Ashampoo burning
JF-Expert Member
- May 12, 2023
- 1,298
- 3,936
Nelson Sakaguchi, mkurugenzi wa benki moja kubwa zaidi nchini Brazil, alipokea simu iliyobadilisha maisha yake. Upande wa pili wa simu alikuwa Gavana wa Benki Kuu ya Nigeria, na alitaka kukuza nchi kwa kujenga uwanja mkubwa wa ndege ambao haujawahi kuonekana nchini humo. Mradi huo ungetumia gharama ya dola milioni 242 na Nelson angeahidiwa kamisheni ya dola milioni 10 kwa kuwekeza kwenye mradi huo. Walikutana London, na Nelson akashikana mikono na Gavana, Naibu Gavana na Mkurugenzi wa Usafiri wa Anga. Walimwonyesha mipango yote ya biashara, maelezo na wakajadili miundombinu yote. Nelson alishawishika kabisa, wakashikana mikono na kufunga dili. Uwekezaji wa ushindi mkubwa kwa Nelson. Kulikuwa na tatizo moja tu – yote yalikuwa uongo.
Hii ndiyo hadithi ya ajabu ya jinsi mhalifu mmoja mwerevu zaidi katika historia aliuza uwanja wa ndege wa bandia kwa dola milioni 242.
Hii ndiyo hadithi ya ajabu ya jinsi mhalifu mmoja mwerevu zaidi katika historia aliuza uwanja wa ndege wa bandia kwa dola milioni 242.