Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,620
- 46,261
Kuna Balozi anayejifanyia mambo tofauti na mila, desturi na nidhamu. Anaingia hadi mitaani mwenyewe kibinafsi kuleta siha njema. Walinda legasi wanapiga makofi, wanasema kufuata protokali ni urasimu.
Kuna msemaji na spika ya chama ambaye anawaamuru na kutoa maagizo kwa wenye mamlaka juu ya watu wote na anashangiliwa sana na walinda legasi, wanasema huko ndiko kutatua kero, kila hatua anayopiga anashangiliwa nao na kuitwa mbunifu.
Pacha aliyewekwa kuondoa giza ndio kwanza giza limezidi ila hakuna miongoni mwa walinda legasi anayedai kuwajibishwa kwake au hata kuuliza lolote. Wanadai Kipara ndiye aendelee kuwajibishwa hata kama hayupo tena! Mpaka lini, sina uhakika.
Kuna msemaji na spika ya chama ambaye anawaamuru na kutoa maagizo kwa wenye mamlaka juu ya watu wote na anashangiliwa sana na walinda legasi, wanasema huko ndiko kutatua kero, kila hatua anayopiga anashangiliwa nao na kuitwa mbunifu.
Pacha aliyewekwa kuondoa giza ndio kwanza giza limezidi ila hakuna miongoni mwa walinda legasi anayedai kuwajibishwa kwake au hata kuuliza lolote. Wanadai Kipara ndiye aendelee kuwajibishwa hata kama hayupo tena! Mpaka lini, sina uhakika.