiongozi anayehubiri migawanyiko, badala ya kuliunganisha taifa, yupo mstari wa mbele kulifitinisha ili yeye atokee "fent fot" kwenye magazeti.
 
Jamani kuna wana ccm wanaeneza chuki ambayo mm nasema tusipo simama kama chama nakuonyana kwenye milango ya vyumba vya ndani itatusumbua sana kama chama huko tuendako. Nilazima tujuwe rais anasehem yake wakati wasaidiz wanasehem yao.
Chuki huleta hasira, chuki huleta uchungu, chuki huleta vita. Wapo watu wachache sana wanaleta chuki na kumfanya Rais aonekane kama sio kitu na yeye ndie mfadhili wa chuki. Mm nakataa nakataa tena kwa herufi kubwa.
Ccm ni chama mama embu tuwe mfano. Tiss mulika mangi meza viongozi.

Ungeanza na Mwenyekiti wako wa Chama Cha Makinikia. Ndiyo aliyeanzisha chuki,visasi na ubaguzi.
 
Back
Top Bottom