Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,700
- 7,422
Imeibuka hofu kubwa inayowatesa watu kiakili. Hofu hii inajulikana kama Koro syndrome, inayomfanya mtu kuamini kuwa sehemu nyeti za mwili wake zinapotea akiguswa bega lake!
Kwa mtu aliyeokoka, anayemjua Mungu na kusimama katika kweli ya Neno lake, hofu ya aina hii haina nafasi kabisa ndani yake. Imani thabiti inamfanya mtu aliyeokoka kuwa imara, asiyepeperushwa na upepo wa hofu.
Kwanini mtu aliyeokoka hababaishwi na Koro Syndrome?
1. Mungu hakutupa roho ya hofu, bali ya nguvu, upendo na moyo wa kiasi (2 Timotheo 1:7). Mkristo haongozwi na hisia za hofu bali na Roho Mtakatifu aliye ndani yake.
2. Koro Syndrome inapoingia katikati ya watu huambatana na imani potofu za kishirikina. Mtu aliyeokoka, hakuna nguvu za giza au za kichawi zinazoweza kumdhuru, kwakuwa anatembea chini ya ulinzi wa Mungu.
Maandiko yanasema "hapana uchawi juu ya Yakobo, wala uganga juu ya Israeli (Hesabu 23:23). Kwahiyo hata kama Koro Syndrome itakuja kishirikina, haimbabaishi mtu aliyeokoka kwa sababu ana silaha za kiroho zenye nguvu ya kubomoa mishale ya moto ya shetani. "Silaha za vita vyetu si za mwili bali zina uwezo katika Mungu kubomoa ngome..." (2 Wakorintho 10:4-5). Mawazo ya hofu hubomolewa kwa Neno la Mungu na Jina la Yesu.
3. Mtu aliyeokoka, anakaa ndani ya Yesu na Yesu anakaa ndani yake. "Yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye ulimwenguni"(1 Yohana 4:4). Nguvu ya Mungu ndani ya mtu aliyeokoka ni kubwa kuliko hofu ya aina yoyote.
Kama umeokoka, kumbuka points hizo, utembee kifua mbele bila kujali hata mtu akikugusa bega!
Na kama hujaokoka, amua leo kutubu dhambi zako zote na kuziacha, na ukubali Yesu awe Bwana na Mwokozi wako kuanzia leo. Ukifanya hivyo you will be free from Koro Syndrome induced by psychological, cultural, or satanic anxiety (John 8:36).
Barikiwa!
Kwa mtu aliyeokoka, anayemjua Mungu na kusimama katika kweli ya Neno lake, hofu ya aina hii haina nafasi kabisa ndani yake. Imani thabiti inamfanya mtu aliyeokoka kuwa imara, asiyepeperushwa na upepo wa hofu.
Kwanini mtu aliyeokoka hababaishwi na Koro Syndrome?
1. Mungu hakutupa roho ya hofu, bali ya nguvu, upendo na moyo wa kiasi (2 Timotheo 1:7). Mkristo haongozwi na hisia za hofu bali na Roho Mtakatifu aliye ndani yake.
2. Koro Syndrome inapoingia katikati ya watu huambatana na imani potofu za kishirikina. Mtu aliyeokoka, hakuna nguvu za giza au za kichawi zinazoweza kumdhuru, kwakuwa anatembea chini ya ulinzi wa Mungu.
Maandiko yanasema "hapana uchawi juu ya Yakobo, wala uganga juu ya Israeli (Hesabu 23:23). Kwahiyo hata kama Koro Syndrome itakuja kishirikina, haimbabaishi mtu aliyeokoka kwa sababu ana silaha za kiroho zenye nguvu ya kubomoa mishale ya moto ya shetani. "Silaha za vita vyetu si za mwili bali zina uwezo katika Mungu kubomoa ngome..." (2 Wakorintho 10:4-5). Mawazo ya hofu hubomolewa kwa Neno la Mungu na Jina la Yesu.
3. Mtu aliyeokoka, anakaa ndani ya Yesu na Yesu anakaa ndani yake. "Yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye ulimwenguni"(1 Yohana 4:4). Nguvu ya Mungu ndani ya mtu aliyeokoka ni kubwa kuliko hofu ya aina yoyote.
Kama umeokoka, kumbuka points hizo, utembee kifua mbele bila kujali hata mtu akikugusa bega!
Na kama hujaokoka, amua leo kutubu dhambi zako zote na kuziacha, na ukubali Yesu awe Bwana na Mwokozi wako kuanzia leo. Ukifanya hivyo you will be free from Koro Syndrome induced by psychological, cultural, or satanic anxiety (John 8:36).
Barikiwa!