Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,319
- 33,124
Mbunge wa Ukonga (CCM), Eugen Mwaiposa, ameitaka Serikali kuwapima akili watahiniwa wa kidato cha nne waliaondika matusi na nyimbo za bongo fleva katika karatasi za majibu ya mitihani yao ya taifa ya kuhitimu elimu ya sekondari.
Mwaiposa alitoa wito huo jana bungeni wakati katika swali lake la nyongeza kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
Alisema kitendo cha wanafunzi kuandika matusi ni kisicho cha kawaida hivyo haiwezekani kuwaacha bila ya kujua matatizo yao.
Akijibu hoja hiyo, Waziri wa Wizara hiyo, Dk. Shukuru Kawambwa alithibitisha kuziona baadhi ya karatasi za wanafunzi ambazo ziliandikwa matusi tofauti na alivyotarajia.
Hata hivyo, Dk. alisema Serikali imeamua kutowafutia matokea yote wanafunzi hao na badala yake imefuta kwa masomo ambayo waliandika matusi na nyimbo hizo.
Naomba niwaambie kuwa tumejipanga kuikomesha tabia hii kuanzia kipindi cha mwaka 2012, alisema
Awali katika swali la msingi, Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Susan Lyimo, alitaka kujua Serikali imechukua hatua gani kwa walimu waliosaidia kufanya udanganyifu kwenye mitihani ya wanafunzi wa darasa la saba katika mitihani ya mwaka 2011.
Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Philipo Mulugo alisema serikali imekuwa ikichukua hatua mara tu yanapojitokeza matatizo kama hayo.
Mulugo alisema kutokana na udanganyifu wa mitahi hiyo, wizara imewashusha vyeo baadhi ya walimu ikiwa ni pamoja na kuwazuia kusimamia mitihani.
Alitolewa mfano kuwa katika adhabu hiyo, walimu nane wa Mufindi walikumbwa na adhabu, Mbeya watano, Ruvuma nane Jiji la Dar es Salaam 18 .
Alisema serikali iliunda tume kwa ajili ya kuchunguza jambo hilo kwa kina na majibu ya tume hiyo yanatarajia kutolewa Aprili mwaka huu na kutoa adhabu kali kwa kwa wahusika.
Katika hatua nyingine; Mulugo amewataka wabunge na wanaharakati kuacha tabia ya kuwaonea huruma wanafunzi wanaopewa adhabu kutokana na udanganyifu.
Naomba mtuache tufanyekazi nyinyi ndiyo mnaowaonea huruma hawa watoto napenda kuwaambia kuwa adhabu za kufutia matokea na kuwasimamisha kutofanya mitihani zitaendelea kwa wanaobainika, alisema
CHANZO: NIPASHE
Mwaiposa alitoa wito huo jana bungeni wakati katika swali lake la nyongeza kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
Alisema kitendo cha wanafunzi kuandika matusi ni kisicho cha kawaida hivyo haiwezekani kuwaacha bila ya kujua matatizo yao.
Akijibu hoja hiyo, Waziri wa Wizara hiyo, Dk. Shukuru Kawambwa alithibitisha kuziona baadhi ya karatasi za wanafunzi ambazo ziliandikwa matusi tofauti na alivyotarajia.
Hata hivyo, Dk. alisema Serikali imeamua kutowafutia matokea yote wanafunzi hao na badala yake imefuta kwa masomo ambayo waliandika matusi na nyimbo hizo.
Naomba niwaambie kuwa tumejipanga kuikomesha tabia hii kuanzia kipindi cha mwaka 2012, alisema
Awali katika swali la msingi, Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Susan Lyimo, alitaka kujua Serikali imechukua hatua gani kwa walimu waliosaidia kufanya udanganyifu kwenye mitihani ya wanafunzi wa darasa la saba katika mitihani ya mwaka 2011.
Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Philipo Mulugo alisema serikali imekuwa ikichukua hatua mara tu yanapojitokeza matatizo kama hayo.
Mulugo alisema kutokana na udanganyifu wa mitahi hiyo, wizara imewashusha vyeo baadhi ya walimu ikiwa ni pamoja na kuwazuia kusimamia mitihani.
Alitolewa mfano kuwa katika adhabu hiyo, walimu nane wa Mufindi walikumbwa na adhabu, Mbeya watano, Ruvuma nane Jiji la Dar es Salaam 18 .
Alisema serikali iliunda tume kwa ajili ya kuchunguza jambo hilo kwa kina na majibu ya tume hiyo yanatarajia kutolewa Aprili mwaka huu na kutoa adhabu kali kwa kwa wahusika.
Katika hatua nyingine; Mulugo amewataka wabunge na wanaharakati kuacha tabia ya kuwaonea huruma wanafunzi wanaopewa adhabu kutokana na udanganyifu.
Naomba mtuache tufanyekazi nyinyi ndiyo mnaowaonea huruma hawa watoto napenda kuwaambia kuwa adhabu za kufutia matokea na kuwasimamisha kutofanya mitihani zitaendelea kwa wanaobainika, alisema
CHANZO: NIPASHE