Walinzi shirikishi wapigwa ‘stop’

Walinzi shirikishi wapigwa ‘stop’

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,618
Reaction score
9,607
Mkuu wa Wilaya ya ilala, Sofia Mjema amemuagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala kuwachukulia hatua askari wake wanaochukua rushwa kutoka kwa waendesha bodaboda.

Pia, amesema kuanzia jana vikundi vya ulinzi shirikishi visiwakamate waendesha bodaboda hao, hivyo jukumu hilo litafanywa na wataalamu ambao ni polisi. Hatua hiyo imekuja baada ya waendesha bodaboda wa wilaya hiyo kulalamika kuwa, kuna baadhi ya polisi wamekuwa wakiwaomba rushwa na kuwachapa viboko wanapokuwa wanaendesha pikipiki.

Mjema alisema polisi wanatakiwa wafanye kazi kwa weledi, hivyo yeyote atakayebainika achukuliwe hatua kali za kisheria. “Nasikia wengine wanawachapa viboko, hivyo namuagiza kamanda wa polisi kuwachukulia hatua haraka wahusika wote,” aliagiza Mjema.

Pia, alisema ulinzi shirikishi hawatakiwi kuwakamata waendesha bodaboda hao, hivyo kutokana na kushindwa kazi hivyo itafanywa na polisi.

Mjema alisema vikundi vya ulinzi shirikishi vinatakiwa kufanya kazi zingine, ikiwamo kuwafichua wahalifu.

Pia, walilalamikia Madalali wa Kampuni ya Tambaza Action Mark, wanapotaka kuwakamata kuwa wanawkimbiza au kumkumbatia jambo ambalo linasababisha ajali.

“Nilishaongea na kiongozi wa Kampuni ya Tambaza atoe elimu kwa watumishi wake, wanapokaa sehemu husika wanatakiwa kuambatana na polisi ndiye mwenye mamlaka ya kuwakamata bodaboda siyo wao,” alisema Mjema.

Mkuu wa Kikosi cha Polisi Mkoa wa Ilala, Mashishanga Mwambambiti aliwataka waendesha bodaboda hao kumpelekea majina ya polisi wanaochukua rushwa huku wakiwa na vielelezo ikiwamo kuwapiga picha.

Aalisema bodaboda hao watakapoleleka vielelezo atavifanyia kazi kwa kuwa anayo mamlaka ya kuwachukulia hatua polisi hao.

Mwakilishi wa Umoja wa Bodaboda wa Wilaya hiyo, Peter Kassalu alimuomba Mjema kuwasajili ili walipe kodi ya mapato. Ilala ina bodaboda 50,000.

mwananchi
 
Naunga Mkono hoja...
Amri iliyotolewa na dc wa ikala ifatwe ..
Bado tnasubiri tamko la dc wa kino naye

Ova
 
Hata Alhamisi iliyopita...
ITV walikuwa na kipindi cha kipima joto hilo suala la ulinzi shirikishi liliongelewa na kupigwa marufuku na mamlaka husika... Kutojihusisha na ukamataji hatarishi wa boda boda...


Cc: mahondaw
 
Na bodaboda pia waache kutoa usafiri kwa waalifu, kwani kuna baadhi ya matukio inasemekana waalifu wanapelekwa na bodaboda na kutokomea na bodaboda. Ingawaje waalifu wanaweza kumiliki bodaboda.

Ni vyema bodaboda sio mualifu, akiona mteja wake anatenda ualifu ni vyema kumuacha badala ya kumsubiri.
 
Back
Top Bottom